Uhakiki huu ni wa msingi wa Tamthiliya ya Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe. Umezingatia zaidi kipengele cha maudhui.
Uhakiki huu umetumia picha kutoka katika mazingira yaliyotuzunguka ili kukazia maarifa kwa wanafunzi.
Mwalimu au mwanafunzi wa fasihi anakaribishwa kutumia uwasilishaji huu.
Kwa mawasiliano zaidi unaweza nitafuta kwa mawasiliano hayo hapo juu.
2. Utangulizi
Ngoswe penzi kitovu cha uzembe ni tamthiliya maarufu sana ambayo imewahi
kuigizwa katika redio Tanzania na katika majukwaa mbalimbali hapa nchini. Ni
tamthiliya ambayo imeundwa vyema katika vipengele vya fani na maudhui.
Ameteua lugha nzuri na yenye mvuto kwa wasomaji yenye mbinu za kifasihi
zilizosheheni, muundo wenye mtiririko mzuri, unaoakisi kuanza kuchipuka kwa
matukio mpaka kilele cha matukio. Wahusika wamebeba vyema uhusika wao
mfano Ngoswe.
Ameibua dhamira kuhusu mambo yanayoigusa jamii ya leo kama vile uzembe,
madhara ya ulevi, uzembe kazini, suala la matabaka kati ya mjini na vijijini.
Mtazamo, falsafa na msimamo wake ni kulenga kuibadilisha jamii na kuleta
maendeleo.
5. Ukosefu wa Elimu
Mwandishi anatumia wahusika wake kuonesha tatizo la
kukosekana kwa elimu miongoni mwa wanajamii.
Mhusika Mzee mitomingi hajui kusoma. Hii inaonekana
pale Ngoswe anapomkabidhi kiitambulisho asome lakini
anashindwa.
Pia watoto katika kijiji kile hawaendi shule. Watoto wa
Mitomingi na wale wa Mama Mjane hawasomi bali
hufanya kazi za nyumbani na shamba tu.
Kwa upande mwingine, mhusika Jimbi kutofahamu tarehe
yake ya kuzaliwa ni ishara tosha kwamba katika kijiji hiki
watu hawafahamu kusoma na kuandika.
Mwisho wahusika kukataa kuhesabiwa kwa kuwa
waliamini kuwa kuhesabiwa ni kurogwa. Hii inadhihirisha
kuwa wananchi hawajui maana na umuhimu wa sensa.
6. Mapenzi ya Ulaghai
Mapenzi ya ulaghai ni yale ambayo
mmoja kati ya wapenzi anakuwa hana
ukweli katika uhusiano husika.
Mwandishi wa tamthiliya hii anaonesha
uwepo wa mapenzi ya ulaghai miongoni
mwa vijana.
Anamtumia mhusika Ngoswe
anayemlaghai Mazoea ili aweze kutoroka
kwa wazazi wake.
Katika jamii yetu kuna vijana walaghai wa
mapenzi.
7. Imani Potofu
Dhamira hii inaibuka kupitia Mama Mjane
anayeficha watoto ili wasihesabiwe.
Katika mawazo yake aliamini kuwa
wanaohesabu watu ni wachawi. Mbali na
hilo mhusika huyu aliamini kuwa
mumewe alikufa kwa kurogwa.
Imana hizi zipo miongoni mwa
wanajamii. Hapa mwandishi anaiakisi
jamii kwa jicho pevu na kuikosoa.
8. Athari za Ulevi
Wanaume wengi hujihusisha na vitendo vya ulevi
wa pombe.
Tabia hii inaathari nyingi kwa familia na jamii kwa
ujumla. Mwandishi anamtumia mhusika Ngoswe
kuonesha athari ya pombe.
Hii imejitokeza pale Ngoswe anapochoma
karatasi za kuhesabia watu.
Pia Ngoswe na Mitomingi kushindwa kufanya
kazi siku iliyofuata.
Hii inadhihirisha namna pombe inavyoweza kuwa
chachu ya uzembe na kurudisha maendeleo
nyuma.
9. Umasikini
Mfumo mzima wa maisha katika kijiji kile
unaonesha kuwa wanachi wa kijiji kile ni
masikini.
Kukosekana kwa elimu, kukosekana kwa
huduma za afya, shule kuwa mbali na
makazi ya watu na imani za kishirikina ni
moja ya mambo yanayoashiria umasikini.
Mwandishi anasawili hali halisi ya vijiji
vingi nchini Tanzania kupitia hali hizi.
10. Mapenzi Chanzo cha Uzembe
Dhamira hii inajidhihirisha kupitia mhusika
Ngoswe ambaye anapoteza takwimu za
serikali kwa sababu za mapenzi.
Vijana wengi kwenye jamii yetu hupoteza
muda mwingi kwenye masuala ya
mapenzi.
Mwandishi anawakumbusha vijana juu ya
hatari ya kuchanganya mambo mawili
wakti mmoja kupitia dhamira hii.
11. Nafasi ya Mwanamke katika Jamii
Mlezi wa familia: mhusika Mama Mazoea
na Mama Mainda
Kama kiumbe asiye na maamuzi sahihi:
kitendo cha mama Mazoea kushindwa
kuwakanya Mazoea na Ngoswe
alipowakuta Kisimani.
Kama kiumbe asiye na msimamo:
Mazoea
Kama mtu anayedharauliwa: Kitendo cha
Mitomingi kumfokea mke wake mbele ya
mgeni
12. Ndoa za Mitala
Utamaduni huu umebainishwa kupitia
familia nyingi ndani ya tamthiliya hii.
Mwandishi anaonesha kuwa wanaume
wengi katika kijiji kile wameoa mke zaidi
ya mmoja.
Hajaonesha wazi kuwa utamaduni huu ni
mbaya ingawa haushauriwi sana katika
jamii.
Hii ni kwa sababu za kiuchumi na kiafya
(kuenea kwa magonjwa ya zinaa)
13. Kukosekana kwa Huduma za Kijamii
Huduma muhimu za kijamii ni kama
shule na hospitali.
Katika mazungumzo ya wahusika
inabainishwa kwamba huduma za kijamii
kama shule, hospitali na huduma
nyingine za kijamii zipo mbali na makazi
ya watu.
Hii inadhihirisha ukosefu wa huduma za
kijamii jambo linaloashirikia umasikini
miongoni mwa wananchi katika kijiji kile.
15. Ujumbe
Mapenzi ni chanzo cha uzembe katika jamii yetu
Kukosekana kwa elimu kunarudisha nyuma
maendeleo
Imani za kishirikina ni adui wa maendeleo
Ni vizuri kufikiri kabla ya kutenda
Pombe ni adui mkubwa wa ustawi wa maendeleo
ya binadamu
Mshika mawili moja humponyoka
Njia ya muongo ni fupi. Mazoea kumdanganya
mama yake.
Kuwa na msimamo husaidia kuepuka vishawishi.
16. Migogoro
Mgogoro kati ya Jimbi na Mitomingi baada ya
jimbi kusahau siku ya kuhesabiwa akatuma
watoto shambani.
Mgogoro kati ya Ngoswe na Mzee Jimbi
wakigombania idadi ya miaka ya mzee Jimbi
Mgogoro kati ya mazoea na Mama Mazoea
baada ya mazoea kuchelewa kurudi mtoni
Mgogoro kati ya Mitomingi na wakinamama
wajane baada ya kuficha watoto wasihesabiwe
Mgogoro nafsia aliokuwa nao ngoswe baada
ya kumkaribisha mama Mazoea ndani akidhani
ni Mazoea.
Mgogoro nafsia aliokuwa nao Ngoswe baada
ya kuchoma karatasi kwa ulevi
17. Muendelezo…
Mgogoro kati ya Mzee Mitomingi na Mama
Mazoea baada ya Mazoea kuitwa na baba yake
kisha akadanganya kuwa alikuwa anamsuka mama
yake.
Mgogoro kati ya Mitomingi na wake zake baada ya
Mazoea kutoroshwa.
Mgogoro kati ya Ngoswe na Mitomingi
Mgogoro wa nafsi aliokuwa nao Ngoswe baada ya
karatasi zake kuchomwa moto.
Mgogoro kati ya Ngoswe, Mitomingi na Serikali.
Mgogoro wa kitabaka kati ya mijini na vijijini
18. Falsafa
Mwandishi anaamini kuwa ni vigumu kwa
mwandamu kuchanganya mapenzi na kazi.
Anafafanua kwamba katika hali kama hiyo
kimoja kitafanywa vizuri zaidi ya kingine.
Anamtumia mhusika Ngoswe aliyepoteza
hesabu ya watu kwa sababu za uzembe wa
kimapenzi.
Pia anaamini kuwa elimu inanafasi ya
kutatua matatizo ya kijamii. Jamii ikielimika
basi maendeleo yatatokea kwa urahisi.
19. Mtazamo na Msimamo
Mwandishi anaiangalia jamii katika
mtazamo yakinifu.
Anabainisha masuala yanayoigusa jamii
waziwazi.
Mwisho anapendekeza masuluhisho ya
masuala hayo.
Huu ni msimamo wa kimapinduzi kwa
kuwa unalengo la kujenga jamii mpya.