SlideShare a Scribd company logo
1 of 20
UHAKIKI
wa
NGOSWE
Penzi Kitovu
cha Uzembe
Mussa Shekinyashi
mussashaky@gmail.com
0714 80 75 65
0743 98 98 29
Utangulizi
 Ngoswe penzi kitovu cha uzembe ni tamthiliya maarufu sana ambayo imewahi
kuigizwa katika redio Tanzania na katika majukwaa mbalimbali hapa nchini. Ni
tamthiliya ambayo imeundwa vyema katika vipengele vya fani na maudhui.
Ameteua lugha nzuri na yenye mvuto kwa wasomaji yenye mbinu za kifasihi
zilizosheheni, muundo wenye mtiririko mzuri, unaoakisi kuanza kuchipuka kwa
matukio mpaka kilele cha matukio. Wahusika wamebeba vyema uhusika wao
mfano Ngoswe.
 Ameibua dhamira kuhusu mambo yanayoigusa jamii ya leo kama vile uzembe,
madhara ya ulevi, uzembe kazini, suala la matabaka kati ya mjini na vijijini.
Mtazamo, falsafa na msimamo wake ni kulenga kuibadilisha jamii na kuleta
maendeleo.
Vipengele
vya
Maudhui
Dhamira
Ukosefu wa Elimu
 Mwandishi anatumia wahusika wake kuonesha tatizo la
kukosekana kwa elimu miongoni mwa wanajamii.
Mhusika Mzee mitomingi hajui kusoma. Hii inaonekana
pale Ngoswe anapomkabidhi kiitambulisho asome lakini
anashindwa.
 Pia watoto katika kijiji kile hawaendi shule. Watoto wa
Mitomingi na wale wa Mama Mjane hawasomi bali
hufanya kazi za nyumbani na shamba tu.
 Kwa upande mwingine, mhusika Jimbi kutofahamu tarehe
yake ya kuzaliwa ni ishara tosha kwamba katika kijiji hiki
watu hawafahamu kusoma na kuandika.
 Mwisho wahusika kukataa kuhesabiwa kwa kuwa
waliamini kuwa kuhesabiwa ni kurogwa. Hii inadhihirisha
kuwa wananchi hawajui maana na umuhimu wa sensa.
Mapenzi ya Ulaghai
 Mapenzi ya ulaghai ni yale ambayo
mmoja kati ya wapenzi anakuwa hana
ukweli katika uhusiano husika.
 Mwandishi wa tamthiliya hii anaonesha
uwepo wa mapenzi ya ulaghai miongoni
mwa vijana.
 Anamtumia mhusika Ngoswe
anayemlaghai Mazoea ili aweze kutoroka
kwa wazazi wake.
 Katika jamii yetu kuna vijana walaghai wa
mapenzi.
Imani Potofu
 Dhamira hii inaibuka kupitia Mama Mjane
anayeficha watoto ili wasihesabiwe.
 Katika mawazo yake aliamini kuwa
wanaohesabu watu ni wachawi. Mbali na
hilo mhusika huyu aliamini kuwa
mumewe alikufa kwa kurogwa.
 Imana hizi zipo miongoni mwa
wanajamii. Hapa mwandishi anaiakisi
jamii kwa jicho pevu na kuikosoa.
Athari za Ulevi
 Wanaume wengi hujihusisha na vitendo vya ulevi
wa pombe.
 Tabia hii inaathari nyingi kwa familia na jamii kwa
ujumla. Mwandishi anamtumia mhusika Ngoswe
kuonesha athari ya pombe.
 Hii imejitokeza pale Ngoswe anapochoma
karatasi za kuhesabia watu.
 Pia Ngoswe na Mitomingi kushindwa kufanya
kazi siku iliyofuata.
 Hii inadhihirisha namna pombe inavyoweza kuwa
chachu ya uzembe na kurudisha maendeleo
nyuma.
Umasikini
 Mfumo mzima wa maisha katika kijiji kile
unaonesha kuwa wanachi wa kijiji kile ni
masikini.
 Kukosekana kwa elimu, kukosekana kwa
huduma za afya, shule kuwa mbali na
makazi ya watu na imani za kishirikina ni
moja ya mambo yanayoashiria umasikini.
 Mwandishi anasawili hali halisi ya vijiji
vingi nchini Tanzania kupitia hali hizi.
Mapenzi Chanzo cha Uzembe
 Dhamira hii inajidhihirisha kupitia mhusika
Ngoswe ambaye anapoteza takwimu za
serikali kwa sababu za mapenzi.
 Vijana wengi kwenye jamii yetu hupoteza
muda mwingi kwenye masuala ya
mapenzi.
 Mwandishi anawakumbusha vijana juu ya
hatari ya kuchanganya mambo mawili
wakti mmoja kupitia dhamira hii.
Nafasi ya Mwanamke katika Jamii
 Mlezi wa familia: mhusika Mama Mazoea
na Mama Mainda
 Kama kiumbe asiye na maamuzi sahihi:
kitendo cha mama Mazoea kushindwa
kuwakanya Mazoea na Ngoswe
alipowakuta Kisimani.
 Kama kiumbe asiye na msimamo:
Mazoea
 Kama mtu anayedharauliwa: Kitendo cha
Mitomingi kumfokea mke wake mbele ya
mgeni
Ndoa za Mitala
 Utamaduni huu umebainishwa kupitia
familia nyingi ndani ya tamthiliya hii.
 Mwandishi anaonesha kuwa wanaume
wengi katika kijiji kile wameoa mke zaidi
ya mmoja.
 Hajaonesha wazi kuwa utamaduni huu ni
mbaya ingawa haushauriwi sana katika
jamii.
 Hii ni kwa sababu za kiuchumi na kiafya
(kuenea kwa magonjwa ya zinaa)
Kukosekana kwa Huduma za Kijamii
 Huduma muhimu za kijamii ni kama
shule na hospitali.
 Katika mazungumzo ya wahusika
inabainishwa kwamba huduma za kijamii
kama shule, hospitali na huduma
nyingine za kijamii zipo mbali na makazi
ya watu.
 Hii inadhihirisha ukosefu wa huduma za
kijamii jambo linaloashirikia umasikini
miongoni mwa wananchi katika kijiji kile.
Vipengele vingine
vya
Maudhui
Ujumbe
 Mapenzi ni chanzo cha uzembe katika jamii yetu
 Kukosekana kwa elimu kunarudisha nyuma
maendeleo
 Imani za kishirikina ni adui wa maendeleo
 Ni vizuri kufikiri kabla ya kutenda
 Pombe ni adui mkubwa wa ustawi wa maendeleo
ya binadamu
 Mshika mawili moja humponyoka
 Njia ya muongo ni fupi. Mazoea kumdanganya
mama yake.
 Kuwa na msimamo husaidia kuepuka vishawishi.
Migogoro
 Mgogoro kati ya Jimbi na Mitomingi baada ya
jimbi kusahau siku ya kuhesabiwa akatuma
watoto shambani.
 Mgogoro kati ya Ngoswe na Mzee Jimbi
wakigombania idadi ya miaka ya mzee Jimbi
 Mgogoro kati ya mazoea na Mama Mazoea
baada ya mazoea kuchelewa kurudi mtoni
 Mgogoro kati ya Mitomingi na wakinamama
wajane baada ya kuficha watoto wasihesabiwe
 Mgogoro nafsia aliokuwa nao ngoswe baada
ya kumkaribisha mama Mazoea ndani akidhani
ni Mazoea.
 Mgogoro nafsia aliokuwa nao Ngoswe baada
ya kuchoma karatasi kwa ulevi
Muendelezo…
 Mgogoro kati ya Mzee Mitomingi na Mama
Mazoea baada ya Mazoea kuitwa na baba yake
kisha akadanganya kuwa alikuwa anamsuka mama
yake.
 Mgogoro kati ya Mitomingi na wake zake baada ya
Mazoea kutoroshwa.
 Mgogoro kati ya Ngoswe na Mitomingi
 Mgogoro wa nafsi aliokuwa nao Ngoswe baada ya
karatasi zake kuchomwa moto.
 Mgogoro kati ya Ngoswe, Mitomingi na Serikali.
 Mgogoro wa kitabaka kati ya mijini na vijijini
Falsafa
 Mwandishi anaamini kuwa ni vigumu kwa
mwandamu kuchanganya mapenzi na kazi.
 Anafafanua kwamba katika hali kama hiyo
kimoja kitafanywa vizuri zaidi ya kingine.
 Anamtumia mhusika Ngoswe aliyepoteza
hesabu ya watu kwa sababu za uzembe wa
kimapenzi.
 Pia anaamini kuwa elimu inanafasi ya
kutatua matatizo ya kijamii. Jamii ikielimika
basi maendeleo yatatokea kwa urahisi.
Mtazamo na Msimamo
 Mwandishi anaiangalia jamii katika
mtazamo yakinifu.
 Anabainisha masuala yanayoigusa jamii
waziwazi.
 Mwisho anapendekeza masuluhisho ya
masuala hayo.
 Huu ni msimamo wa kimapinduzi kwa
kuwa unalengo la kujenga jamii mpya.
Asanteni kwa kunisikiliza

More Related Content

What's hot

Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)
Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)
Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)
Mwl. Mapesa Nestory
 

What's hot (20)

Mjengo wa tungo 3
Mjengo wa tungo 3Mjengo wa tungo 3
Mjengo wa tungo 3
 
Uhakiki wa kazi za fasihi andishi
Uhakiki wa kazi za fasihi andishiUhakiki wa kazi za fasihi andishi
Uhakiki wa kazi za fasihi andishi
 
MAENDELEO YA KISWAHILI
MAENDELEO YA KISWAHILIMAENDELEO YA KISWAHILI
MAENDELEO YA KISWAHILI
 
MATUMIZI YA SARUFI
MATUMIZI YA SARUFIMATUMIZI YA SARUFI
MATUMIZI YA SARUFI
 
UTUMIZI WA LUGHA
UTUMIZI WA LUGHAUTUMIZI WA LUGHA
UTUMIZI WA LUGHA
 
Rejesta
RejestaRejesta
Rejesta
 
FASIHI KWA UJUMLA
FASIHI KWA UJUMLAFASIHI KWA UJUMLA
FASIHI KWA UJUMLA
 
MAENDELEO YA FASIHI SIMULIZI
MAENDELEO YA FASIHI SIMULIZIMAENDELEO YA FASIHI SIMULIZI
MAENDELEO YA FASIHI SIMULIZI
 
MAENDELEO YA KISWAHILI TANZANIA
MAENDELEO YA KISWAHILI TANZANIAMAENDELEO YA KISWAHILI TANZANIA
MAENDELEO YA KISWAHILI TANZANIA
 
Kiswahili ni Pijini au Krioli
Kiswahili ni Pijini au KrioliKiswahili ni Pijini au Krioli
Kiswahili ni Pijini au Krioli
 
Mjengo wa tungo
Mjengo wa tungoMjengo wa tungo
Mjengo wa tungo
 
Maendeleo ya kiswahili
Maendeleo ya kiswahiliMaendeleo ya kiswahili
Maendeleo ya kiswahili
 
Chimbuko na Asili ya Kiswahili
Chimbuko na Asili ya KiswahiliChimbuko na Asili ya Kiswahili
Chimbuko na Asili ya Kiswahili
 
Lahaja za kiswahili kwa ujumla
Lahaja za kiswahili kwa ujumlaLahaja za kiswahili kwa ujumla
Lahaja za kiswahili kwa ujumla
 
Utungaji wa kazi za fasihi andishi
Utungaji wa kazi za fasihi andishiUtungaji wa kazi za fasihi andishi
Utungaji wa kazi za fasihi andishi
 
Waingereza na baada ya uhuru
Waingereza na baada ya uhuruWaingereza na baada ya uhuru
Waingereza na baada ya uhuru
 
Tamthilia ni nini?
Tamthilia ni nini?Tamthilia ni nini?
Tamthilia ni nini?
 
USHAIRI WA KISWAHILI
USHAIRI WA KISWAHILIUSHAIRI WA KISWAHILI
USHAIRI WA KISWAHILI
 
Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)
Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)
Chuo kikuu cha mtakatifu agustino (autosaved)
 
Ngeli za nomino
Ngeli za nominoNgeli za nomino
Ngeli za nomino
 

More from mussa Shekinyashi

More from mussa Shekinyashi (9)

Matumizi ya Lugha Kimuktadha
Matumizi ya Lugha KimuktadhaMatumizi ya Lugha Kimuktadha
Matumizi ya Lugha Kimuktadha
 
Tafsiri na ukalimani
Tafsiri na ukalimaniTafsiri na ukalimani
Tafsiri na ukalimani
 
Evolution of Man (form one)
Evolution of Man (form one)Evolution of Man (form one)
Evolution of Man (form one)
 
Public Speaking Tips
Public Speaking TipsPublic Speaking Tips
Public Speaking Tips
 
Sarufi Matamshi (Fonolojia)
Sarufi Matamshi (Fonolojia)Sarufi Matamshi (Fonolojia)
Sarufi Matamshi (Fonolojia)
 
GENDER CONCEPTS - FORM TWO
GENDER CONCEPTS - FORM TWO GENDER CONCEPTS - FORM TWO
GENDER CONCEPTS - FORM TWO
 
CHIMBUKO LA FASIHI
CHIMBUKO LA FASIHICHIMBUKO LA FASIHI
CHIMBUKO LA FASIHI
 
UHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHA
UHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHAUHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHA
UHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHA
 
Semantiki
SemantikiSemantiki
Semantiki
 

Uhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penzi

  • 1. UHAKIKI wa NGOSWE Penzi Kitovu cha Uzembe Mussa Shekinyashi mussashaky@gmail.com 0714 80 75 65 0743 98 98 29
  • 2. Utangulizi  Ngoswe penzi kitovu cha uzembe ni tamthiliya maarufu sana ambayo imewahi kuigizwa katika redio Tanzania na katika majukwaa mbalimbali hapa nchini. Ni tamthiliya ambayo imeundwa vyema katika vipengele vya fani na maudhui. Ameteua lugha nzuri na yenye mvuto kwa wasomaji yenye mbinu za kifasihi zilizosheheni, muundo wenye mtiririko mzuri, unaoakisi kuanza kuchipuka kwa matukio mpaka kilele cha matukio. Wahusika wamebeba vyema uhusika wao mfano Ngoswe.  Ameibua dhamira kuhusu mambo yanayoigusa jamii ya leo kama vile uzembe, madhara ya ulevi, uzembe kazini, suala la matabaka kati ya mjini na vijijini. Mtazamo, falsafa na msimamo wake ni kulenga kuibadilisha jamii na kuleta maendeleo.
  • 5. Ukosefu wa Elimu  Mwandishi anatumia wahusika wake kuonesha tatizo la kukosekana kwa elimu miongoni mwa wanajamii. Mhusika Mzee mitomingi hajui kusoma. Hii inaonekana pale Ngoswe anapomkabidhi kiitambulisho asome lakini anashindwa.  Pia watoto katika kijiji kile hawaendi shule. Watoto wa Mitomingi na wale wa Mama Mjane hawasomi bali hufanya kazi za nyumbani na shamba tu.  Kwa upande mwingine, mhusika Jimbi kutofahamu tarehe yake ya kuzaliwa ni ishara tosha kwamba katika kijiji hiki watu hawafahamu kusoma na kuandika.  Mwisho wahusika kukataa kuhesabiwa kwa kuwa waliamini kuwa kuhesabiwa ni kurogwa. Hii inadhihirisha kuwa wananchi hawajui maana na umuhimu wa sensa.
  • 6. Mapenzi ya Ulaghai  Mapenzi ya ulaghai ni yale ambayo mmoja kati ya wapenzi anakuwa hana ukweli katika uhusiano husika.  Mwandishi wa tamthiliya hii anaonesha uwepo wa mapenzi ya ulaghai miongoni mwa vijana.  Anamtumia mhusika Ngoswe anayemlaghai Mazoea ili aweze kutoroka kwa wazazi wake.  Katika jamii yetu kuna vijana walaghai wa mapenzi.
  • 7. Imani Potofu  Dhamira hii inaibuka kupitia Mama Mjane anayeficha watoto ili wasihesabiwe.  Katika mawazo yake aliamini kuwa wanaohesabu watu ni wachawi. Mbali na hilo mhusika huyu aliamini kuwa mumewe alikufa kwa kurogwa.  Imana hizi zipo miongoni mwa wanajamii. Hapa mwandishi anaiakisi jamii kwa jicho pevu na kuikosoa.
  • 8. Athari za Ulevi  Wanaume wengi hujihusisha na vitendo vya ulevi wa pombe.  Tabia hii inaathari nyingi kwa familia na jamii kwa ujumla. Mwandishi anamtumia mhusika Ngoswe kuonesha athari ya pombe.  Hii imejitokeza pale Ngoswe anapochoma karatasi za kuhesabia watu.  Pia Ngoswe na Mitomingi kushindwa kufanya kazi siku iliyofuata.  Hii inadhihirisha namna pombe inavyoweza kuwa chachu ya uzembe na kurudisha maendeleo nyuma.
  • 9. Umasikini  Mfumo mzima wa maisha katika kijiji kile unaonesha kuwa wanachi wa kijiji kile ni masikini.  Kukosekana kwa elimu, kukosekana kwa huduma za afya, shule kuwa mbali na makazi ya watu na imani za kishirikina ni moja ya mambo yanayoashiria umasikini.  Mwandishi anasawili hali halisi ya vijiji vingi nchini Tanzania kupitia hali hizi.
  • 10. Mapenzi Chanzo cha Uzembe  Dhamira hii inajidhihirisha kupitia mhusika Ngoswe ambaye anapoteza takwimu za serikali kwa sababu za mapenzi.  Vijana wengi kwenye jamii yetu hupoteza muda mwingi kwenye masuala ya mapenzi.  Mwandishi anawakumbusha vijana juu ya hatari ya kuchanganya mambo mawili wakti mmoja kupitia dhamira hii.
  • 11. Nafasi ya Mwanamke katika Jamii  Mlezi wa familia: mhusika Mama Mazoea na Mama Mainda  Kama kiumbe asiye na maamuzi sahihi: kitendo cha mama Mazoea kushindwa kuwakanya Mazoea na Ngoswe alipowakuta Kisimani.  Kama kiumbe asiye na msimamo: Mazoea  Kama mtu anayedharauliwa: Kitendo cha Mitomingi kumfokea mke wake mbele ya mgeni
  • 12. Ndoa za Mitala  Utamaduni huu umebainishwa kupitia familia nyingi ndani ya tamthiliya hii.  Mwandishi anaonesha kuwa wanaume wengi katika kijiji kile wameoa mke zaidi ya mmoja.  Hajaonesha wazi kuwa utamaduni huu ni mbaya ingawa haushauriwi sana katika jamii.  Hii ni kwa sababu za kiuchumi na kiafya (kuenea kwa magonjwa ya zinaa)
  • 13. Kukosekana kwa Huduma za Kijamii  Huduma muhimu za kijamii ni kama shule na hospitali.  Katika mazungumzo ya wahusika inabainishwa kwamba huduma za kijamii kama shule, hospitali na huduma nyingine za kijamii zipo mbali na makazi ya watu.  Hii inadhihirisha ukosefu wa huduma za kijamii jambo linaloashirikia umasikini miongoni mwa wananchi katika kijiji kile.
  • 15. Ujumbe  Mapenzi ni chanzo cha uzembe katika jamii yetu  Kukosekana kwa elimu kunarudisha nyuma maendeleo  Imani za kishirikina ni adui wa maendeleo  Ni vizuri kufikiri kabla ya kutenda  Pombe ni adui mkubwa wa ustawi wa maendeleo ya binadamu  Mshika mawili moja humponyoka  Njia ya muongo ni fupi. Mazoea kumdanganya mama yake.  Kuwa na msimamo husaidia kuepuka vishawishi.
  • 16. Migogoro  Mgogoro kati ya Jimbi na Mitomingi baada ya jimbi kusahau siku ya kuhesabiwa akatuma watoto shambani.  Mgogoro kati ya Ngoswe na Mzee Jimbi wakigombania idadi ya miaka ya mzee Jimbi  Mgogoro kati ya mazoea na Mama Mazoea baada ya mazoea kuchelewa kurudi mtoni  Mgogoro kati ya Mitomingi na wakinamama wajane baada ya kuficha watoto wasihesabiwe  Mgogoro nafsia aliokuwa nao ngoswe baada ya kumkaribisha mama Mazoea ndani akidhani ni Mazoea.  Mgogoro nafsia aliokuwa nao Ngoswe baada ya kuchoma karatasi kwa ulevi
  • 17. Muendelezo…  Mgogoro kati ya Mzee Mitomingi na Mama Mazoea baada ya Mazoea kuitwa na baba yake kisha akadanganya kuwa alikuwa anamsuka mama yake.  Mgogoro kati ya Mitomingi na wake zake baada ya Mazoea kutoroshwa.  Mgogoro kati ya Ngoswe na Mitomingi  Mgogoro wa nafsi aliokuwa nao Ngoswe baada ya karatasi zake kuchomwa moto.  Mgogoro kati ya Ngoswe, Mitomingi na Serikali.  Mgogoro wa kitabaka kati ya mijini na vijijini
  • 18. Falsafa  Mwandishi anaamini kuwa ni vigumu kwa mwandamu kuchanganya mapenzi na kazi.  Anafafanua kwamba katika hali kama hiyo kimoja kitafanywa vizuri zaidi ya kingine.  Anamtumia mhusika Ngoswe aliyepoteza hesabu ya watu kwa sababu za uzembe wa kimapenzi.  Pia anaamini kuwa elimu inanafasi ya kutatua matatizo ya kijamii. Jamii ikielimika basi maendeleo yatatokea kwa urahisi.
  • 19. Mtazamo na Msimamo  Mwandishi anaiangalia jamii katika mtazamo yakinifu.  Anabainisha masuala yanayoigusa jamii waziwazi.  Mwisho anapendekeza masuluhisho ya masuala hayo.  Huu ni msimamo wa kimapinduzi kwa kuwa unalengo la kujenga jamii mpya.