SlideShare a Scribd company logo
1 of 15
KISWAHILI
NI
PIJINI
AU
KRIOLI?
M.Shekinyashi
+255 743 98 98 29
zingatia mchoro ufuatao:
Lugha AB
Lugha
B
Lugha
A
1. pijini
 Pijini ni zao la lugha mbili zilizokutana.
 Pijini huweza kuzuka mahala ambapo kuna makundi
mawili au zaidi na kila kundi likiwa na lugha yake.
 Ili kurahisisha mawasilano lugha hizi huchanganyika na
kuingiliana.
 Jambo hili huweza kusababisha kuzuka kwa lugha ya
mchanganyiko ambayo inaeleweka na makundi yote
mawili.
 Hivyo pijini huwapa watu uwezo wa kuwasiliana.
Sifa za Pijini
 Huundwa baada ya muingiliano wa lugha mbili tofauti.
 Haina mzungumzaji mzawa, kila mtu huwa na lugha
mama (lugha ya kwanza)
 Huibuka kukidhi mahitaji maalum, kama biashara
 Muundo wa maneno na tungo vimerahisishwa ili
kuwezesha mawasiliano.
 Haina misamiati ya kutosha
 Pijini ikikomaa na ikapata wazungumzaji wazawa huitwa
Krioli.
Aina za pijini
 Loreto Todd anapambanua aina mbili za Pijini;
i.Pijini pana
ii.Pijini finyu
Pijinifinyu
 Hii ni aina ya pijini ambayo huibuka katika muktadha wa
dharura sana baina ya jamii za watu wanaoongea lugha
mbili tofauti.
 Huwa na miundo sahili, hasa ya kisintaksia. Aghalabu
huambatisha ishara za kimwili kama macho, mikono na
viungo vingine vya mwili.
 Idadi kubwa ya misamiati hutoka kwenye lugha tawala.
 Huhusisha lugha mbili tu, na uhusiano baina ya jamii
zenye lugha hizo unapokwisha, basi pijini hufa
pijinipana
 Aina hii ya pijini huibuka kutokana na kudumishwa kwa
pijini.
 Matumizi ya pijini finyu yanapoimarika na kupanuka
hujenga lugha ambayo si thabiti lakini ni bora zaidi ya
pijinifinyu.
 Pijinipana ikipata wazungumzaji wazawa,basi huwa
krioli.
 Wataalamu kama; Bishop Steere, Bwana Taylor na Dkt.R. Reusch
wanadai kuwa lugha ya kiswahili ilitokana na mchanganyiko wa
lugha za Kiarabu na lugha za pwani ya Afrika Mashariki.
 Madai yanayotolewa na wataalamu hao ni kwamba kwa kipindi cha
karne nyingi wafanyabiashara wa kiarabu walikuwa wanakuja
Afrika Mashariki kufanya biashara.
 Katika kuendesha biashara zao ilibidi wenyeji wa pwani na hao
waarabu waunde namna fulani ya lugha ili waweze kuwasiliana.
 Lugha ambayo inajumuisha lugha zao zote; kiarabu na Lugha ya
kibantu.
 Lugha hiyo ndio kiswahili.
Krioli
 Ni Pijini iliyokomaa.
 Watu wanaozungumza pijini wanaweza kuishi pamoja
wakazoeana na kuoana, kisha wakazaa watoto.
 Watoto wakakuta pijini ikizungumzwa kama lugha ya
wazazi wao.
 Kwao hao watoto hii itakuwa lugha ya kwanza.
 Ikifika hatua hii, lugha hii huitwa krioli.
Sifa za krioli
 Huwa na msamiati mipana.
 Huwa na miundo mipana ya kisintaksia na kimofolojia.
 Wakati mwingine fonolojia yake inaanza kuwa thabiti
kutokana na upanuzi wa matumizi yake na dhima yake
katika jamii.
 Huwa na wasemaji wengi zaidi ya Pijini. Hii ni kwa
sababu krioli ina wasemaji wazawa.
 Inakuwa imewekwa kwenye maandishi mbalimbali kama
vile vitabu na majarida.
 Hufanyiwa uchambuzi katika luwaza zote; mofolojia,
fonolojia, sintaksia na semantiki.
 Baadhi ya wataalamu hudai kuwa kiswahili ni lugha ya jamii ya
vizalia waliotokana na mwingiliano kati ya waarabu na wabantu.
 Kutokana na mwingiliano huu kulizaliwa watoto ambao ni
mchanganyiko wa damu.
 Watoto hao ndio waswahili,hawa hawakuwa waarabu wala
wabantu.
 Wataalamu wanaounga mkono nadharia hii ni F. Johnson,
Freeman Genville,Hamo Sassoon na B. Krumm.
 Wao wanadai kuwa kiswahili ni Pijini iliyopata kukomaa, ikapata
vizalia na kupindukia kuwa krioli.
Udhaifu/dosari ya mtazamo huu
 Mtazamo huu umeshindwa kuitaja kinaganaga hiyo lugha ya
kibantu iliyochangamana na Kiarabu kuunda Kiswahili. Na kama ipo
ndio Kiswahili chenyewe.
 Mtazamo huu umesisitiza zaidi juu ya msamiati wa kiswahili wenye
asili ya kiarabu kama kigezo chake na kutupilia mbali vipengele
kama vile matamshi,maumbo na miundo ya sentensi.
 Kiswahili kingekuwa pijini au krioli inayotokana na lugha ya kibantu
na kiarabu, basi sintaksia yake ingefanana na ile ya kiarabu
 Pia, kama Kiswahili kingekuwa ni zao la uchangamano wa Kiarabu
na lugha ya Kibantu basi asilimia hamsini ya misamiati ya kiswahili
ingekuwa na asili ya kiarabu.
 Tofauti na ilivyo ambapo:
Msamiati wa kibantu- 60%
Msamiati wa Kiarabu-30%
Lugha nyingine -10%
 Tukizingatia yote haya, tunaona kwamba hatuna sababu ya
kutushawishi kukubaliana na nadhariatete hii.
 Kiswahili kinabaki kuwa ni lugha yenye asili ya Kibantu
Marejeleo
 Massamba.D.P,Kihore et al (2012)Sarufi Miundo ya
Kiswahili Sanifu: Sekondari na Vyuo. TUKI. DUP. Dar es
Salaam
 Masuko. C.S (2010)Kiswahili 1;Nadharia ya lugha kidato
cha tano na sita. STC publishers. Dar es Salaam.
 Nyambari.N & Masebo .J.A (2012) Nadharia ya Lugha:
Kiswahili 1. Nyambari Nyangwine Publishers. Dar es
Salaam.
 James.J &Mdunda F (2012)Kiswahili Kidatocha Tano na
Sita. Oxford University Press. Dar es salaam.
Kiswahili ni Pijini au Krioli

More Related Content

What's hot (20)

FASIHI KWA UJUMLA
FASIHI KWA UJUMLAFASIHI KWA UJUMLA
FASIHI KWA UJUMLA
 
Rejesta
RejestaRejesta
Rejesta
 
Tafsiri na ukalimani
Tafsiri na ukalimaniTafsiri na ukalimani
Tafsiri na ukalimani
 
TAFSIRI NA UKALIMANI
TAFSIRI NA UKALIMANITAFSIRI NA UKALIMANI
TAFSIRI NA UKALIMANI
 
CHIMBUKO LA FASIHI
CHIMBUKO LA FASIHICHIMBUKO LA FASIHI
CHIMBUKO LA FASIHI
 
Umuhimu wa kujifunza nadharia za fonolojia
Umuhimu wa kujifunza nadharia za fonolojiaUmuhimu wa kujifunza nadharia za fonolojia
Umuhimu wa kujifunza nadharia za fonolojia
 
Mofolojia ya kiswahili
Mofolojia ya kiswahiliMofolojia ya kiswahili
Mofolojia ya kiswahili
 
UTUMIZI WA LUGHA
UTUMIZI WA LUGHAUTUMIZI WA LUGHA
UTUMIZI WA LUGHA
 
Uhusiano fonolojia vs mofolojia
Uhusiano fonolojia vs mofolojiaUhusiano fonolojia vs mofolojia
Uhusiano fonolojia vs mofolojia
 
Uhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penzi
Uhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penziUhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penzi
Uhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penzi
 
Mofolojia
MofolojiaMofolojia
Mofolojia
 
Mjengo wa tungo 3
Mjengo wa tungo 3Mjengo wa tungo 3
Mjengo wa tungo 3
 
USHAIRI WA KISWAHILI
USHAIRI WA KISWAHILIUSHAIRI WA KISWAHILI
USHAIRI WA KISWAHILI
 
Uandishi wa matangazo
Uandishi wa matangazoUandishi wa matangazo
Uandishi wa matangazo
 
Mjengo wa tungo
Mjengo wa tungoMjengo wa tungo
Mjengo wa tungo
 
Uhakiki wa kazi za fasihi andishi
Uhakiki wa kazi za fasihi andishiUhakiki wa kazi za fasihi andishi
Uhakiki wa kazi za fasihi andishi
 
Kuongeza msamiati wa kiswahili
Kuongeza msamiati wa kiswahiliKuongeza msamiati wa kiswahili
Kuongeza msamiati wa kiswahili
 
UTUNGAJI
UTUNGAJIUTUNGAJI
UTUNGAJI
 
Ngeli za nomino
Ngeli za nominoNgeli za nomino
Ngeli za nomino
 
Ufahamu na ufupisho
Ufahamu na ufupishoUfahamu na ufupisho
Ufahamu na ufupisho
 

More from mussa Shekinyashi

More from mussa Shekinyashi (9)

Matumizi ya Lugha Kimuktadha
Matumizi ya Lugha KimuktadhaMatumizi ya Lugha Kimuktadha
Matumizi ya Lugha Kimuktadha
 
Uhifadhi wa fasihi simulizi
Uhifadhi wa fasihi simuliziUhifadhi wa fasihi simulizi
Uhifadhi wa fasihi simulizi
 
Evolution of Man (form one)
Evolution of Man (form one)Evolution of Man (form one)
Evolution of Man (form one)
 
Public Speaking Tips
Public Speaking TipsPublic Speaking Tips
Public Speaking Tips
 
UHAKIKI WA TAMTHILIYA - ORODHA
UHAKIKI WA TAMTHILIYA - ORODHAUHAKIKI WA TAMTHILIYA - ORODHA
UHAKIKI WA TAMTHILIYA - ORODHA
 
Uhuru wa Mtunzi wa Kazi za Fasihi
Uhuru wa Mtunzi wa Kazi za FasihiUhuru wa Mtunzi wa Kazi za Fasihi
Uhuru wa Mtunzi wa Kazi za Fasihi
 
GENDER CONCEPTS - FORM TWO
GENDER CONCEPTS - FORM TWO GENDER CONCEPTS - FORM TWO
GENDER CONCEPTS - FORM TWO
 
UHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHA
UHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHAUHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHA
UHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHA
 
Semantiki
SemantikiSemantiki
Semantiki
 

Kiswahili ni Pijini au Krioli

  • 2. zingatia mchoro ufuatao: Lugha AB Lugha B Lugha A
  • 3. 1. pijini  Pijini ni zao la lugha mbili zilizokutana.  Pijini huweza kuzuka mahala ambapo kuna makundi mawili au zaidi na kila kundi likiwa na lugha yake.  Ili kurahisisha mawasilano lugha hizi huchanganyika na kuingiliana.  Jambo hili huweza kusababisha kuzuka kwa lugha ya mchanganyiko ambayo inaeleweka na makundi yote mawili.  Hivyo pijini huwapa watu uwezo wa kuwasiliana.
  • 4. Sifa za Pijini  Huundwa baada ya muingiliano wa lugha mbili tofauti.  Haina mzungumzaji mzawa, kila mtu huwa na lugha mama (lugha ya kwanza)  Huibuka kukidhi mahitaji maalum, kama biashara  Muundo wa maneno na tungo vimerahisishwa ili kuwezesha mawasiliano.  Haina misamiati ya kutosha  Pijini ikikomaa na ikapata wazungumzaji wazawa huitwa Krioli.
  • 5. Aina za pijini  Loreto Todd anapambanua aina mbili za Pijini; i.Pijini pana ii.Pijini finyu
  • 6. Pijinifinyu  Hii ni aina ya pijini ambayo huibuka katika muktadha wa dharura sana baina ya jamii za watu wanaoongea lugha mbili tofauti.  Huwa na miundo sahili, hasa ya kisintaksia. Aghalabu huambatisha ishara za kimwili kama macho, mikono na viungo vingine vya mwili.  Idadi kubwa ya misamiati hutoka kwenye lugha tawala.  Huhusisha lugha mbili tu, na uhusiano baina ya jamii zenye lugha hizo unapokwisha, basi pijini hufa
  • 7. pijinipana  Aina hii ya pijini huibuka kutokana na kudumishwa kwa pijini.  Matumizi ya pijini finyu yanapoimarika na kupanuka hujenga lugha ambayo si thabiti lakini ni bora zaidi ya pijinifinyu.  Pijinipana ikipata wazungumzaji wazawa,basi huwa krioli.
  • 8.  Wataalamu kama; Bishop Steere, Bwana Taylor na Dkt.R. Reusch wanadai kuwa lugha ya kiswahili ilitokana na mchanganyiko wa lugha za Kiarabu na lugha za pwani ya Afrika Mashariki.  Madai yanayotolewa na wataalamu hao ni kwamba kwa kipindi cha karne nyingi wafanyabiashara wa kiarabu walikuwa wanakuja Afrika Mashariki kufanya biashara.  Katika kuendesha biashara zao ilibidi wenyeji wa pwani na hao waarabu waunde namna fulani ya lugha ili waweze kuwasiliana.  Lugha ambayo inajumuisha lugha zao zote; kiarabu na Lugha ya kibantu.  Lugha hiyo ndio kiswahili.
  • 9. Krioli  Ni Pijini iliyokomaa.  Watu wanaozungumza pijini wanaweza kuishi pamoja wakazoeana na kuoana, kisha wakazaa watoto.  Watoto wakakuta pijini ikizungumzwa kama lugha ya wazazi wao.  Kwao hao watoto hii itakuwa lugha ya kwanza.  Ikifika hatua hii, lugha hii huitwa krioli.
  • 10. Sifa za krioli  Huwa na msamiati mipana.  Huwa na miundo mipana ya kisintaksia na kimofolojia.  Wakati mwingine fonolojia yake inaanza kuwa thabiti kutokana na upanuzi wa matumizi yake na dhima yake katika jamii.  Huwa na wasemaji wengi zaidi ya Pijini. Hii ni kwa sababu krioli ina wasemaji wazawa.  Inakuwa imewekwa kwenye maandishi mbalimbali kama vile vitabu na majarida.  Hufanyiwa uchambuzi katika luwaza zote; mofolojia, fonolojia, sintaksia na semantiki.
  • 11.  Baadhi ya wataalamu hudai kuwa kiswahili ni lugha ya jamii ya vizalia waliotokana na mwingiliano kati ya waarabu na wabantu.  Kutokana na mwingiliano huu kulizaliwa watoto ambao ni mchanganyiko wa damu.  Watoto hao ndio waswahili,hawa hawakuwa waarabu wala wabantu.  Wataalamu wanaounga mkono nadharia hii ni F. Johnson, Freeman Genville,Hamo Sassoon na B. Krumm.  Wao wanadai kuwa kiswahili ni Pijini iliyopata kukomaa, ikapata vizalia na kupindukia kuwa krioli.
  • 12. Udhaifu/dosari ya mtazamo huu  Mtazamo huu umeshindwa kuitaja kinaganaga hiyo lugha ya kibantu iliyochangamana na Kiarabu kuunda Kiswahili. Na kama ipo ndio Kiswahili chenyewe.  Mtazamo huu umesisitiza zaidi juu ya msamiati wa kiswahili wenye asili ya kiarabu kama kigezo chake na kutupilia mbali vipengele kama vile matamshi,maumbo na miundo ya sentensi.  Kiswahili kingekuwa pijini au krioli inayotokana na lugha ya kibantu na kiarabu, basi sintaksia yake ingefanana na ile ya kiarabu
  • 13.  Pia, kama Kiswahili kingekuwa ni zao la uchangamano wa Kiarabu na lugha ya Kibantu basi asilimia hamsini ya misamiati ya kiswahili ingekuwa na asili ya kiarabu.  Tofauti na ilivyo ambapo: Msamiati wa kibantu- 60% Msamiati wa Kiarabu-30% Lugha nyingine -10%  Tukizingatia yote haya, tunaona kwamba hatuna sababu ya kutushawishi kukubaliana na nadhariatete hii.  Kiswahili kinabaki kuwa ni lugha yenye asili ya Kibantu
  • 14. Marejeleo  Massamba.D.P,Kihore et al (2012)Sarufi Miundo ya Kiswahili Sanifu: Sekondari na Vyuo. TUKI. DUP. Dar es Salaam  Masuko. C.S (2010)Kiswahili 1;Nadharia ya lugha kidato cha tano na sita. STC publishers. Dar es Salaam.  Nyambari.N & Masebo .J.A (2012) Nadharia ya Lugha: Kiswahili 1. Nyambari Nyangwine Publishers. Dar es Salaam.  James.J &Mdunda F (2012)Kiswahili Kidatocha Tano na Sita. Oxford University Press. Dar es salaam.