Uwasilishaji huu ni juu ya uhuru wa mtunzi wa kazi za fasihi. Ni nukuu muhimu kwa ajili ya walimu na wanafunzi wa kidato cha tano na sita nchini Tanzania
1. UHURU WA MTUNZI
WA KAZI ZA FASIHI
MUSSA SHEKINYASHI
0714 807565
0743989829
2. Uhuru ni nini?
Uhuru ni hali ya kutotawaliwa na mtu au nchi nyingine;
hali ya kufanya mambo bila kuingiliwa.
3. Uhuru wa mtunzi
Ni hali ya mtunzi wa kazi ya fasihi kutunga au kuandika
kazi zake bila kushinikizwa na mtu, watu,au taasisi fulani
yenye nguvu kiuchumi, kisiasa au kiutawala.
Profesa E.Kezilahabi(1993) anasema dhana ya uhuru wa
mwandishi wa kazi ya fasihi kifalsafa ni uwezo wa mtu
binafsi kufanya uamuzi,kujijua,kujiendesha na
kujirekebisha.
Anaifafanua dhana ya uhuru kama ifuatavyo:
4. 1.Uhuru wa mwandishi umo katika
utashi
Mwandishi anayekosa utashi anakuwa mwoga na hukata
tamaa mapema au huyumbishwa kutokana na
makombora ya wahakiki na wanasiasa.
Lakini mwandishi mwenye utashi, makombora ya
wahakiki watawala na wanasiasa humkomaza.
Waandishi wa kiafrika wenye utashi ni Wole Soyinka wa
Nigeria na Ngugi wa Thiong’o wa Kenya.
5. 2. Uhuru wa mwandishi upo katika
falsafa moja inayoeleweka
Falsafa moja inayoeleweka huyafanya maandishi
yaonekane kama kazi moja yenye mwelekeo maalumu.
Falsafa ndio kamba inayoyafanya maandishi yote ya
mwandishi yawe kazi moja na sio jina lake.
Waandishi wa fasihi ya kiswahili waliosimama katika
falsafa moja ni Shabani Robert na E. Kezirahabi
6. 3. Uhuru wa Mwandishi umo katika
Kuitawala Vema Sanaa Yake
Mwandishi anayeandika aina fulani ya fasihi,kama vile
riwaya,tamthiliya au ushairi; ambayo hana ujuzi nayo hakika
kazi yake itatoka ikiwa hafifu.
Kadhalika,mwandishi anayeshindwa kuunganisha vema
ubunifu na uhalisia kazi yake hupoteza ladha.
Hivyo, uhuru wa mwandishi unategemea na uwezo wake wa
kushughulikia nyanja ya fasihi anayoimudu pia kuweza
kusimamia kipengele cha uhalisia na ubunifu katika viwango
sawa bila kuzidisha kimojawapo.
Mfano wa waandishi wa kiswahili wanaozingatia haya ni
Ebrahim Husseni na Penina Muhando
7. 4. Uhuru wa Mwandishi Umo katika
Kuitawala Lugha Anayoitumia
Mwandishi au mtunzi wa kazi ya fasihi hawezi kuitawala
vema sanaa anayoitumia kama msingi wa lugha
anyoitumia ni mbovu.
Lugha ndio kiungo maalum kati ya mtunzi na hadhira
anayoitungia au kuiandikia.
Kukosekana kwa weledi katika lugha humkosesha uhuru
mwandishi au mtunzi wa kazi za kifasihi.
8. Historia Fupi ya Udhibiti wa Uhuru wa
Mwandishi
Suala la udhibiti wa uhuru wa mwandishi ni la kitabaka
kwani lilianza pale tu jamii ilipogawanyika katika
matabaka mbalimbali ya watu.
Hapa tunazungumzia jamii zilizofuata baada ya mfumo
wa kiujima; yaani utumwa,ukabaila na ubepari.
Mara tu maandishi yalipogundulika,fasihi andishi ya
mwanzo ilikuwa ni teule kwa wachache wenye vyeo na
vyao.
9. Walihakikisha kwamba kuna mbinu inatumika ikiwemo ya udhibiti wa
maandishi ili kulinda utawala wao.
Ingawa tabaka la chini nalo lilikuwa na fasihi yao ambayo kimsingi ilikuwa
simulizi,iliyoelezea hisia zao,majonzi yao,hasira zao na matumaini yao.
Fasihi hii pia ilishambuliwa na rungu la udhibiti hata ikakosa uhuru.
Kutokana na maelezo hayo basi, kazi ya fasihi ni kulinda tabaka tawala.
Tabaka tawala huhakikisha kwamba fasihi inatumiwa kueneza itikadi zake.
10. Mifano ya Kazi za Fasihi zilizokutana
na Udhibiti
Mfano mzuri ni kazi za muamerika kusini Pablo Neruda
ambaye mwanzoni aliandika mashairi yake kusifia viumbe
na mazingira kwa ujumla.
Baadae alibadilisha muelekeo akawa anaelezea dhiki za
watu wa tabaka la chini. Hapo alikutana na upinzani
mkubwa kutoka kwa wahakiki na tabaka tawala.
Pia Ngugi wa Thion’go tamthiliya yake “I will Mary when I
want” “Nitaolewa Nitakapotaka”ilifungiwa kwa kuwa
ilikuwa inalikosoa tabaka tawala.
11. Uhuru wa Mwandishi wa Kazi za
Fasihi Nchini Tanzania
Kabla ya Uhuru
Kwa mujibu wa Senkoro (1993),hapa Tanzania udhibiti wa
uhuru wa mwandishi ulianza tangu enzi ya mkoloni.
Udhibiti huu ulidhihirika kupitia vitabu walivyovitumia
kufundishia mashuleni ambavyo vyote vilitafsiriwa na vina
tukuza na kueneza utamaduni wao.
Mfano wa vitabu hivyo ni kama: Mashimo ya Mfalme
Suleiman, Hadithi za Allan Quarterman ,Safari za Gulliver
na Robinson Kruso.
12. Mbali ya kuwa fasihi hizo zilikuwa na lengo la kupumbaza
uwezo wa mwafrika kujitambua pia zilidhamiria
kupenyeza imani za kidini na kuua imani za dini za jadi za
watanganyika.
Vitabu vya kihistoria vilivyotumika kufundishia mashuleni
vilikuwa vinapotosha uhalisia wa historia ya mtu mweusi
na kudai kuwa mwafrika hana historia kabisa
13. Baada ya Uhuru
Mapinduzi ya Zanzibar na Azimio la Arusha ni moja ya matukio
yaliyoshangiliwa sana nchini Tanzania baada ya uhuru.
Fasihi andishi iliyojitokeza mara tu baada ya matukio haya ilijaa chereko
hoihoi na vifijo vya kuyashangilia.
Kwa upande mwingine matukio hayo yalisaidia kuzichonga kalamu za
baadhi ya waandishi waliokuwa wakifuatilia utekelezaji au ukiukwaji wa
maadili ya matukio hayo kama ilivyotangazwa na wanasiasa.
14. Zao la ufuatiliaji huo ni riwaya ya Rosa Mistika (1971) iliyoandikwa na
Profesa E. Kezilahabi.
Riwaya hiyo ilipigwa marufuku isitumiwe mashuleni na isiuzwe madukani.
Sababu,imekiuka miiko ya kijamii
Pia, imedhalilisha kanisa katoliki kwa kutumia jina mistika
Imewadhalilisha wanawake
15. Mwaka 1974 na 1975 kamati kuu ya TANU ilifungia vitabu
vyote vya David G.Mailu wa Kenya.
Vitabu hivyo ni;
My Dear Bottle (1973)
After4.30 (1973)
Trouble (1974)
Pia walifungia kitabu cha Mamuya “Jando na Unyago”
Hivi vilielezwa kuwa ni vitabu vichafu havikuzingatia
maadili ya jamii.
16. Dhima ya uhuru wa Mwandishi
Nia ya uhuru wa mwandishi ni kumfanya mwandishi
kuikosoa jamii au kulikosoa tabaka lolote lile
linalokwenda kinyume na utaratibu wa jamii bila matatizo.
Mwandishi awe na falsafa inayoeleweka pamoja na utashi.
Mwandishi awe huru kutoa mwongozo kwa jamii, kwa
kuikomboa jamii kutoka katika fikra gandamizi na za
unyonyaji.