SlideShare a Scribd company logo
1 of 18
UHURU WA MTUNZI
WA KAZI ZA FASIHI
MUSSA SHEKINYASHI
0714 807565
0743989829
Uhuru ni nini?
 Uhuru ni hali ya kutotawaliwa na mtu au nchi nyingine;
hali ya kufanya mambo bila kuingiliwa.
Uhuru wa mtunzi
 Ni hali ya mtunzi wa kazi ya fasihi kutunga au kuandika
kazi zake bila kushinikizwa na mtu, watu,au taasisi fulani
yenye nguvu kiuchumi, kisiasa au kiutawala.
 Profesa E.Kezilahabi(1993) anasema dhana ya uhuru wa
mwandishi wa kazi ya fasihi kifalsafa ni uwezo wa mtu
binafsi kufanya uamuzi,kujijua,kujiendesha na
kujirekebisha.
 Anaifafanua dhana ya uhuru kama ifuatavyo:
1.Uhuru wa mwandishi umo katika
utashi
 Mwandishi anayekosa utashi anakuwa mwoga na hukata
tamaa mapema au huyumbishwa kutokana na
makombora ya wahakiki na wanasiasa.
 Lakini mwandishi mwenye utashi, makombora ya
wahakiki watawala na wanasiasa humkomaza.
 Waandishi wa kiafrika wenye utashi ni Wole Soyinka wa
Nigeria na Ngugi wa Thiong’o wa Kenya.
2. Uhuru wa mwandishi upo katika
falsafa moja inayoeleweka
 Falsafa moja inayoeleweka huyafanya maandishi
yaonekane kama kazi moja yenye mwelekeo maalumu.
 Falsafa ndio kamba inayoyafanya maandishi yote ya
mwandishi yawe kazi moja na sio jina lake.
 Waandishi wa fasihi ya kiswahili waliosimama katika
falsafa moja ni Shabani Robert na E. Kezirahabi
3. Uhuru wa Mwandishi umo katika
Kuitawala Vema Sanaa Yake
 Mwandishi anayeandika aina fulani ya fasihi,kama vile
riwaya,tamthiliya au ushairi; ambayo hana ujuzi nayo hakika
kazi yake itatoka ikiwa hafifu.
 Kadhalika,mwandishi anayeshindwa kuunganisha vema
ubunifu na uhalisia kazi yake hupoteza ladha.
 Hivyo, uhuru wa mwandishi unategemea na uwezo wake wa
kushughulikia nyanja ya fasihi anayoimudu pia kuweza
kusimamia kipengele cha uhalisia na ubunifu katika viwango
sawa bila kuzidisha kimojawapo.
 Mfano wa waandishi wa kiswahili wanaozingatia haya ni
Ebrahim Husseni na Penina Muhando
4. Uhuru wa Mwandishi Umo katika
Kuitawala Lugha Anayoitumia
 Mwandishi au mtunzi wa kazi ya fasihi hawezi kuitawala
vema sanaa anayoitumia kama msingi wa lugha
anyoitumia ni mbovu.
 Lugha ndio kiungo maalum kati ya mtunzi na hadhira
anayoitungia au kuiandikia.
 Kukosekana kwa weledi katika lugha humkosesha uhuru
mwandishi au mtunzi wa kazi za kifasihi.
Historia Fupi ya Udhibiti wa Uhuru wa
Mwandishi
 Suala la udhibiti wa uhuru wa mwandishi ni la kitabaka
kwani lilianza pale tu jamii ilipogawanyika katika
matabaka mbalimbali ya watu.
 Hapa tunazungumzia jamii zilizofuata baada ya mfumo
wa kiujima; yaani utumwa,ukabaila na ubepari.
 Mara tu maandishi yalipogundulika,fasihi andishi ya
mwanzo ilikuwa ni teule kwa wachache wenye vyeo na
vyao.
 Walihakikisha kwamba kuna mbinu inatumika ikiwemo ya udhibiti wa
maandishi ili kulinda utawala wao.
 Ingawa tabaka la chini nalo lilikuwa na fasihi yao ambayo kimsingi ilikuwa
simulizi,iliyoelezea hisia zao,majonzi yao,hasira zao na matumaini yao.
 Fasihi hii pia ilishambuliwa na rungu la udhibiti hata ikakosa uhuru.
 Kutokana na maelezo hayo basi, kazi ya fasihi ni kulinda tabaka tawala.
 Tabaka tawala huhakikisha kwamba fasihi inatumiwa kueneza itikadi zake.
Mifano ya Kazi za Fasihi zilizokutana
na Udhibiti
 Mfano mzuri ni kazi za muamerika kusini Pablo Neruda
ambaye mwanzoni aliandika mashairi yake kusifia viumbe
na mazingira kwa ujumla.
 Baadae alibadilisha muelekeo akawa anaelezea dhiki za
watu wa tabaka la chini. Hapo alikutana na upinzani
mkubwa kutoka kwa wahakiki na tabaka tawala.
 Pia Ngugi wa Thion’go tamthiliya yake “I will Mary when I
want” “Nitaolewa Nitakapotaka”ilifungiwa kwa kuwa
ilikuwa inalikosoa tabaka tawala.
Uhuru wa Mwandishi wa Kazi za
Fasihi Nchini Tanzania
 Kabla ya Uhuru
 Kwa mujibu wa Senkoro (1993),hapa Tanzania udhibiti wa
uhuru wa mwandishi ulianza tangu enzi ya mkoloni.
 Udhibiti huu ulidhihirika kupitia vitabu walivyovitumia
kufundishia mashuleni ambavyo vyote vilitafsiriwa na vina
tukuza na kueneza utamaduni wao.
 Mfano wa vitabu hivyo ni kama: Mashimo ya Mfalme
Suleiman, Hadithi za Allan Quarterman ,Safari za Gulliver
na Robinson Kruso.
 Mbali ya kuwa fasihi hizo zilikuwa na lengo la kupumbaza
uwezo wa mwafrika kujitambua pia zilidhamiria
kupenyeza imani za kidini na kuua imani za dini za jadi za
watanganyika.
 Vitabu vya kihistoria vilivyotumika kufundishia mashuleni
vilikuwa vinapotosha uhalisia wa historia ya mtu mweusi
na kudai kuwa mwafrika hana historia kabisa
 Baada ya Uhuru
 Mapinduzi ya Zanzibar na Azimio la Arusha ni moja ya matukio
yaliyoshangiliwa sana nchini Tanzania baada ya uhuru.
 Fasihi andishi iliyojitokeza mara tu baada ya matukio haya ilijaa chereko
hoihoi na vifijo vya kuyashangilia.
 Kwa upande mwingine matukio hayo yalisaidia kuzichonga kalamu za
baadhi ya waandishi waliokuwa wakifuatilia utekelezaji au ukiukwaji wa
maadili ya matukio hayo kama ilivyotangazwa na wanasiasa.
 Zao la ufuatiliaji huo ni riwaya ya Rosa Mistika (1971) iliyoandikwa na
Profesa E. Kezilahabi.
 Riwaya hiyo ilipigwa marufuku isitumiwe mashuleni na isiuzwe madukani.
 Sababu,imekiuka miiko ya kijamii
 Pia, imedhalilisha kanisa katoliki kwa kutumia jina mistika
 Imewadhalilisha wanawake
 Mwaka 1974 na 1975 kamati kuu ya TANU ilifungia vitabu
vyote vya David G.Mailu wa Kenya.
 Vitabu hivyo ni;
 My Dear Bottle (1973)
 After4.30 (1973)
 Trouble (1974)
 Pia walifungia kitabu cha Mamuya “Jando na Unyago”
 Hivi vilielezwa kuwa ni vitabu vichafu havikuzingatia
maadili ya jamii.
Dhima ya uhuru wa Mwandishi
 Nia ya uhuru wa mwandishi ni kumfanya mwandishi
kuikosoa jamii au kulikosoa tabaka lolote lile
linalokwenda kinyume na utaratibu wa jamii bila matatizo.
 Mwandishi awe na falsafa inayoeleweka pamoja na utashi.
 Mwandishi awe huru kutoa mwongozo kwa jamii, kwa
kuikomboa jamii kutoka katika fikra gandamizi na za
unyonyaji.
 Kupunguza uandishi wa kikasuku
 Mwandishi awe huru kuielimisha jamii.
ASANTENI

More Related Content

What's hot

Chimbuko na Asili ya Kiswahili
Chimbuko na Asili ya KiswahiliChimbuko na Asili ya Kiswahili
Chimbuko na Asili ya Kiswahilimussa Shekinyashi
 
USHAIRI WA KISWAHILI
USHAIRI WA KISWAHILIUSHAIRI WA KISWAHILI
USHAIRI WA KISWAHILIPeter Deus
 
UHAKIKI WA FASIHI ANDISHI
UHAKIKI WA FASIHI ANDISHIUHAKIKI WA FASIHI ANDISHI
UHAKIKI WA FASIHI ANDISHIshahzadebaujiti
 
Uhakiki wa kazi za fasihi andishi
Uhakiki wa kazi za fasihi andishiUhakiki wa kazi za fasihi andishi
Uhakiki wa kazi za fasihi andishiMussaOmary3
 
Maendeleo ya kiswahili
Maendeleo ya kiswahiliMaendeleo ya kiswahili
Maendeleo ya kiswahiliMussaOmary3
 
Mofolojia ya kiswahili
Mofolojia ya kiswahiliMofolojia ya kiswahili
Mofolojia ya kiswahiliGeophery sanga
 
Uhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penzi
Uhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penziUhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penzi
Uhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penzimussa Shekinyashi
 
Umuhimu wa kujifunza nadharia za fonolojia
Umuhimu wa kujifunza nadharia za fonolojiaUmuhimu wa kujifunza nadharia za fonolojia
Umuhimu wa kujifunza nadharia za fonolojiaHamad Khamis Juma
 
Ushairi wa Kiswahili kuanzia karne ya 16 mpaka karne ya 20
Ushairi wa Kiswahili kuanzia karne ya 16 mpaka karne ya 20Ushairi wa Kiswahili kuanzia karne ya 16 mpaka karne ya 20
Ushairi wa Kiswahili kuanzia karne ya 16 mpaka karne ya 20Mathieu Roy
 
Kuongeza msamiati wa kiswahili
Kuongeza msamiati wa kiswahiliKuongeza msamiati wa kiswahili
Kuongeza msamiati wa kiswahiliKAZEMBETVOnline
 

What's hot (20)

MATUMIZI YA SARUFI
MATUMIZI YA SARUFIMATUMIZI YA SARUFI
MATUMIZI YA SARUFI
 
Chimbuko na Asili ya Kiswahili
Chimbuko na Asili ya KiswahiliChimbuko na Asili ya Kiswahili
Chimbuko na Asili ya Kiswahili
 
USHAIRI WA KISWAHILI
USHAIRI WA KISWAHILIUSHAIRI WA KISWAHILI
USHAIRI WA KISWAHILI
 
UTUMIZI WA LUGHA
UTUMIZI WA LUGHAUTUMIZI WA LUGHA
UTUMIZI WA LUGHA
 
UHAKIKI WA FASIHI ANDISHI
UHAKIKI WA FASIHI ANDISHIUHAKIKI WA FASIHI ANDISHI
UHAKIKI WA FASIHI ANDISHI
 
Uhakiki wa kazi za fasihi andishi
Uhakiki wa kazi za fasihi andishiUhakiki wa kazi za fasihi andishi
Uhakiki wa kazi za fasihi andishi
 
Sarufi Matamshi (Fonolojia)
Sarufi Matamshi (Fonolojia)Sarufi Matamshi (Fonolojia)
Sarufi Matamshi (Fonolojia)
 
UTUNGAJI
UTUNGAJIUTUNGAJI
UTUNGAJI
 
Maendeleo ya kiswahili
Maendeleo ya kiswahiliMaendeleo ya kiswahili
Maendeleo ya kiswahili
 
TAFSIRI NA UKALIMANI
TAFSIRI NA UKALIMANITAFSIRI NA UKALIMANI
TAFSIRI NA UKALIMANI
 
Mofolojia ya kiswahili
Mofolojia ya kiswahiliMofolojia ya kiswahili
Mofolojia ya kiswahili
 
Tafsiri na ukalimani
Tafsiri na ukalimaniTafsiri na ukalimani
Tafsiri na ukalimani
 
Tamthilia ni nini?
Tamthilia ni nini?Tamthilia ni nini?
Tamthilia ni nini?
 
Dhima za kamusi
Dhima za kamusiDhima za kamusi
Dhima za kamusi
 
Uhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penzi
Uhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penziUhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penzi
Uhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penzi
 
Mofolojia
MofolojiaMofolojia
Mofolojia
 
Mjengo wa tungo 3
Mjengo wa tungo 3Mjengo wa tungo 3
Mjengo wa tungo 3
 
Umuhimu wa kujifunza nadharia za fonolojia
Umuhimu wa kujifunza nadharia za fonolojiaUmuhimu wa kujifunza nadharia za fonolojia
Umuhimu wa kujifunza nadharia za fonolojia
 
Ushairi wa Kiswahili kuanzia karne ya 16 mpaka karne ya 20
Ushairi wa Kiswahili kuanzia karne ya 16 mpaka karne ya 20Ushairi wa Kiswahili kuanzia karne ya 16 mpaka karne ya 20
Ushairi wa Kiswahili kuanzia karne ya 16 mpaka karne ya 20
 
Kuongeza msamiati wa kiswahili
Kuongeza msamiati wa kiswahiliKuongeza msamiati wa kiswahili
Kuongeza msamiati wa kiswahili
 

More from mussa Shekinyashi

More from mussa Shekinyashi (9)

Rejesta
RejestaRejesta
Rejesta
 
Matumizi ya Lugha Kimuktadha
Matumizi ya Lugha KimuktadhaMatumizi ya Lugha Kimuktadha
Matumizi ya Lugha Kimuktadha
 
Uhifadhi wa fasihi simulizi
Uhifadhi wa fasihi simuliziUhifadhi wa fasihi simulizi
Uhifadhi wa fasihi simulizi
 
Evolution of Man (form one)
Evolution of Man (form one)Evolution of Man (form one)
Evolution of Man (form one)
 
Public Speaking Tips
Public Speaking TipsPublic Speaking Tips
Public Speaking Tips
 
UHAKIKI WA TAMTHILIYA - ORODHA
UHAKIKI WA TAMTHILIYA - ORODHAUHAKIKI WA TAMTHILIYA - ORODHA
UHAKIKI WA TAMTHILIYA - ORODHA
 
GENDER CONCEPTS - FORM TWO
GENDER CONCEPTS - FORM TWO GENDER CONCEPTS - FORM TWO
GENDER CONCEPTS - FORM TWO
 
UHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHA
UHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHAUHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHA
UHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHA
 
Semantiki
SemantikiSemantiki
Semantiki
 

Uhuru wa Mtunzi wa Kazi za Fasihi

  • 1. UHURU WA MTUNZI WA KAZI ZA FASIHI MUSSA SHEKINYASHI 0714 807565 0743989829
  • 2. Uhuru ni nini?  Uhuru ni hali ya kutotawaliwa na mtu au nchi nyingine; hali ya kufanya mambo bila kuingiliwa.
  • 3. Uhuru wa mtunzi  Ni hali ya mtunzi wa kazi ya fasihi kutunga au kuandika kazi zake bila kushinikizwa na mtu, watu,au taasisi fulani yenye nguvu kiuchumi, kisiasa au kiutawala.  Profesa E.Kezilahabi(1993) anasema dhana ya uhuru wa mwandishi wa kazi ya fasihi kifalsafa ni uwezo wa mtu binafsi kufanya uamuzi,kujijua,kujiendesha na kujirekebisha.  Anaifafanua dhana ya uhuru kama ifuatavyo:
  • 4. 1.Uhuru wa mwandishi umo katika utashi  Mwandishi anayekosa utashi anakuwa mwoga na hukata tamaa mapema au huyumbishwa kutokana na makombora ya wahakiki na wanasiasa.  Lakini mwandishi mwenye utashi, makombora ya wahakiki watawala na wanasiasa humkomaza.  Waandishi wa kiafrika wenye utashi ni Wole Soyinka wa Nigeria na Ngugi wa Thiong’o wa Kenya.
  • 5. 2. Uhuru wa mwandishi upo katika falsafa moja inayoeleweka  Falsafa moja inayoeleweka huyafanya maandishi yaonekane kama kazi moja yenye mwelekeo maalumu.  Falsafa ndio kamba inayoyafanya maandishi yote ya mwandishi yawe kazi moja na sio jina lake.  Waandishi wa fasihi ya kiswahili waliosimama katika falsafa moja ni Shabani Robert na E. Kezirahabi
  • 6. 3. Uhuru wa Mwandishi umo katika Kuitawala Vema Sanaa Yake  Mwandishi anayeandika aina fulani ya fasihi,kama vile riwaya,tamthiliya au ushairi; ambayo hana ujuzi nayo hakika kazi yake itatoka ikiwa hafifu.  Kadhalika,mwandishi anayeshindwa kuunganisha vema ubunifu na uhalisia kazi yake hupoteza ladha.  Hivyo, uhuru wa mwandishi unategemea na uwezo wake wa kushughulikia nyanja ya fasihi anayoimudu pia kuweza kusimamia kipengele cha uhalisia na ubunifu katika viwango sawa bila kuzidisha kimojawapo.  Mfano wa waandishi wa kiswahili wanaozingatia haya ni Ebrahim Husseni na Penina Muhando
  • 7. 4. Uhuru wa Mwandishi Umo katika Kuitawala Lugha Anayoitumia  Mwandishi au mtunzi wa kazi ya fasihi hawezi kuitawala vema sanaa anayoitumia kama msingi wa lugha anyoitumia ni mbovu.  Lugha ndio kiungo maalum kati ya mtunzi na hadhira anayoitungia au kuiandikia.  Kukosekana kwa weledi katika lugha humkosesha uhuru mwandishi au mtunzi wa kazi za kifasihi.
  • 8. Historia Fupi ya Udhibiti wa Uhuru wa Mwandishi  Suala la udhibiti wa uhuru wa mwandishi ni la kitabaka kwani lilianza pale tu jamii ilipogawanyika katika matabaka mbalimbali ya watu.  Hapa tunazungumzia jamii zilizofuata baada ya mfumo wa kiujima; yaani utumwa,ukabaila na ubepari.  Mara tu maandishi yalipogundulika,fasihi andishi ya mwanzo ilikuwa ni teule kwa wachache wenye vyeo na vyao.
  • 9.  Walihakikisha kwamba kuna mbinu inatumika ikiwemo ya udhibiti wa maandishi ili kulinda utawala wao.  Ingawa tabaka la chini nalo lilikuwa na fasihi yao ambayo kimsingi ilikuwa simulizi,iliyoelezea hisia zao,majonzi yao,hasira zao na matumaini yao.  Fasihi hii pia ilishambuliwa na rungu la udhibiti hata ikakosa uhuru.  Kutokana na maelezo hayo basi, kazi ya fasihi ni kulinda tabaka tawala.  Tabaka tawala huhakikisha kwamba fasihi inatumiwa kueneza itikadi zake.
  • 10. Mifano ya Kazi za Fasihi zilizokutana na Udhibiti  Mfano mzuri ni kazi za muamerika kusini Pablo Neruda ambaye mwanzoni aliandika mashairi yake kusifia viumbe na mazingira kwa ujumla.  Baadae alibadilisha muelekeo akawa anaelezea dhiki za watu wa tabaka la chini. Hapo alikutana na upinzani mkubwa kutoka kwa wahakiki na tabaka tawala.  Pia Ngugi wa Thion’go tamthiliya yake “I will Mary when I want” “Nitaolewa Nitakapotaka”ilifungiwa kwa kuwa ilikuwa inalikosoa tabaka tawala.
  • 11. Uhuru wa Mwandishi wa Kazi za Fasihi Nchini Tanzania  Kabla ya Uhuru  Kwa mujibu wa Senkoro (1993),hapa Tanzania udhibiti wa uhuru wa mwandishi ulianza tangu enzi ya mkoloni.  Udhibiti huu ulidhihirika kupitia vitabu walivyovitumia kufundishia mashuleni ambavyo vyote vilitafsiriwa na vina tukuza na kueneza utamaduni wao.  Mfano wa vitabu hivyo ni kama: Mashimo ya Mfalme Suleiman, Hadithi za Allan Quarterman ,Safari za Gulliver na Robinson Kruso.
  • 12.  Mbali ya kuwa fasihi hizo zilikuwa na lengo la kupumbaza uwezo wa mwafrika kujitambua pia zilidhamiria kupenyeza imani za kidini na kuua imani za dini za jadi za watanganyika.  Vitabu vya kihistoria vilivyotumika kufundishia mashuleni vilikuwa vinapotosha uhalisia wa historia ya mtu mweusi na kudai kuwa mwafrika hana historia kabisa
  • 13.  Baada ya Uhuru  Mapinduzi ya Zanzibar na Azimio la Arusha ni moja ya matukio yaliyoshangiliwa sana nchini Tanzania baada ya uhuru.  Fasihi andishi iliyojitokeza mara tu baada ya matukio haya ilijaa chereko hoihoi na vifijo vya kuyashangilia.  Kwa upande mwingine matukio hayo yalisaidia kuzichonga kalamu za baadhi ya waandishi waliokuwa wakifuatilia utekelezaji au ukiukwaji wa maadili ya matukio hayo kama ilivyotangazwa na wanasiasa.
  • 14.  Zao la ufuatiliaji huo ni riwaya ya Rosa Mistika (1971) iliyoandikwa na Profesa E. Kezilahabi.  Riwaya hiyo ilipigwa marufuku isitumiwe mashuleni na isiuzwe madukani.  Sababu,imekiuka miiko ya kijamii  Pia, imedhalilisha kanisa katoliki kwa kutumia jina mistika  Imewadhalilisha wanawake
  • 15.  Mwaka 1974 na 1975 kamati kuu ya TANU ilifungia vitabu vyote vya David G.Mailu wa Kenya.  Vitabu hivyo ni;  My Dear Bottle (1973)  After4.30 (1973)  Trouble (1974)  Pia walifungia kitabu cha Mamuya “Jando na Unyago”  Hivi vilielezwa kuwa ni vitabu vichafu havikuzingatia maadili ya jamii.
  • 16. Dhima ya uhuru wa Mwandishi  Nia ya uhuru wa mwandishi ni kumfanya mwandishi kuikosoa jamii au kulikosoa tabaka lolote lile linalokwenda kinyume na utaratibu wa jamii bila matatizo.  Mwandishi awe na falsafa inayoeleweka pamoja na utashi.  Mwandishi awe huru kutoa mwongozo kwa jamii, kwa kuikomboa jamii kutoka katika fikra gandamizi na za unyonyaji.
  • 17.  Kupunguza uandishi wa kikasuku  Mwandishi awe huru kuielimisha jamii.