SlideShare a Scribd company logo
1 of 31
KUKUA NA KUENEA
KWA
KISWAHILI
Mussa Shekinyashi
Kukua kwa Lugha.
 Kukua kwa lugha ni kuongezeka kwa msamiati na
kuimarika kwa sarufi ya lugha husika.
 Lugha ya Kiswahili imepitia katika vipindi mbalimbali vya
mabadiliko ya kimfumo wa kimaisha na kiutawala.
 Watawala mbalimbali, kama waarabu, wajerumani na
waingereza wamechangia kukua kwa lugha ya Kiswahili.
 Katika vipindi hivi vyote lugha ya Kiswahili imeongeza
msamiati, imeimarisha sarufi na kuimarisha matumizi yake
katika jamii.
 Mfano wa misamiati ya Kiswahili yenye asili ya lugha za
kigeni ni: Bakora, kitabu, meza ,shule, alasiri, n.k
Kuenea kwa Lugha
 Kuenea kwa lugha ni ongezeko la watumiaji wa lugha hiyo
kutoka katika jamii lugha ya asili.
 Hii inamaana kuwa, lugha inapopanuka kimatumizi kutoka
katika chimbuko lake la asili lugha hiyo husemwa kuwa
imeenea.
 Lugha ya Kiswahili ina asili ya kibantu na chimbuko lake ni
pwani ya Afrika Mashariki.
 Lakini leo hii Kiswahili kinazungumzwa katika sehemu
mbalimbali Afrika na duniani kwa ujumla. Hivyo Kiswahili
kimeenea.
 Zipo sababu za msingi zilizopelekea Kiswahili kuenea na
kufikia kilipo leo.
Kukua na Kuenea kwa Kiswahili Kabla ya
Uhuru
 Kukua na kuenea kwa Kiswahili kabla ya uhuru kunaweza
kutazamwa katika vipi vitatu;
Katika enzi ya Waarabu
Katika enzi ya wajerumani
Katika enzi ya waingereza
Kukua na
Kuenea kwa
Kiswahili enzi
ya Waarabu
Kiswahili Katika Enzi ya Waarabu
 Waarabu walipofika katika upwa wa Afrika Mashariki katika karne ya nane (8)
walikuta wabantu wakizungumza lugha zao za kibantu kikiwemo Kiswahili.
 Walijishughulisha na mambo mablimbali yaliyopelekea kukua na kuenea kwa
Kiswahili katika kipindi hicho.
 Mambo hayo ni kama ;
 Dini
 Biashara
 Elimu
 kuoana.
Dini
 Waarabu waliopata kufika katika upwa wa Afrika Mashariki katika
karne ya nane na kuendelea. Mbali na malengo mengine walikuja na
lengo la kueneza dini ya kiislamu.
 Iliwapasa kujifunza Kiswahili ili wakitumie kufanya mawaidha. Hivyo
kwa kufanya hivyo Kiswahili kilipata nafasi ya kutumika katika
kueneza dini ya kiislamu.
 Katika matumizi hayo misamiati kama sharia, kitabu, jehanamu,
mufti, maalim (mwalimu), na sahil (Swahili) iliongezwa katika
Kiswahili. Hapa Kiswahili kilipata nafasi ya kukua.
 Katika shughuli hizi za kidini Kiswahili kilitumika hadi bara ya Afrika
Mashariki. Mfano Kigoma na Tabora. Maeneo haya yote yalifikiwa na
waarabu. Huko kote walitumia Kiswahili. Hapa Kiswahili kilipata
kuenea.
 Hivyo, kuenezwa kwa dini ya kiislamu kulisaidia kukua na kuenea kwa
Kiswahili.
Jamii ya Bantu waliosilimu na kuwa waumini wa dini ya
Kiislamu katika karne ya 10 hadi 14. Hawa pia walipata
nafasi ya kukifahamu kiswahili.
Biashara
 Biashara ndio lengo kuu la ujio wa Waarabu katika pwani ya Afrika
Mashariki. Walifanya biashara kwa kubadilishana bidhaa na wenyeji
wa Afrika mashariki.
 Bidhaa kubwa walizoleta waarabu ilikuwa ni nguo, viungo vya chakula,
shanga, silaha na urembo.
 Bidhaa walizohitaji kutoka kwa waafrika ni pembe za ndovu, dhahabu,
watumwa na ngozi za wanyama.
 Katika shughuli hizi za kibiashara Kiswahili kilitumika. Hivyo misamiati
mingi iliongezeka katika lugha ya Kiswahili kutokana na uhitaji wa
biashara. Hivyo Kiswahili kilikua kimsamiati.
 Lakini pia waarabu walifanya biashara na jamii za bara ya Afrika
Mashariki. Hivyo iliwalazimu kuunda misafara ya kwenda na kurudi
kutoka bara. Walifika hadi Tabora, Kigoma hadi kongo. Huko kote
walitumia Kiswahili kama lugha ya mawasiliano. Kwa kufanya hivyo
Kiswahili kilienea.
 Hivyo, biashara na waarabu ilisaidia Kiswahili kukua na kuenea.
Ramani ya Afrika Mashariki Kuonesha
misafara ya kibiashara wakati wa
biashara kati ya wabantu na waarabu.
Mzagao huu ulisaidia Kiswahili kukua
na kuenea
Msafara wa watumwa kutoka bara
wakielekea pwani. Hawa
walichukuliwa utumwa. Biashara
hii ilichochea kukua na kuenea
kwa Kiswahili.
Elimu
 Kutambulishwa kwa dini ya kiislamu kulifungumana na utoaji wa elimu
ya dini.
 Madrasa zilianzishwa ili kutoa elimu hiyo kwa watoto na vijana wa
kibantu. Lugha iliyotumika kutoa elimu hiyo ni Kiswahili.
 Hapo misamiati kama kitabu, madrasa, darasa, bakora, juzuu n.k
iliongezeka katika lugha ya Kiswahili.
 Pia, hati ya kiarabu ilitumika kuandika lugha ya Kiswahili. Mfano
utenzi wa Fumo Lyongo Ulianza kwa kuandikwa kwa hati ya kiarabu.
Hivyo Kiswahili kilikua.
 Elimu hiiyo haikutolewa katika maeneo ya pwani tu bali iliendelea
kutolea hadi bara ya Afrika Mashariki. Maeneo kama Ujiji, Kondoa na
Tabora madrasa zilifunguliwa ili kutoa elimu hiyo ya dini. Hivyo
Kiswahili kilienea.
 Hivyo elimu iliyotolewa na waarabu kwa Wabantu ilisaidia kukua na
kuenea kwa Kiswahili.
Baadhi ya watoto wa kibantu
wakipata mawaidha ya dini
ya Kiislamu kwa Lugha ya
Kiswahili
Mfano wa Madrasa za mwazo
zilizotumiwa na waarabu
kufundisha elimu ya dini ya
Kiislamu
Ndoa
 Mbali na masuala ya biashara na dini waarabu walioana na wakazi wa
Afrika mashariki na kujenga makazi katika pwani hata bara ya Afrika
mashariki.
 Muunganiko huo wa Kifamilia ulisaidia kukuza lugha ya Kiswahili kwa
kuwa baadhi ya misamiati ya kiarabu iliibukia katika Kiswahili; mfano
neno chotara, ami n. k
 Watoto waliozaliwa katika ndoa hizo walikuwa ni chotara na
walizungumza Kiswahili.
 Kadri waarabu walivyosambaa ndivyo ndoa kati yao na wabantu
zilivyoongezeka na ndivyo lugha ya Kiswahili ilivyopata nafasi ya
kuzungumzwa zaidi na zaidi.
 Hivyo, ndoa kati ya waarabu na wabantu zilipelekea kukua nakuenea
kwa Kiswahili.
Kwa kuhitimisha…
 Biashara
 Dini
 Elimu na
 Ndoa
 Vyote kwa pamoja, katika kipindi cha utawala wa
waarabu, vilichangia katika kukuza na kueneza lugha ya
Kiswahili.
Kukua na
Kuenea kwa
Kiswahili enzi
ya
Wajerumani
 Wajerumani walifika Afrika Mashariki mnamo karne ya 19.
Waliichukua na kuitawala Tanganyika kama koloni.
 Wajerumani walipofika Tanganyika walikuta lugha ya
Kiswahili ndio lugha kuu katika sehemu kuu ya nchii
nzima. Misingi hii ilikuwa imejengwa na mwarabu katika
kipindi chake chote cha utawala wa Afrika Mashariki.
 Pamoja na vikwazo kadhaa kutoka Ujerumani lakini
hawakuwa na budi kuendelea kukitumia Kiswahili katika
nyanja mbalimbali za kiutawala na kiuchumi.
 Kwa nafasi yao, wajerumani walichangia kukua na kuenea
kwa Kiswahili kama ifuatavyo:
Utawala
 Shughuli za ki-utawala katika kipindi
hiki cha ukoloni wa mjerumani
Kiswahili kilitumika kama lugha ya
mawasiliano.
 Kila akida alilazimika kufahamu
kiswahili ili aweze kupewa jukumu la
kusimamia shughuli mbalimbali za
kiserikali.
 Kwa kuwa utawala wa Kijerumani
ulienea kila sehemu katika nchi ya
Tanganyika hivyo kiswahili kilienea
pia.
 Hivyo utawala umesaidia kuenea kwa
kiswahili.
Elimu
 Wajerumani walitoa elimu kwa
waafrika ili kuandaa wasaidizi
katika utawala wao.
 Shule hizi zilifundisha masomo
mbalimbali. Masomo yote
yalitolewa kwa lugha ya kiswahili.
 Wajerumani walijenga shule
sehemu kama; Tabora, Ujiji,
Kasangu, Tukuyu , Moshi n.k
 Kiswahili kilipata nafasi ya
kufahamika vyema katika sehemu
mbalimbali za Tanganyika kutokana
na elimu iliyokuwa ikitolewa.
Mahakama
 Ili kuweza kuwatawala waafrika
iliwapasa wajerumani kuweka
sharia mbalimbali na mahakama
yakusimamia sharia hizo.
 Mahakama zote nchini Tanganyika
ziliendeshwa kwa kutumia lugha ya
kiswahili.
 Hivyo lugha ya kiswahili ilitumika
katika sehemu kubwa ya
Tanganyika.
 Hivyo, kiswahili kilikuwa na kuenea
kwa kasi.
Mashamba na shughuli za Kiuchumi
 Wajerumani walianzisha mashamba
mengi na makubwa.
 Walilazimisha watu kutoka bara na
pwani kufanyakazi katika
mashamba hayo.
 Kwa kuwa watu walikuwa
wanatoka kwenye makabila
mbalimbali hivyo walizungumza
lugha tofauti tofauti.
 Wajerumani walilazimisha Kiswahili
kiwe lugha ya mawasiliano
miongoni mwa wafanyakazi hao.
 Hivyo Kiswahili kiliendelea kukua.
Shughuli za Kidini (Wamishenari)
 Wajerumani walisambaza dini ya
kikristo.
 Walitumia Kiswahili kufanya
mahubiri.
 Kwa kuwa makanisa yalisambaa
kila sehemu katika Tanganyika
hivyo Kiswahili nacho kilisambaa.
 Mashirika ya kimishenari ya
kijerumani yaliandika sarufi ya
Kiswahili ya kwanza.
 Hivyo Kiswahili kilikua.
Kukua na
Kuenea kwa
Kiswahili enzi
ya Waingereza
 Baada ya vita vya kwanza vya dunia, koloni la Tanganyika liliwekwa chini ya
utawala wa Waingereza.
 Waingereza walikuta mifumo ya kiutawala iliyowekwa na mjerumani, hivyo
wao nao waliiendeleza katika utawala wao.
 Kiswahili nacho kilienedelea kutumiwa na watawala hawa katika nyanja
mbalimbali za kiutawala, kielimu na kiuchumi kama njia ya mawasiliano baina
yao na wenyeji wa Tanganyika.
 matumizi haya ya Kiswahili yalipelea kuendelea kukua na kuenea kwa lugha
hii yenye asili ya pwani ya Afrika Mashariki.
 Sababu zilizosaidia kukua na kuenea kwa Kiswahili katika enzi za Waingereza
ni kama zifuatazo:
Kusanifisha Kiswahili
 Kusanifisha lugha ni kulinganisha
lugha na kuifanya ikubalike na
wazungumzaji wake.
 Waingereza walikisanifisha
Kiswahili kwa kuchagua kiunguja
kuwa Kiswahili fasaha kutoka
katika lahaja nyingi za Kiswahili.
 Kiunguja kilitumiwa katika nyaraka
za serikali, kufundishia mashuleni,
mahakamani na katika huduma
zote za kijamii.
 Kwa kufanya hivyo Kiswahili kilikua
na kuenea kwa kasi zaidi.
Elimu
 Waingereza nao pia walitoa elimu
kwa waafrika (watanganyika).
 Katika elimu hiyo Kiswahili
kilitumika kama lugha ya
kufundishia kuanzia darasa la
kwanza mpaka darasa la nne.
 Kuanzia darasa la tano hadi la kumi
na mbili Kiswahili kilifundishwa
kama somo.
 Kwa mfumo huu wa elimu Kiswahili
kilipata nafasi ya kukua na kuenea
katika sehemu kubwa ya
Tanganyika.
Shughuli za Kidini
 Madhehebu ya Kikristo yenye asili
ya Uingereza yalitambulishwa
nchini Tanganyika.
 Mfano dhehebu la Ki-Angrikana.
 Mbali na hayo, madhehebu
mengine ya kikristo yaliruhusiwa
kuendeleza shughuli zao za
kimishenari nchini Tanganyika.
 Mahubiri yalifanywa kwa Kiswahili.
 Walitafsiri biblia kutoka kingereza
kwenda lugha ya Kiswahili.
 Pia, walianzisha shule za ki-
seminari zilizotoa elimu kwa
Kiswahili.
 Hivyo Kiswahili kilikua na kuenea
kwa kasi
Vyombo vya Habari
 Waingereza walianzisha vyombo
mbalimbali vya habari kama redio
na magazeti.
 Madhumini makuu ya vyombo hivi
ilikuwa ni kuwapasha habari
wananchi katika masuala
mbalimbali.
 Kiswahili kilitumika katika kurusha
matangazo na kuandika habari
hizo.
 Mfano Redio Tanganyika ilianzishwa
na Gazeti la Mwangaza.
 Kupitia vyombo vya habari
Kiswahili kilikua na kuenea kwa
kasi nchini Tanganyika.
Jeshi na Vikosi vya Usalama
 Katika vikosi vya usalama kama
majeshi la KAR na jeshi la Polisi
Kiswahili kilitumika kama lugha ya
mawasiliano.
 Maofisa wa jeshi na askari wote
walikitumia Kiswahili katika
masuala yao ya kijeshi.
 Kwa kufanya hivyo Kiswahili
kilienea na kukua kwa kasi Zaidi.
Suala la Utawala
 Kama ilivyokuwa kwa wajerumani,
waingereza nao walilazimisha kila
chifu afahamu Kiswahili ili atumike
katika shughuli za kiutawala.
 Wafanyakazi wote katika ngazi ya
chini ya ajira serikalini iliwapasa
wafahamu Kiswahili.
 Vigezo hivi vilikuwa chachu ya
kukua na kuenea kwa Kiswahili
nchini Tanganyika wakati wa
utawala wa mkoloni.
Kwa kuhitimisha…
 Watawala hawa; waarabu, wajerumani na waingereza wamechangika
kwa kiasi kikubwa katika kukua na kuenea kwa lugha ya Kiswahili.
 Hoja kadhaa zilizojadiliwa katika uwasilishaji huu zinaonesha
mchango wao katika kukuza na kueneza Kiswahili.
Asanteni kwa kunisikiliza…

More Related Content

What's hot

What's hot (20)

Lahaja za kiswahili kwa ujumla
Lahaja za kiswahili kwa ujumlaLahaja za kiswahili kwa ujumla
Lahaja za kiswahili kwa ujumla
 
Uhuru wa Mtunzi wa Kazi za Fasihi
Uhuru wa Mtunzi wa Kazi za FasihiUhuru wa Mtunzi wa Kazi za Fasihi
Uhuru wa Mtunzi wa Kazi za Fasihi
 
Mjengo wa tungo 3
Mjengo wa tungo 3Mjengo wa tungo 3
Mjengo wa tungo 3
 
Uhifadhi wa fasihi simulizi
Uhifadhi wa fasihi simuliziUhifadhi wa fasihi simulizi
Uhifadhi wa fasihi simulizi
 
Sarufi Matamshi (Fonolojia)
Sarufi Matamshi (Fonolojia)Sarufi Matamshi (Fonolojia)
Sarufi Matamshi (Fonolojia)
 
CHIMBUKO LA FASIHI
CHIMBUKO LA FASIHICHIMBUKO LA FASIHI
CHIMBUKO LA FASIHI
 
MAENDELEO YA FASIHI SIMULIZI
MAENDELEO YA FASIHI SIMULIZIMAENDELEO YA FASIHI SIMULIZI
MAENDELEO YA FASIHI SIMULIZI
 
Mjengo wa tungo
Mjengo wa tungoMjengo wa tungo
Mjengo wa tungo
 
Uhakiki wa kazi za fasihi andishi
Uhakiki wa kazi za fasihi andishiUhakiki wa kazi za fasihi andishi
Uhakiki wa kazi za fasihi andishi
 
Utungaji wa kazi za fasihi
Utungaji  wa kazi za fasihiUtungaji  wa kazi za fasihi
Utungaji wa kazi za fasihi
 
Matumizi ya Lugha Kimuktadha
Matumizi ya Lugha KimuktadhaMatumizi ya Lugha Kimuktadha
Matumizi ya Lugha Kimuktadha
 
MATUMIZI YA SARUFI
MATUMIZI YA SARUFIMATUMIZI YA SARUFI
MATUMIZI YA SARUFI
 
TAFSIRI NA UKALIMANI
TAFSIRI NA UKALIMANITAFSIRI NA UKALIMANI
TAFSIRI NA UKALIMANI
 
Rejesta
RejestaRejesta
Rejesta
 
Lexical variation
Lexical variationLexical variation
Lexical variation
 
Mofolojia ya kiswahili
Mofolojia ya kiswahiliMofolojia ya kiswahili
Mofolojia ya kiswahili
 
Language families
Language familiesLanguage families
Language families
 
Uhusiano fonolojia vs mofolojia
Uhusiano fonolojia vs mofolojiaUhusiano fonolojia vs mofolojia
Uhusiano fonolojia vs mofolojia
 
USHAIRI WA KISWAHILI
USHAIRI WA KISWAHILIUSHAIRI WA KISWAHILI
USHAIRI WA KISWAHILI
 
5 language and dialect
5 language and dialect5 language and dialect
5 language and dialect
 

More from mussa Shekinyashi

More from mussa Shekinyashi (8)

Tafsiri na ukalimani
Tafsiri na ukalimaniTafsiri na ukalimani
Tafsiri na ukalimani
 
Evolution of Man (form one)
Evolution of Man (form one)Evolution of Man (form one)
Evolution of Man (form one)
 
Uhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penzi
Uhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penziUhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penzi
Uhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe penzi
 
Public Speaking Tips
Public Speaking TipsPublic Speaking Tips
Public Speaking Tips
 
UHAKIKI WA TAMTHILIYA - ORODHA
UHAKIKI WA TAMTHILIYA - ORODHAUHAKIKI WA TAMTHILIYA - ORODHA
UHAKIKI WA TAMTHILIYA - ORODHA
 
GENDER CONCEPTS - FORM TWO
GENDER CONCEPTS - FORM TWO GENDER CONCEPTS - FORM TWO
GENDER CONCEPTS - FORM TWO
 
UHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHA
UHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHAUHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHA
UHAKIKI WA RIWAYA - USIKU UTAKAPOKWISHA
 
Semantiki
SemantikiSemantiki
Semantiki
 

KUKUA NA KUENEA KWA KISWAHILI

  • 2. Kukua kwa Lugha.  Kukua kwa lugha ni kuongezeka kwa msamiati na kuimarika kwa sarufi ya lugha husika.  Lugha ya Kiswahili imepitia katika vipindi mbalimbali vya mabadiliko ya kimfumo wa kimaisha na kiutawala.  Watawala mbalimbali, kama waarabu, wajerumani na waingereza wamechangia kukua kwa lugha ya Kiswahili.  Katika vipindi hivi vyote lugha ya Kiswahili imeongeza msamiati, imeimarisha sarufi na kuimarisha matumizi yake katika jamii.  Mfano wa misamiati ya Kiswahili yenye asili ya lugha za kigeni ni: Bakora, kitabu, meza ,shule, alasiri, n.k
  • 3. Kuenea kwa Lugha  Kuenea kwa lugha ni ongezeko la watumiaji wa lugha hiyo kutoka katika jamii lugha ya asili.  Hii inamaana kuwa, lugha inapopanuka kimatumizi kutoka katika chimbuko lake la asili lugha hiyo husemwa kuwa imeenea.  Lugha ya Kiswahili ina asili ya kibantu na chimbuko lake ni pwani ya Afrika Mashariki.  Lakini leo hii Kiswahili kinazungumzwa katika sehemu mbalimbali Afrika na duniani kwa ujumla. Hivyo Kiswahili kimeenea.  Zipo sababu za msingi zilizopelekea Kiswahili kuenea na kufikia kilipo leo.
  • 4. Kukua na Kuenea kwa Kiswahili Kabla ya Uhuru  Kukua na kuenea kwa Kiswahili kabla ya uhuru kunaweza kutazamwa katika vipi vitatu; Katika enzi ya Waarabu Katika enzi ya wajerumani Katika enzi ya waingereza
  • 6. Kiswahili Katika Enzi ya Waarabu  Waarabu walipofika katika upwa wa Afrika Mashariki katika karne ya nane (8) walikuta wabantu wakizungumza lugha zao za kibantu kikiwemo Kiswahili.  Walijishughulisha na mambo mablimbali yaliyopelekea kukua na kuenea kwa Kiswahili katika kipindi hicho.  Mambo hayo ni kama ;  Dini  Biashara  Elimu  kuoana.
  • 7. Dini  Waarabu waliopata kufika katika upwa wa Afrika Mashariki katika karne ya nane na kuendelea. Mbali na malengo mengine walikuja na lengo la kueneza dini ya kiislamu.  Iliwapasa kujifunza Kiswahili ili wakitumie kufanya mawaidha. Hivyo kwa kufanya hivyo Kiswahili kilipata nafasi ya kutumika katika kueneza dini ya kiislamu.  Katika matumizi hayo misamiati kama sharia, kitabu, jehanamu, mufti, maalim (mwalimu), na sahil (Swahili) iliongezwa katika Kiswahili. Hapa Kiswahili kilipata nafasi ya kukua.  Katika shughuli hizi za kidini Kiswahili kilitumika hadi bara ya Afrika Mashariki. Mfano Kigoma na Tabora. Maeneo haya yote yalifikiwa na waarabu. Huko kote walitumia Kiswahili. Hapa Kiswahili kilipata kuenea.  Hivyo, kuenezwa kwa dini ya kiislamu kulisaidia kukua na kuenea kwa Kiswahili.
  • 8. Jamii ya Bantu waliosilimu na kuwa waumini wa dini ya Kiislamu katika karne ya 10 hadi 14. Hawa pia walipata nafasi ya kukifahamu kiswahili.
  • 9. Biashara  Biashara ndio lengo kuu la ujio wa Waarabu katika pwani ya Afrika Mashariki. Walifanya biashara kwa kubadilishana bidhaa na wenyeji wa Afrika mashariki.  Bidhaa kubwa walizoleta waarabu ilikuwa ni nguo, viungo vya chakula, shanga, silaha na urembo.  Bidhaa walizohitaji kutoka kwa waafrika ni pembe za ndovu, dhahabu, watumwa na ngozi za wanyama.  Katika shughuli hizi za kibiashara Kiswahili kilitumika. Hivyo misamiati mingi iliongezeka katika lugha ya Kiswahili kutokana na uhitaji wa biashara. Hivyo Kiswahili kilikua kimsamiati.  Lakini pia waarabu walifanya biashara na jamii za bara ya Afrika Mashariki. Hivyo iliwalazimu kuunda misafara ya kwenda na kurudi kutoka bara. Walifika hadi Tabora, Kigoma hadi kongo. Huko kote walitumia Kiswahili kama lugha ya mawasiliano. Kwa kufanya hivyo Kiswahili kilienea.  Hivyo, biashara na waarabu ilisaidia Kiswahili kukua na kuenea.
  • 10. Ramani ya Afrika Mashariki Kuonesha misafara ya kibiashara wakati wa biashara kati ya wabantu na waarabu. Mzagao huu ulisaidia Kiswahili kukua na kuenea Msafara wa watumwa kutoka bara wakielekea pwani. Hawa walichukuliwa utumwa. Biashara hii ilichochea kukua na kuenea kwa Kiswahili.
  • 11. Elimu  Kutambulishwa kwa dini ya kiislamu kulifungumana na utoaji wa elimu ya dini.  Madrasa zilianzishwa ili kutoa elimu hiyo kwa watoto na vijana wa kibantu. Lugha iliyotumika kutoa elimu hiyo ni Kiswahili.  Hapo misamiati kama kitabu, madrasa, darasa, bakora, juzuu n.k iliongezeka katika lugha ya Kiswahili.  Pia, hati ya kiarabu ilitumika kuandika lugha ya Kiswahili. Mfano utenzi wa Fumo Lyongo Ulianza kwa kuandikwa kwa hati ya kiarabu. Hivyo Kiswahili kilikua.  Elimu hiiyo haikutolewa katika maeneo ya pwani tu bali iliendelea kutolea hadi bara ya Afrika Mashariki. Maeneo kama Ujiji, Kondoa na Tabora madrasa zilifunguliwa ili kutoa elimu hiyo ya dini. Hivyo Kiswahili kilienea.  Hivyo elimu iliyotolewa na waarabu kwa Wabantu ilisaidia kukua na kuenea kwa Kiswahili.
  • 12. Baadhi ya watoto wa kibantu wakipata mawaidha ya dini ya Kiislamu kwa Lugha ya Kiswahili Mfano wa Madrasa za mwazo zilizotumiwa na waarabu kufundisha elimu ya dini ya Kiislamu
  • 13. Ndoa  Mbali na masuala ya biashara na dini waarabu walioana na wakazi wa Afrika mashariki na kujenga makazi katika pwani hata bara ya Afrika mashariki.  Muunganiko huo wa Kifamilia ulisaidia kukuza lugha ya Kiswahili kwa kuwa baadhi ya misamiati ya kiarabu iliibukia katika Kiswahili; mfano neno chotara, ami n. k  Watoto waliozaliwa katika ndoa hizo walikuwa ni chotara na walizungumza Kiswahili.  Kadri waarabu walivyosambaa ndivyo ndoa kati yao na wabantu zilivyoongezeka na ndivyo lugha ya Kiswahili ilivyopata nafasi ya kuzungumzwa zaidi na zaidi.  Hivyo, ndoa kati ya waarabu na wabantu zilipelekea kukua nakuenea kwa Kiswahili.
  • 14. Kwa kuhitimisha…  Biashara  Dini  Elimu na  Ndoa  Vyote kwa pamoja, katika kipindi cha utawala wa waarabu, vilichangia katika kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili.
  • 15. Kukua na Kuenea kwa Kiswahili enzi ya Wajerumani
  • 16.  Wajerumani walifika Afrika Mashariki mnamo karne ya 19. Waliichukua na kuitawala Tanganyika kama koloni.  Wajerumani walipofika Tanganyika walikuta lugha ya Kiswahili ndio lugha kuu katika sehemu kuu ya nchii nzima. Misingi hii ilikuwa imejengwa na mwarabu katika kipindi chake chote cha utawala wa Afrika Mashariki.  Pamoja na vikwazo kadhaa kutoka Ujerumani lakini hawakuwa na budi kuendelea kukitumia Kiswahili katika nyanja mbalimbali za kiutawala na kiuchumi.  Kwa nafasi yao, wajerumani walichangia kukua na kuenea kwa Kiswahili kama ifuatavyo:
  • 17. Utawala  Shughuli za ki-utawala katika kipindi hiki cha ukoloni wa mjerumani Kiswahili kilitumika kama lugha ya mawasiliano.  Kila akida alilazimika kufahamu kiswahili ili aweze kupewa jukumu la kusimamia shughuli mbalimbali za kiserikali.  Kwa kuwa utawala wa Kijerumani ulienea kila sehemu katika nchi ya Tanganyika hivyo kiswahili kilienea pia.  Hivyo utawala umesaidia kuenea kwa kiswahili.
  • 18. Elimu  Wajerumani walitoa elimu kwa waafrika ili kuandaa wasaidizi katika utawala wao.  Shule hizi zilifundisha masomo mbalimbali. Masomo yote yalitolewa kwa lugha ya kiswahili.  Wajerumani walijenga shule sehemu kama; Tabora, Ujiji, Kasangu, Tukuyu , Moshi n.k  Kiswahili kilipata nafasi ya kufahamika vyema katika sehemu mbalimbali za Tanganyika kutokana na elimu iliyokuwa ikitolewa.
  • 19. Mahakama  Ili kuweza kuwatawala waafrika iliwapasa wajerumani kuweka sharia mbalimbali na mahakama yakusimamia sharia hizo.  Mahakama zote nchini Tanganyika ziliendeshwa kwa kutumia lugha ya kiswahili.  Hivyo lugha ya kiswahili ilitumika katika sehemu kubwa ya Tanganyika.  Hivyo, kiswahili kilikuwa na kuenea kwa kasi.
  • 20. Mashamba na shughuli za Kiuchumi  Wajerumani walianzisha mashamba mengi na makubwa.  Walilazimisha watu kutoka bara na pwani kufanyakazi katika mashamba hayo.  Kwa kuwa watu walikuwa wanatoka kwenye makabila mbalimbali hivyo walizungumza lugha tofauti tofauti.  Wajerumani walilazimisha Kiswahili kiwe lugha ya mawasiliano miongoni mwa wafanyakazi hao.  Hivyo Kiswahili kiliendelea kukua.
  • 21. Shughuli za Kidini (Wamishenari)  Wajerumani walisambaza dini ya kikristo.  Walitumia Kiswahili kufanya mahubiri.  Kwa kuwa makanisa yalisambaa kila sehemu katika Tanganyika hivyo Kiswahili nacho kilisambaa.  Mashirika ya kimishenari ya kijerumani yaliandika sarufi ya Kiswahili ya kwanza.  Hivyo Kiswahili kilikua.
  • 22. Kukua na Kuenea kwa Kiswahili enzi ya Waingereza
  • 23.  Baada ya vita vya kwanza vya dunia, koloni la Tanganyika liliwekwa chini ya utawala wa Waingereza.  Waingereza walikuta mifumo ya kiutawala iliyowekwa na mjerumani, hivyo wao nao waliiendeleza katika utawala wao.  Kiswahili nacho kilienedelea kutumiwa na watawala hawa katika nyanja mbalimbali za kiutawala, kielimu na kiuchumi kama njia ya mawasiliano baina yao na wenyeji wa Tanganyika.  matumizi haya ya Kiswahili yalipelea kuendelea kukua na kuenea kwa lugha hii yenye asili ya pwani ya Afrika Mashariki.  Sababu zilizosaidia kukua na kuenea kwa Kiswahili katika enzi za Waingereza ni kama zifuatazo:
  • 24. Kusanifisha Kiswahili  Kusanifisha lugha ni kulinganisha lugha na kuifanya ikubalike na wazungumzaji wake.  Waingereza walikisanifisha Kiswahili kwa kuchagua kiunguja kuwa Kiswahili fasaha kutoka katika lahaja nyingi za Kiswahili.  Kiunguja kilitumiwa katika nyaraka za serikali, kufundishia mashuleni, mahakamani na katika huduma zote za kijamii.  Kwa kufanya hivyo Kiswahili kilikua na kuenea kwa kasi zaidi.
  • 25. Elimu  Waingereza nao pia walitoa elimu kwa waafrika (watanganyika).  Katika elimu hiyo Kiswahili kilitumika kama lugha ya kufundishia kuanzia darasa la kwanza mpaka darasa la nne.  Kuanzia darasa la tano hadi la kumi na mbili Kiswahili kilifundishwa kama somo.  Kwa mfumo huu wa elimu Kiswahili kilipata nafasi ya kukua na kuenea katika sehemu kubwa ya Tanganyika.
  • 26. Shughuli za Kidini  Madhehebu ya Kikristo yenye asili ya Uingereza yalitambulishwa nchini Tanganyika.  Mfano dhehebu la Ki-Angrikana.  Mbali na hayo, madhehebu mengine ya kikristo yaliruhusiwa kuendeleza shughuli zao za kimishenari nchini Tanganyika.  Mahubiri yalifanywa kwa Kiswahili.  Walitafsiri biblia kutoka kingereza kwenda lugha ya Kiswahili.  Pia, walianzisha shule za ki- seminari zilizotoa elimu kwa Kiswahili.  Hivyo Kiswahili kilikua na kuenea kwa kasi
  • 27. Vyombo vya Habari  Waingereza walianzisha vyombo mbalimbali vya habari kama redio na magazeti.  Madhumini makuu ya vyombo hivi ilikuwa ni kuwapasha habari wananchi katika masuala mbalimbali.  Kiswahili kilitumika katika kurusha matangazo na kuandika habari hizo.  Mfano Redio Tanganyika ilianzishwa na Gazeti la Mwangaza.  Kupitia vyombo vya habari Kiswahili kilikua na kuenea kwa kasi nchini Tanganyika.
  • 28. Jeshi na Vikosi vya Usalama  Katika vikosi vya usalama kama majeshi la KAR na jeshi la Polisi Kiswahili kilitumika kama lugha ya mawasiliano.  Maofisa wa jeshi na askari wote walikitumia Kiswahili katika masuala yao ya kijeshi.  Kwa kufanya hivyo Kiswahili kilienea na kukua kwa kasi Zaidi.
  • 29. Suala la Utawala  Kama ilivyokuwa kwa wajerumani, waingereza nao walilazimisha kila chifu afahamu Kiswahili ili atumike katika shughuli za kiutawala.  Wafanyakazi wote katika ngazi ya chini ya ajira serikalini iliwapasa wafahamu Kiswahili.  Vigezo hivi vilikuwa chachu ya kukua na kuenea kwa Kiswahili nchini Tanganyika wakati wa utawala wa mkoloni.
  • 30. Kwa kuhitimisha…  Watawala hawa; waarabu, wajerumani na waingereza wamechangika kwa kiasi kikubwa katika kukua na kuenea kwa lugha ya Kiswahili.  Hoja kadhaa zilizojadiliwa katika uwasilishaji huu zinaonesha mchango wao katika kukuza na kueneza Kiswahili.