Uwasilishaji huu unajikita katika kufafanua chimbuko na asili ya Kiswahili. Umejitosheleza kwa mujibu wa mukhtasari wa Kiswahili kwa kidato cha tatu na nne.
Kwa maswali zaidi au kama unahitaji kujifunza na mimi usisite kunipigia kwa namba unazoziona hapo.
1. CHIMBUKO NA ASILI YA
KISWAHILI(kidato cha tatu)
Mussa Shekinyashi
+255 743 98 98 29
2. UTANGULIZI
• Lugha ya Kiswahili ni moja ya lugha zenye asili
ya Afrika ambazo zimefikia upeo wa kutumiwa
kama lugha za kiutandawazi ndani na nje ya bara
la Afrika.
• Kiswahili kinatumika kama lugha ya taifa katika
mataifa mawili ya Afrika Mashariki; Tanzania na
Kenya.
• Katika ulimwengu wa teknolojia pia Kiswahili
kinatumika kama lugha ya kiteknolojia.
• Kwa ujumla, Kiswahili kimepaa na kuwa lugha
yenye watumiaji wengi zaidi kuliko lugha
nyingine yenye asili ya kiafrika.
• Lakini tujiulize maswali ya msingi…
4. Chimbuko
• Chimbuko ni neno linalorejelea
mahala kitu kilipoanzia.
• Tunapoangazia chimbuko la Kiswahili
tunajikita kutaka kujua ni wapi hasa
(kijiografia) Kiswahili kimetokea.
Asili
• Neno asili lina maana ya jinsi au
namna kitu kilivyotokea.
• Tunapoangalia asili ya Kiswahili
tutakuwa tunazingatia namna Kiswahili
kilivyoanza.
5. KUNA NADHARIA NNE (4) ZA CHIMBUKO NA ASILI YA KISWAHILI
Kiswahili ni Kikongo
Kiswahili ni kiarabu
Kiswahli ni Pijini na Creoli
Kiswahili Kibantu
6. KISWAHILI NI KIKONGO
Nadharia hii inafungamana na historia ya
wabantu.
Wanahistoria wanasema wabantu walihama
kutoka katika misitu ya Kongo ambako ndio
chimbuko lao.
Shughuli za kibiashara,ufugaji,kilimo na vita
ndio sababu za kuhama kwao.
Wabantu kutoka Kongo walisambaa katika
sehemu mbalimbali za Afrika ikiwemo Afrika
Mashariki hadi wakatika pwani.
Inasemekana kuwa walikuja na lugha yao
ambayo ndicho Kiswahili.
Hivyo Kiswahili ni Kikongo.
7. UDHAIFU WA NADHARIA HII…
• Hakuna uthibitisho wa lini hasa wabantu hawa walihama kutoka Kongo kuja pwani
ya Afrika Mashariki.
• Lugha huwa imara na thabiti zaidi kule ilikoanzia kuliko kule ilikopelekwa. Kiswahili
cha Kongo ni dhaifu kimatamshi na kimsamiati ukilinganisha na kile cha pwani ya
Afrika Mashariki.
• Hii inathibitisha kuwa Kiswahili hakikuanzia Kongo bali kilipelekwa.
8. KISWAHILI NI KIARABU
• Wapo baadhi ya wataalamu
waliopendekeza kuwa Kiswahili ni
lugha ya kiarabu.
• Wao wanatoa hoja kwamba
maingiliano baina ya waarabu na
wabantu yalipelekea kufifia na kufa
kwa vijilugha vyote vilivyokuwako
katika upwa wa Afrika Mashariki na
kiarabu kikashika hatamu.
• Wanathibitisha hoja yao kwa uwepo
wa msamiati wenye asili ya Kiarabu
kwa asilimia 30 katika lugha ya
Kiswahili.
9. UDHAIFU WA NADHARIA HII
• Mtazamo huu umesisitiza zaidi juu ya msamiati wa kiswahili wenye asili ya kiarabu
kama kigezo chake na kutupilia mbali vipengele kama vile matamshi,maumbo na
miundo ya sentensi.
• Kiswahili kama lugha nyingine kimekopa msamiati kukidhi mawasiliano. Hiyo
haiwezi kuwa sababu ya chenyewe kuwa Kiarabu.
10. KISWAHILI NI PIJINI NA KREOLI
• Pijini ni lugha ya kati inayozuka baada ya
lugha mbili zenye asili tofauti zinapokutana
kimatumizi.
• Pijini huweza kuzuka mahala ambapo
kuna makundi mawili au zaidi na kila kundi
likiwa na lugha yake.
• Ili kurahisisha mawasilano lugha hizi
huchanganyika na kuingiliana.
• Jambo hili huweza kusababisha kuzuka
kwa lugha ya mchanganyiko ambayo
inaeleweka na makundi yote mawili.
• Hivyo pijini huwapa watu hao uwezo wa
kuwasiliana. Lugha AB
Lugha
B
Lugha
A
11. KREOLI
• Ni Pijini iliyokomaa.
• Watu wanaozungumza pijini wanaweza kuishi pamoja wakazoeana na kuoana, kisha
wakazaa watoto.
• Watoto wakakuta pijini ikizungumzwa kama lugha ya wazazi wao.
• Kwao hao watoto hii itakuwa lugha ya kwanza.
• Ikifika hatua hii, lugha hii huitwa krioli.
12. HIVYO…
• Wanaoshikilia nadharia hii wanadai kuwa Kiswahili ni Pijini ambayo ilikoma na kuwa
Kreoli.
• Wanasema, ujio wa Waarabu katika pwani ya Afrika Mashariki ulipelekea kuundwa
kwa lugha ya kati (pijini) ambayo ilichanganya Kiarabu na Kibantu.
• Baada ya maingiliano ya kiutamaduni ikiwemo kuoana baina ya waarabu na
wabantu vizazi vilivyofuata vilitumia pijini hiyo kama lugha yao ya kwanza.
• Ikawa Kreoli.
• Hivyo ndivyo Kiswahili kilivyoanza.
• Kwa hiyo Kiswahili na Pijini na Kreoli ya Kibantu na Kiarabu.
13. UDHAIFU WA NADHARIA HII
• Mtazamo huu umeshindwa kuitaja kinaganaga hiyo lugha ya kibantu iliyochangamana na
Kiarabu kuunda Kiswahili. Na kama ipo ndio Kiswahili chenyewe.
• Mtazamo huu umesisitiza zaidi juu ya msamiati wa kiswahili wenye asili ya kiarabu kama
kigezo chake na kutupilia mbali vipengele kama vile matamshi,maumbo na miundo ya
sentensi.
• Kiswahili kingekuwa pijini au krioli inayotokana na lugha ya kibantu na kiarabu, basi sintaksia
yake ingefanana na ile ya kiarabu
• Pia, kama Kiswahili kingekuwa ni zao la uchangamano wa Kiarabu na lugha ya Kibantu basi
asilimia hamsini ya misamiati ya kiswahili ingekuwa na asili ya kiarabu.
• Tofauti na ilivyo ambapo:
Msamiati wa kibantu- 60%
Msamiati wa Kiarabu-30%
Lugha nyingine -10%
14. KISWAHILI NI KIBANTU
• Nadharia hii inashikilia msimamo kuwa
Kiswahili si kiarabu, pijini au kreoli na
wala si Kikongo bali Kiswahili ni lugha
ya kibantu.
• Lugha za Kibantu ni lugha zenye asili
ya Kiafrika, hasa zile zinazopatikana
kusini mwa jangwa la sahala.
• Wataalamu wanoshikilia nadharia hii
wanasema Kiswahili ni moja ya lugha
hizo.
• Kuthibitisha hoja yao wanatoa ushaidi
wa Kihistoria na Kiisimu.
16. UGUNDUZI WA ALI – IDRISI
• Huyu ni mwana Jeografia aliyepata
kuzunguka sehemu kubwa ya Bahari ya
Hindi katika karne ya 10.
• Katika maandiko yake yaliyogunduliwa
huko Sicily, katika mahakama ya Mfalme
Roger II yanaonesha kuwa alipata kufika
katika upwa wa Afrika Mashariki.
• Amevielezea visiwa vya Zanzibar kwa jina la
“UNGUJA”
• Huu ni ushahidi kuwa kabla ya ujio wa
Waarabu walioleta neno Zanzibar, Visiwa
hivi vilikuwa na jina ‘Unguja’.
• Hii ni wazi kwamba wakazi wa visiwa hivi
walikuwa na lugha yao.
• Lugha hiyo ndicho Kiswahili.
• Kwa hiyo Kiswahili si Kiarabu wala si pijini
bali ni Kibantu
17. USHAHIDI WA MARCO-POLO
• Huyu ni mwanajeogarfia wa Kizungu
aliyepata kusafiri sehemu mbalimbali
duniani.
• Katika maandiko yake anaonesha kuwa
alipata kutembelea Afrika Mashariki katika
karne ya 10 na kuendelea.
• Katika maandishi yake anazungumzia asili
ya watu aliowakuta Afrika Mashariki, lugha,
dini na vyakula vyao.
• Maelezo ya Marco Polo yanakiri uwepo wa
lugha ya watu wa Afrika Mashariki.
• Hakusema kuwa lugha hiyo Kiarabu bali
lugha ya kibantu.
• Lugha hiyo ndicho Kiswahili.
• Hivyo Kiswahili ni Kibantu wala si kiarabu.
18. USHAHIDI WA AL-MASUDI
• Huyu ni mwanajeografia na historia wa
Kiarabu.
• Naye alipata nafasi ya kufika katika Pwani
ya Afrika Mashariki katika karne ya 10.
• Katika maandiko yake amefafanua majina
ya viongozi wa pwani ya Afrika Mashariki
kuwa ni Wakilimi.
• Pia, alistaajabishwa kusikia kuwa watu
Waafrika waliitwa Wazanji na nchi yao
Zanjibar.
• Ushahidi huu wa Al-Masudi
unatudhihirishia kuwa hata waarabu
wenyewe waliotembelea Afrika Mashariki
walikuta waafrika wakitumia lugha yao
ingawa ilikuwa na jina la Kiarabu.
• Hivyo Kiswahili si Kiarabu bali ni Kibantu.
19. HISTORIA YA MJI WA KILWA
• Katika historia, habari zinaeleza kuwepo
kwa masultani wa Kilwa waliopewa
majina kama Mkoma watu Nguo Nyingi
Hasha Hazifiki.
• Majina haya yanathibitisha kuwepo kwa
matumizi ya Kiswahili kabla ya ujio wa
utawala wa Mwarabu.
• Hivyo Kiswahili si Kiarabu wa Pijini bali
ni lugha yenye asili ya Kibantu.
20. UTENZI WA FUMO LIYONGO
• Kisa cha shujaa Lyongo kilikuwa
kikighaniwa kama ushairi kwa karne nyingi
kabla hakijarekodiwa kwenye maandishi
mnamo karne ya 13.
• Uwepo wa kisa hiki katika utenzi
kinadhihirisha kuwepo kwa lugha ya
Kiswahili kabla ya ujio wa waarabu.
• Mfano wa beti zake:
“Liyongo Kitamkali,
Akabalighi vijali,
Akawa mtu wa kweli,
Na hiba huongeya.”
• Utenzi huu unathibitisha kuwa Kiswahili ni
lugha yenye asili ya Kiafrika.
21. HIVYO…
• Kama tulivyoona hapo awali. Historia inathibitisha kuwa Kiswahili ni lugha yenye asili
ya Kibantu.
• Watu mashuhuri waliopata kuitembelea Afrika Mashariki wanaafiki katika maandishi
yao kuwa Kiswahili kilipata kuwapo na kuongelewa kabla ya ujio wa wageni.
• Hivyo Kiswahili ni Lugha yenye asili ya Kibantu.
23. MISAMIATI
• Msamiati ni sehemu ya msingi ya lugha.
• Sehemu kubwa ya msamiati wa Kiswahili unafanana na ule wa lugha za kibantu.
• Hii inamaana kwamba, misamiati katika lugha ya Kiswahili inaelekea kuwiana kimatamshi na
hata katika viambishi vichache.
• Mfano:
• Mifano hapo juu inaonesha knamna ambavyo misamiati katika lugha ya Kiswahili
inavyoelekea kufanana na mingine katika lugha nyingine za kibantu.
• Hivyo Kiswahili ni moja ya lugha za kibantu.
KISWAHILI KISAMBAA KIKURYA KIJITA
mtu mdhu omonto omontu
Maji mazi amanche amanji
Moto moto omoro omulilo
24. TUNGO ZA KISWAHILI
• Muundo wa tungo sentensi katika Kiswahili unafanana na muundo wa sentensi
katika lugha nyingine za kibantu.
• Sentensi katika Kiswahili zinazingatia muundo wa KIIMA na KIARIFU, kadharika
sentensi katika lugha nyingine za kibantu.
• Kufanana kwa muundo wa tungo kati ya Kiswahili na lugha nyingine za kibantu
kunathibitisha kuwa Kiswahili ni moja ya lugha zenye asili ya kibantu.
KIIMA KIARIFU
KISWAHILI Juma anakula ugali
KIZIGUA Juma adya ugali
KISUKUMA Juma alelya bugali
KINDALI Juma akulya ubhughali
25. UPATANISHO CHA KISARUFI
• Katika kigezo hiki tunazingatia uhusiano uliopo kati ya NOMINO(viwakilishi) na viambishi
awali vya nafsi katika vitenzi vya Kiswahili tukifananisha na lugha nyingine za kibantu.
• Ukichunguza kwa makini utagundua kuwa viambishi katika vitenzi vya Kiswahili hubadilika
kutokana na maumbo ya umoja na wingi wa nomino au kiwakilishi katika sentenis.
• Tabia hii pia inajidhihirisha katika lugha nyingine za kibantu.
• Mfano:
• Hii inathibitisha kuwa kiswahili ni moja ya lugha za kibantu.
UMOJA WINGI
KISWAHILI Baba analima Baba wanalima
KINDALI Utata akulima Abhatata bhakulima
KIKURYA Tata ararema Batata bararema
KISAMBAA Tate ataima Tate wataima
26. MPANGILIO WA VIAMBISHI
• Vitenzi katika lugha za kibantu huundwa na MZIZI ambao huambikwa viambishi ili
kukamilisha maana yake.
• Kiswahili pia hufuata utaratibu huu. Vitenzi vyake huundwa na mzizi kisha
kuambikwa viambishi.
• Mfano:
• Katika mfano hapo juu utagundua kuwa mbali na kuthibitisha kuwa vitenzi vya
Kiswahili na vile vya lugha za kibantu vinaundwa na mzizi na viambishi lakini pia
utagundua vyote vinampangilio sawa.
• Yaani viambishi vya nafsi huanza kisha vinafuata vya njeo kisha mzizi.
• Hii inathibitisha kuwa Kiswahili ni moja ya lugha za kibantu.
KISWAHILI analima a-na-lim-a
KISAMBAA ataima A-ta- im-a
KIKURYA arerema A-re-rem-a
27. IDADI YA IRABU
• Kiswahili na lugha nyingine za kibantu, zote zina irabu ambazo ni:
a , e , I , o , u
• Hii inathibitisha kuwa Kiswahili ni Kibantu na wala si Kiarabu.
28. HIVYO…
• Kama tulivyoona katika ushahidi wa kiisimu, Kiswahili kina sifa sawa za kiisimu na
lugha nyingine kusini mwa jangwa la sahara.
• Hii inathibitisha kuwa Kiswahili ni KIBANTU.
29. HITIMISHO
• Kiswahili kimepitia historia kubwa sana kimaendeleo.
• Katika makala yetu tumeona nadharia mbalimbali zinazojaribu kuangalia chimbuko
na asili ya Kiswahili.
• Kati ya nadharia zote imethibitika kuwa Kiswahili ni lugha ya kibantu.
• Hivyo; Kwa asili Kiswahili ni lugha ya kibantu na chimbuko lake ni katika pwani ya
Afrika Mashariki.