2. MALENGO YA SOMO
• Kufikia mwisho wa somo:
• Tujikumbushe maana ya Fasihi Simulizi
• Tufahamu sifa bainifu za Fasihi Simulizi
• Tufahamu Njia za uhifadhi wa Fasihi Simulizi
tukizingatia: Ubora na athari (udhaifu) zake kwa
fasihi simulizi.
3. MAANA YA FASIHI SIMULIZI
• Fasihi simulizi ni aina ya fasihi inayowasilishwa
kwa njia ya mazungumzo ya mdomo.
• Aina hii ya fasihi imekuwepo tangu enzi na
enzi.
• Imekuwa ikirithishwa kutoka kizazi kimoja
hadi kingine kwa njia ya mazungumzo ya
mdomo.
• Mfano wa fasihi simulizi ni hadithi
tunazosimuliwa na wazazi wetu, nyimbo
tunazoimba, maigizo yanayoigizwa.
4. SIFA BAINIFU ZA FASIHI
SIMULIZI
• Huwasilishwa kwa njia ya mzungumzo ya mdomo.
• Huifadhiwa kichwani
• Humpa uhuru msanii wa kufanya mabadiliko kwa
kuzingatia mazingira na uhitaji.
• Huwa ni mali ya jamii nzima.
• Huwa na wakati maalum na pahala maalum pa
kuiwasilisha.
• Huwa inaruhusu fanani na hadhira kukutana ana
kwa ana.
• Huruhusu viungo vingine vya mwili kutumika
katika uwasilishaji.
5. UHIFADHI
• Fasihi inaweza kukusanywa na kuhifadhiwa
kwa njia zifuatazo :
• Kichwa
• Maandishi
• Kanda za kunasia sauti
• Kanda za video, televisheni na filamu za
sinema (CD,DVD na kompyuta)
6. KICHWA
• Kwa asili uhifadhi wa fasihi
simulizi hufanywa kwa vichwa
vya watu kutoka kizazi hadi
kizazi.
• Njia hii imetumika kwa kipindi
kirefu sana.
• Kutokana na njia hii fasihi
imeweza kuwepo kutoka
vizazi vya kale hadi hiki cha
sasa.
8. UDHAIFU/ ATHARI ZA UHIFADHI
WA KICHWA
• Kupungua kwa kumbukumbu za mhifadhi/fanani
• Kufa kwa fanani
• Fanani anaweza kubadilisha mambo muhimu katika
simulizi na hivyo kubadili kiini cha masimulizi hayo.
• Ukosekananji wa wahifadhi wa fasihi kwa kichwa. Ni
vigumu kupata watu wanaopenda na wanaoweza kuhifadhi
fasihi simulizi
9. MAANDISHI
• Njia hii imeimeza fasihi simulizi kwa manufaa ya
baadae.
• Ugunduzi wa alama za uandishi ndio uliopelekea
fasihi simulizi kuhifadhiwa katika maandishi.
• Leo hii ni vigumu kuifahamu kazi ya fasihi simulizi
iliyowekwa kwenye maandishi.
• Njia pekee ya kuipambanua ni kuangalia tabia za
fasihi simulizi ambazo ni: “paukwa…pakawa”au
“hadithi….hadithi njoo”
11. UDHAIFU/ATHARI YA UHIFADHI
WA MAANDISHI
• Uhifadhi kwa maandishi huwa na matatizo yafuatayo:
• Kukosekana kwa utendaji,sauti,kuimba vitabia.
• Kukosekana kwa uhusiano wa moja kwa moja kati ya
hadhira na fanani
• Kukosekana kwa mabadiliko ya mara kwa mara.
• Ufinyu wa hadhira, itakuwa na watu wachache tu, wale
wanaojua kusoma na kuandika.
• Inakuwa ni nyenzo ya kibiashara ambapo inahitaji
kugharamiwa.
12. KANDA ZA KUNASIA SAUTI
• Njia hii pia hutumika kuhifadhi fasihi simulizi.
• Hii ni teknolojia iliyochipukia baada ya maandishi.
• Ilikuwa na uwezo zaidi wa kuhifadhi uhalisia wa
fasihi simulizi ukilinganisha na njia ya uhifadhi kwa
maandishi.
• Katika njia hii kanda hutumika, kanda hizo hushika
sauti pamoja na vichombezo vyake.
14. UDHAIFU/ATHARI ZA KANDA ZA
KUNASIA SAUTI
• Sauti husikika, lakini…
• Ni vigumu kuona matendo ya fanani .
• Hadhira haishirikishwi
• Ni gharama kuipata
• Uhifadhi unahitajika uwe wa hali ya juu
• Kudumaa kwa kazi ilihifadhiwa, haitapata
mabadiliko kamwe.
15. KANDA ZA
VIDEO,TELEVISHENI,FILAMU ZA
SINEMA, KOMPYUTA, MTANDAO,
SIMU ZA MIKONONI, CD NA DVD
• Uhifadhi wa namna hii hujumuisha sura na sauti
zinazoonekana kwenye skirini ya video.
• Vifaa maalumu hutumika kutengeneza picha za
namna hiyo.
• Fasihi simulizi imeweza kuhifadhiwa katika vifaa
hivi.
• Hapa uhalisia wa fasihi simulizi hujitokeza zaidi
ukilinganisha na njia zile za mwanzo.
• Hapa matendo na sauti vinaonekana wazi.
20. SIMU YA
MKONONI
Hii ni njia rahisi ya kurekodi na
kusambaza kazi za fasihi simulizi
kupitia mitandao ya kijamii kama
facebook, whatsApp na mingineyo
21. UDHAIFU/ ATHARI YA NJIA HII
YA UHIFADHI
• Upungufu wa ushirikishwaji wa hadhira
• Njia hii ni ya gharama sana
• Haitabadilika kulingana na mahitaji ya hadhira
• Uhifadhi wa vifaa hivi ni wa gharama sana.
22. UMUHIMU WA KUHIFADHI KAZI
ZA FASIHI SIMULIZI
• Hukuza na kuendeleza utamaduni wa jamii.
• Zinasaidia katika kuvutia watalii
• Ni sehemu ya ajira.
• Kazi ya fasihi inapohifadhiwa huwa ni chachu
ya umoja wa kitaifa.