3. Mimi ni Mwislamu
Kwa jina la Mungu wa Rehema
hgfedc ba`_
: ¯ kji
Na mtu anataka dini nyingine zaidi ya
Uislamu wala kukubali kuwa wakati ni
mmoja wa wenye kukhasiri Akhera
Al-Imran: 85
4. Mimi ni Mwislamu
Copyright, distribution and translation are
reserved for every Muslim
Legal Deposit No. 22274 / 2008
International Serial 977-6157-64-5
For charitable distribution call:
0020101459613
For suggestions e-mail:
anamuslim@windowslive.com
WWW.Iam-Muslim.com
5. Mimi ni Mwislamu
(1) KUMWAMINI MWENYEZI
MUNGU
Mimi ni Mwislamu…
• Ninamwamini Mwenyezi Mungu
Pekee Asiye na mshirika na hakuna
mola mwingine isipokuwa Yeye,
Hakuzaa wala Hakuzaliwa, na
hakuna kamwe kifano chake.
• Ameumba mbingu na ardhi, Naye
Ndiye Anayezimiliki. Anayajua
yaliyofichikana na yenye kuonekana.
Yu Hai na Hafi, Anayasimamia
mambo yote milele na Halali.
• Ana Majina Mazuri Kabisa na Sifa za
Juu. Kati yake ni Majina tisini na tisa,
mwenye kuyajua na kuyadhibiti
vyema na akamwomba Mwenyezi
Mungu Kwayo, ataingia peponi.
• Kati yake ni Sifa za Upweke, kwani Yeye
Subhaanahu wa Taalaa ni Mmoja wa
Dhati, Sifa na Vitendo, Aliyepwekeka, Aliye
Pekee, Mkusudiwa, Mmiliki wa
ufalme.
6. Mimi ni Mwislamu
• Na Sifa za Utukufu, kwani Yeye ni
Mwenye hekima, Mwenye habari ya
kila jambo, Mwelekezaji wa manufaa,
Haki, wa Mwanzo, wa Mwisho, wa
Dhahiri, wa Siri, Mrithi, Mwenye
Kubakia, Mkwasi, Mtakasifu, Mwenye
Kushuhudia, Aliye Karibu, Mbora wa
Kupangilia, Mwadilifu, Nuru ya
mbingu na ardhi, Mwenye Utukufu na
Ukarimu.
• Na Sifa za Uadhama, kwani Yeye ni
Mshindi Asiyeshindika, Mwenye Sifa
zote Tukufu, Mwenye Uadhama,
Mwenye Sifa za Utukuzo, Mwenye
Kulazimisha, Mwenye Nguvu, Aliye
Imara, Mteza nguvu, Mweza, Mwenye
uwezo wa juu, Mwingi wa Kunusuru,
Aliye Juu, Aliye Juu ya vyote.
• Na Sifa za Uwezo, kwani Yeye ni
Mwingi wa Ujuzi, Mwenye Kusikia,
Mwenye kuona, Yu Hai,
Mwenye Kukamata, Mwenye Kukunjua,
Mwenye Kushusha, Mwenye
Kupandisha, Mwenye Kutukuza,
Mwenye Kudhalilisha, Mwenye Kutoa,
Mwenye Kuzuia, Mwenye Kunufaisha,
7. Mimi ni Mwislamu
Mwenye Kudhuru, Mwenye Kuhuisha,
Mwenye Kufisha, Mwenye Kutanguliza
na Mwenye Kuchelewesha.
• Na Sifa za Uumbaji, kwani Yeye ni
Muumbaji, Msanifu wa Maumbile,
Mtiaji Sura, Hakimpiti au Kumshinda
kitu, Mbunifu, Mwenye Kuanzisha,
Mwenye Kurejesha, Mwenye Kufufua,
Mwenye Kukusanya, Mpaji Mkuu,
Mfunguzi wa kila jambo, Mwingi wa
Kuruzuku, Mwenye Kutajirisha,
Mdhibiti wa idadi, Mwenye Kudhibiti
mambo, Mwenye Kuhifadhi, Mlinzi na
Muumbaji wa mbingu na ardhi bila
ruwaza.
• Sifa za Rehma, kwani Yeye ni Mwingi
wa Rehma, Mwingi wa Kurehemu,
Mwingi wa Huruma, Mwenye
Kuneemesha neema nzuri, Mwingi wa
Penzi, Mtenda Wema, Mwingi wa
Kughufiria, Mwenye Kusamehe, Mwingi
wa Kukubali toba, Mwenye Amani,
Mtoaji amani na imani, Mpole, Mwenye
Kulipa vyema, Mkarimu, Mwenye
Kuneemesha, Mwingi wa Kutoa,
Mwenye Kusaidia, Mwenye Kujibu,
8. Mimi ni Mwislamu
Mkunjufu, Mwingi wa subira, Mvumilivu
kwa Waja Wake, Latifu, Wakili, Mwenye
Kutoa Misaada, Mwenye Kuombwa
msaada na Mwenye Kukubali toba.
• Amemneemesha mwanadamu neema
nyingi zisizo na hesabu. Na hakuna
neema yoyote anayoneemeka nayo
mja ila hutoka kwa Mwenyezi Mungu
Pekee, kwani Yeye Ndiye Aliyemuumba
na Akampa uhai, Akamfanya asikie na
aone, Akamkirimu, kisha Akamruzuku
na Akamfanyia wema.
• Kwa ajili hiyo, ni lazima mja
amwabudu Mwenyezi Mungu Peke
Yake – nako ni kufuata amri Yake na
kuacha makatazo Yake – kwa kuwa
hastahiki yeyote kuabudiwa
isipokuwa Mwenyezi Mungu Peke
Yake.
• Vile vile, bila shaka Mwenyezi Mungu
Anazijua hali zote za mja kati ya
utiifu
9. Mimi ni Mwislamu
na uasi. Hivyo basi, ni wajibu moyo wa
mja ujae haiba kwa Mwenyezi Mungu
Mtukufu, utukuzo na mapenzi, na aone
haya kumwasi na aachane na maasi,
kwani Mwenyezi Mungu Humwona
wakati akiyafanya.
• Anafurahi kwa amali zake njema
zinazomkurubisha kwenye radhi za
Muumbaji wake Subhaanahuu wa
Taala. Hivyo huzidi kufanya amali
hizo hadi kufikia ngazi ya ihsani,
kwani imani huzidi kwa matendo
mema na hupungua kwa maasi.
• Asivutike kwenye matamanio, hawaa
au bid'a, bali avutike kwa Mwenyezi
Mungu Pekee huku akifuata
maamrisho ya Mtume Swalla Allaahu
Alayhi wa Aalihii wa Sallam.
Asitafute kwa amali yake starehe
ndogo ya dunia bali atafute kwayo
malipo toka kwa Mwenyezi Mungu tu.
• Aidha, hakika Mwenyezi Mungu Ana
huruma mno kwa mwanadamu kuliko
huruma ya mama kwa mwanaye. Na
rehma Yake imekienea kila kitu.
10. Mimi ni Mwislamu
Hivyo basi, ni wajibu kwa mja
amwombe na anyenyekee Kwake
katika haja zake za kidunia na za
kiakhera, na wala asimwombe yeyote
mwingine.
• Kwa vile hakuna faida yoyote ya
kumwomba asiye Mwenyezi Mungu,
kwa kuwa hamiliki uwezo ulio kamili
isipokuwa Mwenyezi Mungu, na
hakuna asikiaye ya siri na
minong'ono ila Mwenyezi Mungu, na
hakuna anayemiliki makadirio
isipokuwa Mwenyezi Mungu, basi
kwa maana hiyo, hakuna wa kujibu
dua isipokuwa Mwenyezi Mungu.
• Na kwa ajili hiyo, haijuzu kwa
Mwislamu kuliomba kaburi, au
kumwomba aliyezikwa humo
vyovyote awavyo, kwa kuwa yeye
hamsikii. Na kama hamsikii, basi ni
vipi atamjibu au kumnufaisha? Hakika
Mwenyezi Mungu Pekee Ndiye
Mwenye Kunufaisha na Mwenye
Kudhuru. Na kwa ajili hiyo, ni wajibu
kwa Mwislamu asijenge msikiti juu ya
makaburi, kwani Mtume Swalla
11. Mimi ni Mwislamu
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam
amelikataza hilo.
• Kadhalika, ni wajibu kwa mja
alinganishe kati ya udhaifu wake na
Nguvu za Mwenyezi Mungu Mtukufu,
na kati ya umasikini wake na Utajiri
wa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kati
ya ujinga wake na Elimu ya
Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kati ya
unyonge wake na Utukufu wa
Mwenyezi Mungu Mtukufu.
• Na ajue kwamba utukufu ni wa
Mwenyezi Mungu, Mtume Wake na
Waumini.
• Hivyo yampasa awe ni miongoni mwa
Waumini hawa ambao hawatawakali
isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu
Pekee, wala hawaombi msaada
isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu,
wala hawaombi kinga na kujilinda
isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu,
wala hawaombi msaada wa dharura
ila kwa Mwenyezi Mungu, wala
hawamwogopi isipokuwa Mwenyezi
Mungu, wala hawataraji isipokuwa
kwa Mwenyezi Mungu, wala
12. Mimi ni Mwislamu
hawamwombi isipokuwa Mwenyezi
Mungu, wala hawachinji isipokuwa
kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, wala
hawaweki nadhiri isipokuwa kwa ajili
ya Mwenyezi Mungu, wala hawaapi
isipokuwa kwa Jina la Mwenyezi
Mungu, wala hawaweki talasimu na
hirizi (amali), wala hawasadiki
wasemayo makuhani, watabiri
(wanajimu) na wachawi, na wala
hawawaendei.
• Na wao hawakosi rajua, na huwa na
tahadhari ya mponyoko wa ndimi zao
ili wasije kutelezea motoni.
Hawasemi: "Amependa Mwenyezi
Mungu na amependa fulani", "lau si
Mwenyezi Mungu na wewe",
"nimetawakali kwa Mwenyezi Mungu
na kwako". Bali waseme:
"Nimetawakali kwa Mwenyezi Mungu
Pekee", "Amependa Mwenyezi
Mungu kisha amependa fulani".
Maneno haya humsawazisha
Mwenyezi Mungu na waja Wake, na ni
katika shirki ndogo.
13. Mimi ni Mwislamu
• Na kama ilivyo wajibu kwetu
kumwamini Mwenyezi Mungu, ni
wajibu wetu vile vile tuwakatae
mataghuti.
• Na kigogo wa mataghuti ni shetani
na kila yule aliyeabudiwa badala ya
Mwenyezi Mungu naye akaridhia hilo.
• Na kati ya mataghuti hawa ni yule
aliyetunga sheria zinazoharamisha
Aliyoyahalalisha Mwenyezi Mungu,
au kuhalalisha Aliyoyaharamisha
Mwenyezi Mungu.
• Aidha, taghuti ni kila yule
aliyelingania hilo, au akawaamuru
watu hilo, au akahukumu kwa hilo,
kwa vile ametaadi na akavuka mpaka
wa kiumbe wa kusikia na kutii.
• Basi Allaah Pekee Ndiye
Aliyewaumba wanadamu, na Ndiye
Anayejua yanayowafaa, na kwa
hivyo, hakuna yeyote awezaye
kuwapangia sheria isipokuwa Yeye
tu.
14. Mimi ni Mwislamu
(2) KUWAAMINI MALAIKA
• Ninaamini kuwepo malaika ambao
Mwenyezi Mungu Amewaumba
kutokana na nuru, na Akawafanya
kuwa na mbawa mbili mbili, tatu
tatu, na nne nne. Nao hawali,
hawanywi, hawalali wala hawaoi.
Amewaamuru kufanya kazi na
kusimamia majukumu mbalimbali,
nao hutekeleza hayo.
• Malaika siku zote humtii Mwenyezi
Mungu bila kuchoka. Hawamwasi na
humwogopa Mola wao toka juu yao.
Kuna kati yao aliyesujudu toka siku
Alipoziumba Mwenyezi Mungu
mbingu na ardhi hadi siku ya Kiyama.
Na atakaponyanyua kichwa chake
atasema: "Subhaanak!
Hatujakuabudu ukweli wa
kukuabudu".
• Wao ni waja wa Mwenyezi Mungu na
si wanawake, na wala si wasaidizi
Wake, na wao watawaombea shifaa
15. Mimi ni Mwislamu
Waumini – kwa idhini ya Mwenyezi
Mungu – siku ya Kiyama.
Kati ya malaika hawa, wapo:
• Walinzi ambao huwalinda viumbe
na madhara.
• Watukufu waandishi ambao
huandika matendo ya wanadamu,
mema yao na mabaya yao.
• Wenye kumsabihi Mwenyezi
Mungu. Hawa humsabihi
Mwenyezi Mungu mchana na usiku
na hawachoki mpaka siku ya
Kiyama.
• Wenye kuvinjari ambao
huhudhuria vikao vya dhikri,
kisomo cha Qura-aan na vikao vya
elimu.
• Wabebaji Arshi ambao idadi yao ni
wanane. Ni viumbe wakubwa mno
kati ya viumbe wa Mwenyezi
Mungu. Ndege huruka toka ncha
ya sikio la mmoja wao hadi
shingoni kwa muda wa miaka mia
tano.
16. Mimi ni Mwislamu
• Malaika wa mauti anayezitoa roho
za viumbe kwa Amri ya Mwenyezi
Mungu. Huyu ana wasaidizi wake.
• Israfil atakayelipuliza baragumu,
kisha viumbe vyote vitakufa kabla
ya kutokea Kiyama. Kisha
litapulizwa jingine, na hapo
watasimama viumbe wakiangalia.
• Mikaili anayesimamia jukumu la
mvua.
• Ridhwaan ambaye ni mlinzi wa
Pepo. Yeye ana wasaidizi wake
walio mbioni kuwahudumia
Waumini Peponi.
• Maalik ambaye ni mlinzi wa moto.
Ana wasaidizi wake ambao
viongozi wao ni kumi na tisa.
Wana marungu ya chuma ya
kuwaadhibu makafiri motoni -
Mwenyezi Mungu Atuepushe na
hayo.
• Mkuu wa Malaika ni Jibril
aliyewakilishwa kupeleka wahyi
kwa Manabii na Mitume.
17. Mimi ni Mwislamu
• Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam alimwona katika
umbile lake. Kutokana na ukubwa
wake, alizifunika peo za mbingu.
Ana mbawa mia sita, naye ndiye
aliyekikamata kijiji cha Lut kwa
ncha ya ubawa wake,
akakinyanyua hadi juu mbinguni,
kisha akakipindua juu chini.
• Kuna malaika wengineo wengi
zaidi ya hawa, na hakuna ajuaye
askari wa Mola wako isipokuwa
Yeye tu.
:¯ ´ ³ ²± °
• Malaika huwapenda Waumini
ambao Mwenyezi Mungu
Huwapenda na huwaombea
maghfira.
• Malaika mbali na nguvu zao hizi
hupigana pamoja na Waumini.
18. Mimi ni Mwislamu
(3) KUVIAMINI VITABU
• Ninaviamini Vitabu vya Mwenyezi
Mungu Alivyoviteremsha kwa Mitume
Wake, na kwamba katika asili ya
kuteremshwa Kwake, ni Maneno ya
Mwenyezi Mungu Aliyowafunulia ili
waifikishe sheria na dini Yake. Vitabu
vikubwa zaidi ni:
Quraan Tukufu iliyoteremshwa
kwa Mtume wetu Muhammad
Swalla Allaahu Alayhi wa Aalihii wa
Sallam.
Injili iliyoteremshwa kwa Iysa
Alayhi Ssalaam.
Taurat iliyoteremshwa kwa
Musa Alayhi Ssalaam.
Zaburi iliyoteremshwa kwa
Daud Alayhi Ssalaam.
Sahifa zilizoteremshwa kwa
Ibrahim Alayhi Ssalaam.
19. Mimi ni Mwislamu
• Kati ya hivi, kuna vilivyopotolewa na
kubadilishwa kabla ya kushuka Qur-
aan.
• Na Qur-aan ndiyo iliyo juu ya Vitabu
hivi, na ndiyo yenye kuongoza sheria
zote na hukumu zake, na yenye
kuondosha yale yote yenye kwenda
kinyume na hukumu zake baada tu
ya kuteremka kwake.
• Na kwamba Mwenyezi Mungu
Hatokubali siku ya Kiyama ila amali
kupitia uongofu wa Qur-aan.
Hatokubali amali kwa kufuata Vitabu
vilivyotangulia baada ya kuteremka
Qur-aan kwa Mtume Muhammad
Swalla Allaahu Alayhi wa Aalihii wa
Sallam.
• Na kwamba Qur-aan ni Maneno ya
Mwenyezi Mungu ya miujiza. Maneno
haya yana utukufu wake, na wala
hayaingiliwi na batili kabla yake wala
baada yake. Mwenye kuyasema,
amesema kweli, na mwenye
kuhukumia kwayo, amefanya
uadilifu, na mwenye kuyafanyia kazi
20. Mimi ni Mwislamu
basi hakika ameongolewa katika njia
iliyonyooka, mwenye kushikamana
nayo amefuzu na kuokoka, na
mwenye kuyakengeuka atakuwa ni
katika wenye kuhiliki.
• Ni kwamba watu wa Qur-aan, hao
ndio watu wa Mwenyezi Mungu
waliokurubishwa Kwake, na kwamba
mbora zaidi wa watu ni yule
aliyejifundisha Qur-aan na
akawafundisha watu, kwani Qur-aan
hii itakuja siku ya Kiyama
ikimwombea shifaa kila aliyeisoma,
akaihifadhi na akaifanyia kazi, na
itawaombea watu wake Pepo.
• Qur-aan huzitwaharisha nyoyo
kutokana na shubha na matamanio
yanayozichafua, huzikurubisha kwa
Muumbaji Wake Subhaanahuu wa
Ta'alaa, na huzihimiza kufanya kazi
ili kufuzu na kupata neema za
kudumu milele.
• Kati ya adabu za kusoma Qur-aan ni:
Kuwa twahara na wudhuu.
21. Mimi ni Mwislamu
Kuelekea Kibla.
Kukaa kwa adabu na heshima.
Kutoisoma kwa haraka.
Kuwa na unyenyekevu.
Kuonyesha huzuni kwa
madhambi na kuvuka mipaka.
Kulia kutokana na kumwogopa
Mwenyezi Mungu na Utukufu wa
Maneno Yake.
Kusoma kwa sauti nzuri.
Kusoma kwa sauti ya chini ili
kutowabughudhi wenye kuswali.
Kuzingatia maana ya maneno.
Kuhudhurisha moyo.
Kutaamuli kwa kina Aayah za
Mwenyezi Mungu.
Tuwe na yakini kuwa
kusimamisha hukumu za Kitabu
hiki kwa watu ni moja kati ya
sababu za kumakinishwa katika
ardhi na kuwashinda maadui.
22. Mimi ni Mwislamu
Basi harakia ndugu yangu Mwislamu
kwenda kwa Mola wako, na kikamate
Kitabu hiki kwa hima. Kuwa na shime
asikutangulie yeyote kuelekea kwa
Mwenyezi Mungu, kwani Mwenyezi
Mungu Hufurahi zaidi kwa kurejea
kwako Kwake kuliko wanavyofurahi
watu kwa kurejea mtu wao aliyekuwa
mbali.
23. Mimi ni Mwislamu
(4) KUWAAMINI MITUME
• Ninawaamini Mitume wa Mwenyezi
Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu
Aliwateua Mitume kati ya wanadamu,
Akawafunulia Sheria Yake kwa njia ya
wahyi, na Akawaamuru kuifikisha kwa
watu, na kwamba mwenye kuwatii
ataingia peponi, na mwenye kuwaasi
ataingia motoni.
• Kisha Akawatilia nguvu kwa miujiza
yenye kuonyesha ukweli wao ili
iwasaidie mbele ya wakadhibishaji, na
ili iwe ni hoja kwao.
• Na kwamba Mtume wa mwanzo ni
Nuhu, na wa mwisho wao ni
Muhammad Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam.
24. Mimi ni Mwislamu
• Na kuwa Mitume hawa ni watu;
wanakula, wanakunywa,
wanaoa,wanaugua na wanakufa. Wao
ndio viumbe bora kabisa wa Mwenyezi
Mungu na wamehifadhiwa na maasi.
• Mitume wa Mwenyezi Mungu ni wengi.
Mwenyezi Mungu Amewataja baadhi
yao katika Qur-aan. Nao ni Muhammad
Swalla Allaahu Alayhi wa Aalihii wa
Sallam, Ibrahim Khalili wa Ar-
Rahmaan, Musa aliyesemeshwa na
Allaah, Iysa Neno la Mwenyezi Mungu
na Nuhu. Hawa ndio Mitume wenye
azma ya juu Rehma na Amani ziwe juu
yao. Pia Ismail, Is-haaq, Yakub,
Harun, Ayyub, Yunus, Sulayman,
Daawud, Yahya, Zakariya, Hud, Saleh,
25. Mimi ni Mwislamu
Yusuf, Shuayb, Ilyaas, Lut, Dhulkifl,
Idris, na wengi wengineo. Kati yao
kuna Aliowahadithia Mwenyezi Mungu
katika Qur-aan na wengineo
Hakuwahadithia.
• Jambo la kwanza walilolilingania
Mitume ni tawhid, na jambo kubwa
zaidi walilolikataza ni shirki, na wote
wamekuja na Uislamu na wito.
• wa tawhid. Lakini sheria zao na
mifumo ya kumwabudu Mwenyezi
Mungu Mtukufu ilitofautiana kutokana
na kutofautiana zama zao na nchi zao.
• Na kwamba Mitume walitoa bishara ya
kuja kwa Nabii Muhammad Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam na
26. Mimi ni Mwislamu
wakawaamrisha kaumu zao
kumwamini Muhammad Swalla Allaahu
Alayhi wa Aalihii wa Sallam
atakapotumwa kwao.
• Tofauti kati ya Rasuli (Mtume) na
Nabii ni kuwa Rasuli ni yule
aliyefunuliwa sheria mpya na
akaamrishwa kuifikisha kwa watu.
Ama Nabii, ni yule aliyetumwa ili
kuithibitisha na kuipitisha sheria ya
Rasuli aliyemtangulia.
• Ninaamini kuwa mbora wa Mitume
mbele ya Allaah ni Muhammad Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam
toka kwa mwana wa Ismaili bin
Ibrahim Alayhima Ssalaam. Allaah
Amemtuma kwa watu wote,
27. Mimi ni Mwislamu
Akahitimisha Unabii kwa Unabii wake,
na Utume kwa Utume wake.
• Akamtilia nguvu kwa miujiza,
Akamfanya bora kuliko Mitume wote.
Pia Ameufanya Utume wake kuwa
bora kuliko Utume wote uliotangulia,
na sheria yake kuwa bora kuliko
sheria zinginezo zilizopita, na Kitabu
chake Qur-aan kuwa bora kuliko
Vitabu vyote, na umati wake –
Waislamu – kuwa bora kuliko uma
nyinginezo.
• Na Mola wake Akampa mambo ambayo
Hakumpa yeyote katika Manabii
waliomtangulia. Kati ya mambo hayo
ni:
28. Mimi ni Mwislamu
(1) Al Wasiylah: Nayo ndiyo daraja ya
juu kabisa Peponi ambayo
Mwenyezi Mungu Amemwandalia
Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam.
(2) Al Kawthar: Nao ni mto Peponi
wenye kupita chini ya Arshi ya Ar
Rahman.
(3) Al Hawdh: Ni sehemu ambayo
Waislamu peke yao ndio
watakayokunywa siku ya Kiyama.
Siku ambayo watu watapatwa na
kiu kikali, na jasho litawafika hadi
magotini, viunoni na mabegani –
kila mmoja kwa mujibu wa amali
yake – na Waislamu watakunywa
hapo kwa vikombe atakavyowapa
29. Mimi ni Mwislamu
Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam kwa mikono yake
mitukufu. Baada ya hapo
hawatapatwa na kiu milele.
(4) Shafaa: Ni makamu ya kuhimidiwa
siku ya Kiyama. Hapo Mtume Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam
ataomba shifaa kwa Mwenyezi
Mungu ili Waislamu waliofanya
maasi watolewe motoni, na
hatobakia ndani ya moto yeyote
anayeshuhudia kwamba hapana
Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu
na Muhammad ni Mtume wa Allaah.
Aliyefanya maasi hatosalia milele
motoni, bali atatoka baada ya
kutakaswa na maasi yake.
30. Mimi ni Mwislamu
Aliyewaamini Manabii wote na wala
hakumwamini Muhammad Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam,
basi hatatoka motoni.
(5) Na kwamba Allaah Amemnusuru na
Akawanusuru askari wake na
wafuasi wake hadi siku ya Kiyama
kwa kuzagaza hofu ndani ya nyoyo
za maadui umbali wa mwendo wa
mwezi. Na hakuna Nabii yeyote
aliyepewa hili kabla yake
Muhammad Swalla Allaahu Alayhi
wa Aalihii wa Sallam.
(6) Na ardhi imefanywa kwake na
Waislamu kuwa msikiti (sehemu ya
kuswalia) na twahara, na
31. Mimi ni Mwislamu
haikufanywa hivyo kwa Manabii
waliomtangulia.
(7) Na Allaah Amemtuma kwa watu na
majini wote, lakini Mitume wengine
wametumwa maalumu kwa watu
wao tu.
(8) Na kuwa yeye ndiye wa mwanzo
kaburi lake kufunguka, na ndiye
mwombezi wa kwanza, na ndiye wa
kwanza kupewa shifaa, na ndiye wa
kwanza kugonga mlango wa Pepo.
Atakapougonga, mlinzi
wa Pepo Ridhwaan atamuuliza: "Nani
wewe?" Atajibu: "Muhammad". Ridhwaan
atamwambia: "Kwako nimeamrishwa
nisimfungulie yeyote kabla yako".
32. Mimi ni Mwislamu
Na kati ya miujiza ya Mtume Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam ni:
Kupasuka mwezi.
Alilirejesha jicho la Qatada
lilipopofuliwa siku ya Uhud, macho yake
yakarudi yakawa mazima kabisa.
Aliurejesha muundi wa Ibn Al
Hakam kama ulivyokuwa ulipovunjwa
siku ya Vita vya Badr.
Aliutaka mti utamke shahada,
nao ukatamka shahada mbili mara tatu
mbele ya kafiri, naye akasilimu.
Kigogo cha mti alichokuwa
akihutubia juu yake kililia wakati
alipokiacha na hakikunyamaza mpaka
alipoiweka mikono yake juu yake.
33. Mimi ni Mwislamu
Alikifanya chakula kidogo kuwa
kingi baina ya mikono yake miwili, na
wakaweza kula na kushiba zaidi ya
watu 80 chakula cha kujaa viganja
viwili.
Aliyafanya maji kidogo kuwa
mengi siku ya Hudaybiyah wakati jeshi
lilipobakiwa na bakuli moja tu ya maji.
Hapo Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam aliingiza mikono yake
ndani, maji yakaanza kububujika kati ya
vidole vyake kama chemchemu,
wakanywa maji Waislamu wote na
wakatawadhia maji hayo. Walikuwa
kiasi cha watu 1400.
Alipelekwa usiku hadi Msikiti
wa Al Aqsa, na kisha alipandishwa hadi
34. Mimi ni Mwislamu
mbingu za juu na kukomea Sidrat Al
Muntahaa.
Alielezea na kuhadithia habari
za umma zilizotangulia na Manabii wao
nailhali yeye hana kisomo; hajui
kusoma wala kuandika. Pia alielezea
matukio yatakayotokea siku za usoni
kwa kufunguliwa Fursi na Rome,
kusambaratishwa ufalme wa Kisra
aliyechanachana barua ya Mtume Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam
aliyomtumia, pamoja na miujiza
mingineyo mingi.
Muujiza mkubwa zaidi wa
Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa Aalihii
wa Sallam ni Qur-aan Tukufu. Ni
35. Mimi ni Mwislamu
muujiza utakaosalia hadi siku ya
Kiyama.
Kisha Allaah Ameunyanyua
utajo wake, Akaliandamisha jina la
Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa Aalihii
wa Sallam na Jina Lake Subhaanahuu
wa Taalaa, na Akaifanya shahada ya
kuwa hapana mola isipokuwa Allaah na
kwamba Muhammad ni Mtume wa
Mwenyezi Mungu kuwa ndio jambo la
kwanza analoingia nalo mja katika
Uislamu,na jambo la mwisho analotoka
nalo duniani. Basi yeyote ambaye neno
lake la mwisho litakuwa ni "Laailaaha
illa Allaah", ataingia peponi.
• Ni wajibu wetu kwa upande wa
Mtume wetu Swalla Allaahu Alayhi
36. Mimi ni Mwislamu
wa Aalihii wa Sallam tusilitangulize
neno la kiumbe yeyote juu ya neno
lake, au rai ya yeyote hata kama ana
sauti kwa watu. Na ikiwa watu
watakutangulia kuhamia kwake, basi
hama wewe kwenda katika sunnah
yake katika kila jambo lako na wala
usimfuate mwingine zaidi yake. Ni
wajibu wetu tushikamane sote
pembezoni mwa amri yake na tumtii,
kwani mwenye kumtii Mtume, basi
huwa amemtii Mwenyezi Mungu.
: GFEDCBA
• Na tusimwiite ila kwa kusema Mtume
wa Mwenyezi Mungu Swalla Allaahu
Alayhi wa Aalihii wa Sallam.
Tusiseme (Muhammad) basi.
37. Mimi ni Mwislamu
• Tujipambe kwa adabu zake, na
tumwige katika hali zake zote; kulala
kwake, kula kwake, kutembea
kwake, kuswali kwake, kufunga
kwake, kutoa kwake sadaka, na
jihadi yake.
• Na tumpende zaidi kuliko nafsi zetu,
wana wetu, wazazi wetu na watu
wote.
• Na tumpende kila yule anayempenda
Mtume wa Mwenyezi Mungu Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam
na kumfanya kiigizo chake, na
tumchukie kila yule anayemchukia
Mtume wa Mwenyezi Mungu Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam
na wala hawajibiki na sheria yake.
38. Mimi ni Mwislamu
• Hivyo basi, ni lazima kwa Mwislamu
awapende Waumini, awanusuru,
ajifananishe nao, ashughulikie
mambo yao, asaidiane nao katika
mambo ya kheri, na awafanye kuwa
marafiki zake wa dhati.
• Ni wajibu kwake awabughudhi
makafiri na ukafiri wao, asiwatii,
asiungane nao dhidi ya Waislamu,
wala asisaidiane nao katika ubatilifu
wao, na wala asishiriki katika
sikukuu zao. Ni haramu kwake
kuwadhulumu, na linalotakiwa ni
kuwatendea haki.
• Ni wajibu wetu tuwapende Mama wa
Waumini; Wakeze Mtume Swalla
Allaahu Alayhi wa Aalihii wa Sallam,
39. Mimi ni Mwislamu
na tuwapende Maswahaba Wake
Swalla Allaahu Alayhi wa Aalihii wa
Sallam, kwani wao ndio bora wa
watu baada ya Manabii.
• Pia ni wajibu wetu tuihuishe Sunnah
yake Mtume Swalla Allaahu Alayhi
wa Aalihii wa Sallam, tuidhihirishe
sheria yake, na tubalighishe
ulinganio wake kwa watu wote.
Kisha tusubiri maudhi na kero
zinazotupata katika kuyapigania
hayo, kwani hayo hayaepukiki.
• Kwa vile Mwenendo wa Mwenyezi
Mungu uliopita kwa viumbe Vyake
unahukumia kuwa hakuna Nabii au
walii yeyote aliyelingania haki hii ila
alifanyiwa uadui na kuudhiwa.
40. Mimi ni Mwislamu
• Zindukana ndugu yangu Mwislamu!
Maudhi ya makafiri yasikufanye
ukaiacha dini yako. Kwani Mtume wa
Mwenyezi Mungu Swalla Allaahu
Alayhi wa Aalihii wa Sallam
aliudhiwa wakati Maswahaba
walipokuwa wachache, nao pia
waliudhiwa wakafanya subira.
• Na wala usilegeze azma yako hata
kama watakwambia kuwa
unayoyazungumza ni upuuzi, una
misimamo migumu, au umepitwa na
wakati. Au wakisema: "ashachezewa
akili huyo". Kwani wewe una kiigizo
chema kwa Mtume wa Mwenyezi
Mungu, yeye ashaambiwa mshairi na
hata mwendawazimu.
41. Mimi ni Mwislamu
• Wala usisononeke ukiambiwa
mpotevu mwenye siasa kali. Hii ndio
tabia ya makafiri kwa Waumini.
:
((Na wanapowaona, husema hakika
hawa bila shaka ni wapotevu)).
• Ikiwa watu wako makundi mawili, je
haikutoshi wewe kuwepo katika
kundi aliloko Mtume wako
Muhammad Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam?!
• Achana nao hao mpaka ifike siku
ambayo dhalimu ataviuma vidole
vyake aseme: "Laiti mimi
ningeliifuata njia pamoja na Mtume".
42. Mimi ni Mwislamu
: ¯
• Wala usibabaike au kuchanganyikiwa
kama watakwambia kuwa wewe ni
gaidi au mwovu, kwani hayo ndio
madai ya madhalimu dhidi ya
Waumini duniani na akhera. Ni kuwa
pale Malaika watakapowaongoza
kwenda Jahannamu wakisunukia,
wataangalia humo kisha waseme:
: JIH GFEDCBA
((Na watasema: Mbona
hatuwaoni watu tuliokuwa
tukiwazingatia kuwa ni katika
waovu?))
43. Mimi ni Mwislamu
• Na hapa, Waumini (ambao makafiri
wamewaita kuwa ni waovu)
watawaita toka kwenye magorofa ya
juu kabisa ya Firdaws wakiwaambia:
: ¯ LKJIHGF
٤٤ : اف (( ا ر و و )) أن
((Hakika sisi tumeyakuta
Aliyotuahidi Mola wetu kuwa ni
kweli))
44. Mimi ni Mwislamu
(5) KUAMINI SIKU YA MWISHO
• Ninaiamini siku ya mwisho, nayo ni
iku ambayo dunia (nyumba ya amali)
itamalizika, na akhera (nyumba ya
malipo) itasimama, wema wakalipwa
Pepo, na waovu wakalipwa moto.
• Katika siku ya Kiyama, mizani
itawekwa, na kila mja atapewa
kitabu chake. Atakayepokea kitabu
chake kwa mkono wake wa kuume,
basi Mtume Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam atakuwa pamoja
naye Peponi. Ama yule atakayepokea
kitabu chake kwa mkono wake wa
kushoto, basi atakuwa pamoja na
45. Mimi ni Mwislamu
Firauni –laana ziwe juu yake–
motoni.
• Sirati itawekwa, atakayefanikiwa
kuivuka basi atafikia Peponi. Ama
ambaye kulabu zitamnyakua kutokana
na amali zake mbovu, basi
ataangukia motoni.
• Siku ya Kiyama ina dalili, ina alama
ndogo na ina alama kubwa.
• Miongoni mwa alama ndogo ni
kupotea uaminifu, kukithiri mauaji,
madaraka kukamatwa kwa mabavu
na mafasiki, na masuala muhimu
kuzungumziwa na wasiojua kitu.
• Na miongoni mwa alama kubwa ni
kuibuka Al Mahdi, kusimama ukhalifa
46. Mimi ni Mwislamu
wongofu utakaokwenda juu ya
misingi ya njia ya Utume kabla ya
kutokea Kiyama, na kudhihiri masihi
mwongo.
• Pia kuteremka Iysa Alayhi Ssalaam ili
awaongoze Waislamu, apigane na
makafiri, avunje vunje misalaba, aue
nguruwe, na azikatae dini zote
nyingine ila Uislamu tu.
• Basi haitobakia nyumba yoyote ya
mjini au ya mashambani ila
Mwenyezi Mungu Ataiingiza dini hii,
kwa heshima ya mwenye nguvu, au
kwa udhalili wa mnyonge.
• Vile vile kutoka Yaajuju na Maajuju.
Pia atatoka mnyama
47. Mimi ni Mwislamu
anayewasemesha watu, na jua
litachomoza toka magharibi, Qur-aan
itaondoshwa na mambo mengineyo.
• Basi yeyote atakayefanya amali ya
uzito wa atomu ikiwa ni ya kheri au
ni ya shari, ataiona siku ya Kiyama
ndani ya kitabu chake.
• Basi harakieni kwenye mambo ya
kheri kabla haujamalizka muda wa
kusajiliwa kwa kufa mja katika muda
ambao haujui yeyote ila Mwenyezi
Mungu Pekee.
• Wakamwosha jamaa zake,
wakamvisha sanda, wakamswalia,
wakamzika. Kisha akajiwa na Malaika
wawili; Munkari na Nakiyr,
48. Mimi ni Mwislamu
wakamkalisha kitako na kumwuuliza:
"Nani Mola wako? Nini dini yako?
Nani Nabii wako?"
• Ikiwa atajibu kuwa: "Allaah ni Mola
wangu, na Uislamu ndiyo dini yangu,
na Muhammad Swalla Allaahu Alayhi
wa Aalihii wa Sallam ndiye Nabii
wangu na Mtume wangu" – na Allaah
Akamwezesha hilo – basi
itafunguliwa katika kaburi lake
harufu ya rayhaan hadi peponi,
akaona mashukio yake huko, na
makasri yake na ufalme wake. Hapo
atashangilia kwa furaha kubwa, na
kaburi lake litapanuliwa upeo wa
macho.
49. Mimi ni Mwislamu
• Na ikiwa ni katika makafiri, basi
hatoweza kujibu chochote, kwani
majibu wakati huo si kwa akili au
werevu wa mtu.
• Bali Mwenyezi Mungu Huwathibitisha
na kuwaimarisha watu wa imani
wakati huo kwa yale
waliyoyatanguliza kati ya amali
njema zilizosimamia juu ya tawhid,
utekelezaji wa faradhi, kushiriki
jihadi, kutenda mema, kuamrisha
mema, kukataza mabaya, kutoa
sadaka, kusoma Qur-aan, kufunga
siku za joto kali, na kusimama
kuswali muda mrefu usiku wa baridi
kali.
50. Mimi ni Mwislamu
• Ama akiwa ni katika makafiri, basi
kaburi lake humbana hadi mbavu
zake zikaingiana katika mwili wake,
na kaburi lake huwa ni shimo katika
mashimo ya motoni kwa sababu ya
amali zake mbaya.
• Basi jitahidi ndugu yangu Mwislamu,
kwani leo ni amali na hakuna hisabu,
lakini kesho ni hisabu na hakuna
amali.
• Na siku hiyo, Waislamu watiifu
wataingia Peponi peke yao, kwa vile
Mwenyezi Mungu Hatoikubali dini
yoyote siku ya Kiyama isipokuwa
Uislamu.
51. Mimi ni Mwislamu
• Ndani ya Pepo kuna neema ambazo
hakuna sikio lililowahi kuzisikia, wala
jicho lililowahi kuziona, wala hata
kuwaziwa katika akili ya
mwanadamu. Neema zake zitasalia
milele wala hazitomalizika, na
waliomo humo hawatakufa milele.
Neema kubwa zaidi ya zote humo, ni
kuuangalia Uso wa Mwenyezi Mungu
Mola wa walimwengu wote.
• Na waasi, waovu na makafiri
wataingia motoni. Ndani ya moto,
kuna adhabu zisizoweza kuvumilika
Alizoziandaa Mwenyezi Mungu kwa
ajili ya makafiri. Milima mirefu thabiti
haiwezi kuzivumilia adhabu hizi, na
52. Mimi ni Mwislamu
hao wataadhibiwa humo bila
kupumzishwa.
• Na humo, wafuasi wa mataghuti
wataomba adhabu iongezwe
maradufu kwa wakubwa wao
waliowapoteza. Na hapo Mwenyezi
Mungu Ataamuru adhabu iongezwe
maradufu kwa wote.
• Basi thibiti ndugu yangu Mwislamu
juu ya haki hii, wala usidanganyike
kabisa kuona kuwa wavunjaji sheria
ni wengi zaidi, kwani ikiwa wewe
utawatii na ukawafuata wengi
waliomo ardhini, basi watakupoteza
njia ya Mwenyezi Mungu. Nawe pita
pamoja na wenye kupita kuelekea
kwa Mwenyezi Mungu.
53. Mimi ni Mwislamu
• Kwani kundi katika umma wa
Muhammad Swalla Allaahu Alayhi wa
Aalihii wa Sallam litaendelea kuwa
juu ya haki likiwa na nguvu, hawezi
kuwadhuru yeyote aliyekwenda nao
kinyume au aliyewasaliti mpaka siku
ya Kiyama.
• Basi ni mbinu zipi za kuzijua ngazi
hizo za kupanda juu, na kuokoka na
ngazi hizo za kuporomokea chini? Na
ni mbinu zipi za kuwafikia
waliotangulia wenye kukurubishwa,
na kujiweka mbali na wapingaji
wenye kuangamia? Bila shaka ni toba
ya kweli ya kusahihisha na
kurekebisha yaliyopita, na amali
njema za kuweka sawa umri
54. Mimi ni Mwislamu
uliosalia, na kuweka nia ya kweli ya
kunyooka na kutokengeuka.
• Basi kuwa pamoja na watu kwa
kiwiliwili chako, ukiuza, ukinunua,
ukioa na ukiiamirisha ardhi kwa yale
Aliyokuhalalishia Mwenyezi Mungu.
• Wala moyo wako usifungamane na
kitu chochote cha kidunia, bali nenda
na moyo wako pale ambapo
unatakikana uwe, huko chini ya Arshi
ya Ar Rahmaan, na sujudu kwa moyo
wako sijdah ambayo utaendelea
kuisujudu hadi siku ya Kiyama.
55. Mimi ni Mwislamu
(6) KUAMINI QADHAA NA QADARI
• Nako ni kuamini kwamba Mwenyezi
Mungu Anayajua yote yaliyomo
ulimwenguni, yote yanayofanyika na
yatakayotokea hadi siku ya Kiyama.
Hata chembe ndogo mno, Yeye
Hakosi kuijua. Na kwamba Yeye
Anavijua vitendo vya waja, riziki zao,
muda wao wa kuishi, na nani kati yao
atakuwa wa peponi, na nani kati yao
atakuwa wa motoni kabla
Hajawaumba.
• Na kwamba Mwenyezi Mungu
Ameyaandika makadirio haya katika
Lawh Al Mahfuudh kabla hata
Hajaziumba mbingu na ardhi kwa
miaka elfu hamsini, na kwamba Lawh
56. Mimi ni Mwislamu
Al Mahfuudh hii hakuna malaika wa
karibu au hata Nabii aliyetumwa
awezaye kuichungulia.
• Hata kijusi kinapokuwa ndani ya
tumbo la uzazi la mama yake,
Mwenyezi Mungu Huwaamrisha
Malaika waandike kama ni cha kike
au kiume, waandike na riziki yake,
amali yake, muda wake wa kuishi na
hatima yake (ima peponi au motoni).
Pia waandike mazuri na mabaya
atakayokabiliana nayo.
• Kisha unapoingia usiku wa cheo
(Laylatul Qadr), huteremka
makadirio ya mwaka mzima toka
Lawh al Mahfuudh kati ya ajali za
watu, riziki zao, nani kati yao atahiji
mwaka huo na mengineyo. Katika
57. Mimi ni Mwislamu
usiku huo, hukadiriwa mambo ya
mwaka mzima.
• Kisha huteremka makadirio ya kila
siku kwa nyakati zake na watu wake,
hapo Mwenyezi Mungu Huwanyanyua
watu na wengine Huwashusha.
• Na tuamini kuwa Mapendeleo ya
Mwenyezi Mungu ndiyo yawayo,
Alilolitaka huwa na Asilolitaka haliwi.
Mwenyezi Mungu Hana wa
kumshinda, na Yeye Ndiye Mwenye
kuzipindua nyoyo. Humwongoa
Amtakaye kwa fadhila Zake na rehma
Zake, na Humpoteza Amtakaye kwa
Uadilifu Wake na Hekima Yake,
kwani Yeye Ndiye Ajuaye zaidi nani
anastahiki uongofu na nani
anastahiki upotevu.
58. Mimi ni Mwislamu
• Na Mwenyezi Mungu Haulizwi yale
Ayafanyayo lakini watu huulizwa.
• Na tuamini kuwa Mwenyezi Mungu
Amekiumba kila kitu, na hakuna
chembe yoyote ndogo ulimwenguni
isipokuwa Mwenyezi Mungu
Ameiumba na Akaumba kutikisika
kwake na kutulia kwake.
• `Na kwamba Yeye Amewaumba waja
na vitendo vyao, na kwamba Yeye
Amewaumbia waja uwezo na
mapendeleo yao ili wajichagulie
wenyewe vitendo vyao.
• Na kwamba Mwenyezi Mungu
Mtukufu Amewaamuru viumbe Wake
wamtii, na Akawaahidi kuwapa Pepo
Yake wakifanya hivyo, na
Amewakataza kumwasi Yeye, na
59. Mimi ni Mwislamu
Akawapa onyo la kuwaingiza ndani
ya moto Wake wakifanya hivyo, na
wala Hakuwakalifisha kazi isipokuwa
ile ambayo wanaweza kuifanya. Na
hapo wakagawanyika makundi
mawili: Waumini na makafiri; kwa
hiari yao wenyewe, kwa mapendeleo
yao wenyewe na kwa uwezo wao
wenyewe, na yote hayo Mwenyezi
Mungu Amewaumbia.
• Na kwamba thawabu na adhabu
hutokana na kuifuata sheria, si kwa
kutangulia Elimu ya Mwenyezi Mungu
kwao. Basi yeyote atakayefanya amali
yoyote ya kheri ya uzito wa atomu,
atalipwa kwayo. Na yeyote atakayefanya
amali yoyote ya shari ya uzito wa
atomu, basi ataadhibiwa kwayo.
60. Mimi ni Mwislamu
• Na kwamba kinachozingatiwa ni
mwisho wa matendo, na kwamba kila
mja ni mwenye kuendeshwa katika
lile aliloumbiwa kati ya kufurahika
Peponi au kupata shakawa motoni.
• Na kwa ajili hiyo, ni wajibu kwa mja
aogope mwisho mbaya, na aendelee
daima kumwomba Mwenyezi Mungu
na amhitajie, Amhidi katika njia
iliyonyooka, na adumu kumwomba
Amsaidie katika kumtii, na ajilinde
Kwake na maasia, kwa vile mja hana
hila wala nguvu zozote za kuyafanya
hayo ila kwa Uwezo wa Mwenyezi
Mungu.
• Na kwamba Waumini Huridhia
Qadhaa ya Mwenyezi Mungu na
Qadari Yake; ya kheri yake na ya
61. Mimi ni Mwislamu
shari yake, katika misukosuko na
katika furaha, na wana yakini kuwa
hawezi yeyote kuwanufaisha
isipokuwa kwa Qadari ya Mwenyezi
Mungu, na wala hawadhuru
isipokuwa liwe lisha andikwa na
Mwenyezi Mungu.
• Na mja hatopata utamu wa imani
mpaka pale atakapojua kwamba
lililompata lisingekuwa la kumkosa,
na lililomkosa lisingekuwa la
kumpata.
Na mwisho naomba nikisema:
"Ninamhimidi Mwenyezi Mungu, na
ninamwomba Aniingize Peponi mimi na
Waislamu wengine, na Anilinde na moto
mimi na Waislamu wengine". Aamiyn.
63. Mimi ni Mwislamu
ed c b a ` _
k j ih g f
[٨٥:ان ]ل
Ù
anamuslim@windowslive.com Ø × ª Ø
WWW.Iam-Muslim.com
٢٠١٠ J ١٤٣١
و ق ا
٢٠٠٩L٢٢٢٧٤ W
٠١٢٠١٥٢٩٠٨ :ª W