SlideShare a Scribd company logo
1 of 2
Date: 14th April 2010

KUTOA SHUKURANI

UTANGULIZI.

     Siku ya leo ni siku kubwa sana, siku ya mothering Sunday.
     Ni siku ya kumshukuru Mungu kwa sababu ya akina mama na hasa
     wazazi wetu.
     Basi ni vizuri kujifundisha kuhusu kutoa shukurani na tutatumia Luka
     17:11- 19



NENO: Luka 17:11-19

     Yesu alipokuwa hapa ulimwenguni alienda akitenda mema kama jinsi
     anavyofanya hata sasa.
     Wakati huu aliwatendea wema wanaume kumi waliokuwa na ugonjwa wa
     ukoma. Ugonjwa huu ulikuwa mbaya sana kwa sababu watu wengine
     hawakutaka kuwakaribia. Lakini Yesu anatupenda hata jinsi tulivyo.
     Wagonjwa hawa walipomuona Yesu walisimama mbali. Pengine
     walifikiri Yesu atawapuuza kama wale watu wengine lakini Mungu wetu
     sio hivyo.
     Wagonjwa hawa walipaaza sauti zao kwa sababu ni vizuri kumwambia
     Bwana mahitaji yetu. Walimwambia awahurumie.
     Yesu alipowaona aliwahurumia na kuwaambia waende wajionnyeshe
     kwa makuhani nao wakatii sauti ya Bwana. Ni vizuri kuitii sauti ya
     Bwana kila wakati.
     Hawa walipokuwa wakienda waliponywa kwa sababu hakuna lolote
     linalomshinda Mungu wetu.
     Mmoja wao peke yake ndiye aliyerudi kumshukuru Yesu. Naye alikuwa
     msamaria. Aliona hakustahili kubarikiwa na Yesu hadi akarudi
     kumshukuru.
     Jambo hili likamshangaza Yesu kwa sababu ingawaje wote waliponywa
     ni mmoja tu alirudi kushukuru.
     Yesu akamwambia ya kwamba imani yake ndiyo ilimuokoa.
MAFUNDISHO:
Katika hadithi hii twaweza kujifundisha mambo yafuatayo:

   1. Hata sasa Yesu yuko hapa na anaenda akitenda mema. Hata hapo mbeleni
      ameenda akitenda mema. Ametupa wazazi wetu. Ametupa watoto.
      Ametupa waume na wake. Ametuponya magonjwa na kutukinga na hatari
      zote. Hakika ametupa mambo mengi kiasi cha kwamba hatuwezi
      kuelezea yote.
   2. Tunapaswa kila wakati kumwendea Yesu kwa maombi. Tupaaze sauti
      zetu tumwite Bwana kama vile wale wanaume kumi walivyofanya.
      Tuombe bila kukoma ili nyumba zetu zisimame na kanisa letu lizidi pia
      kusimama wima. Naye Yesu ataturehemu.
   3. Ni vizuri kuitii sauti ya Mungu. Wenye ukoma hawa walitii walipoambia
      waende wakajionyeshe kwa makuhani. Basi hata nasi tunaposikia sauti ya
      Bwana tusifanye mioyo yetu kuwa migumu.
   4. Jambo kubwa sana ni kumshukuru Mungu kwa yote aliotutendea. Ni
      mara ngapi umemshukuru Mungu kwa yale yote aliokutendea?
   5. Siku ya mothering Sunday ilianzishwa miaka mingi liyopita ili
      kuwashukuru akina mama wazazi wetu. Siku hii inaadhimishwa jumapili
      ya nne wakati wa saumu. Watoto huwashukuru wazazi wao kwa sababu
      ya kuwazaa na kuwatunza miaka yote.
   6. Leo tunashukuru Mungu kwa sababu ya akina mama. Na hatuwezi
      kwenda mbele ya Mungu mikono mitupu. Kwa hivyo tuliwapa bahasha
      ili tuweze kumshukuru Mungu. Lakini ningewaomba baada ya service
      tukawashukuru wazazi wetu kwa njia yoyote. Pengine tuwatembelee na
      kupelekea kitu. Nanyi waume wetu tufanyieni kitu leo.
   7. Jambo la mwisho tunaloona hapa katika somo hili ni kwamba imani ni
      kitu cha maana sana. Wenye ukoma walipona kwa sababu ya imani. Hata
      nasi tutatendewa mambo makubwa na Mungu kwa sababu ya imani yetu.

   Basi nikimaliza nawaomba tumshukuru Mungu na hata akina mama kwa
   yote waliotutendea.

More Related Content

Featured

Social Media Marketing Trends 2024 // The Global Indie Insights
Social Media Marketing Trends 2024 // The Global Indie InsightsSocial Media Marketing Trends 2024 // The Global Indie Insights
Social Media Marketing Trends 2024 // The Global Indie Insights
Kurio // The Social Media Age(ncy)
 
Good Stuff Happens in 1:1 Meetings: Why you need them and how to do them well
Good Stuff Happens in 1:1 Meetings: Why you need them and how to do them wellGood Stuff Happens in 1:1 Meetings: Why you need them and how to do them well
Good Stuff Happens in 1:1 Meetings: Why you need them and how to do them well
Saba Software
 

Featured (20)

Content Methodology: A Best Practices Report (Webinar)
Content Methodology: A Best Practices Report (Webinar)Content Methodology: A Best Practices Report (Webinar)
Content Methodology: A Best Practices Report (Webinar)
 
How to Prepare For a Successful Job Search for 2024
How to Prepare For a Successful Job Search for 2024How to Prepare For a Successful Job Search for 2024
How to Prepare For a Successful Job Search for 2024
 
Social Media Marketing Trends 2024 // The Global Indie Insights
Social Media Marketing Trends 2024 // The Global Indie InsightsSocial Media Marketing Trends 2024 // The Global Indie Insights
Social Media Marketing Trends 2024 // The Global Indie Insights
 
Trends In Paid Search: Navigating The Digital Landscape In 2024
Trends In Paid Search: Navigating The Digital Landscape In 2024Trends In Paid Search: Navigating The Digital Landscape In 2024
Trends In Paid Search: Navigating The Digital Landscape In 2024
 
5 Public speaking tips from TED - Visualized summary
5 Public speaking tips from TED - Visualized summary5 Public speaking tips from TED - Visualized summary
5 Public speaking tips from TED - Visualized summary
 
ChatGPT and the Future of Work - Clark Boyd
ChatGPT and the Future of Work - Clark Boyd ChatGPT and the Future of Work - Clark Boyd
ChatGPT and the Future of Work - Clark Boyd
 
Getting into the tech field. what next
Getting into the tech field. what next Getting into the tech field. what next
Getting into the tech field. what next
 
Google's Just Not That Into You: Understanding Core Updates & Search Intent
Google's Just Not That Into You: Understanding Core Updates & Search IntentGoogle's Just Not That Into You: Understanding Core Updates & Search Intent
Google's Just Not That Into You: Understanding Core Updates & Search Intent
 
How to have difficult conversations
How to have difficult conversations How to have difficult conversations
How to have difficult conversations
 
Introduction to Data Science
Introduction to Data ScienceIntroduction to Data Science
Introduction to Data Science
 
Time Management & Productivity - Best Practices
Time Management & Productivity -  Best PracticesTime Management & Productivity -  Best Practices
Time Management & Productivity - Best Practices
 
The six step guide to practical project management
The six step guide to practical project managementThe six step guide to practical project management
The six step guide to practical project management
 
Beginners Guide to TikTok for Search - Rachel Pearson - We are Tilt __ Bright...
Beginners Guide to TikTok for Search - Rachel Pearson - We are Tilt __ Bright...Beginners Guide to TikTok for Search - Rachel Pearson - We are Tilt __ Bright...
Beginners Guide to TikTok for Search - Rachel Pearson - We are Tilt __ Bright...
 
Unlocking the Power of ChatGPT and AI in Testing - A Real-World Look, present...
Unlocking the Power of ChatGPT and AI in Testing - A Real-World Look, present...Unlocking the Power of ChatGPT and AI in Testing - A Real-World Look, present...
Unlocking the Power of ChatGPT and AI in Testing - A Real-World Look, present...
 
12 Ways to Increase Your Influence at Work
12 Ways to Increase Your Influence at Work12 Ways to Increase Your Influence at Work
12 Ways to Increase Your Influence at Work
 
ChatGPT webinar slides
ChatGPT webinar slidesChatGPT webinar slides
ChatGPT webinar slides
 
More than Just Lines on a Map: Best Practices for U.S Bike Routes
More than Just Lines on a Map: Best Practices for U.S Bike RoutesMore than Just Lines on a Map: Best Practices for U.S Bike Routes
More than Just Lines on a Map: Best Practices for U.S Bike Routes
 
Ride the Storm: Navigating Through Unstable Periods / Katerina Rudko (Belka G...
Ride the Storm: Navigating Through Unstable Periods / Katerina Rudko (Belka G...Ride the Storm: Navigating Through Unstable Periods / Katerina Rudko (Belka G...
Ride the Storm: Navigating Through Unstable Periods / Katerina Rudko (Belka G...
 
Barbie - Brand Strategy Presentation
Barbie - Brand Strategy PresentationBarbie - Brand Strategy Presentation
Barbie - Brand Strategy Presentation
 
Good Stuff Happens in 1:1 Meetings: Why you need them and how to do them well
Good Stuff Happens in 1:1 Meetings: Why you need them and how to do them wellGood Stuff Happens in 1:1 Meetings: Why you need them and how to do them well
Good Stuff Happens in 1:1 Meetings: Why you need them and how to do them well
 

Kushukuru

  • 1. Date: 14th April 2010 KUTOA SHUKURANI UTANGULIZI. Siku ya leo ni siku kubwa sana, siku ya mothering Sunday. Ni siku ya kumshukuru Mungu kwa sababu ya akina mama na hasa wazazi wetu. Basi ni vizuri kujifundisha kuhusu kutoa shukurani na tutatumia Luka 17:11- 19 NENO: Luka 17:11-19 Yesu alipokuwa hapa ulimwenguni alienda akitenda mema kama jinsi anavyofanya hata sasa. Wakati huu aliwatendea wema wanaume kumi waliokuwa na ugonjwa wa ukoma. Ugonjwa huu ulikuwa mbaya sana kwa sababu watu wengine hawakutaka kuwakaribia. Lakini Yesu anatupenda hata jinsi tulivyo. Wagonjwa hawa walipomuona Yesu walisimama mbali. Pengine walifikiri Yesu atawapuuza kama wale watu wengine lakini Mungu wetu sio hivyo. Wagonjwa hawa walipaaza sauti zao kwa sababu ni vizuri kumwambia Bwana mahitaji yetu. Walimwambia awahurumie. Yesu alipowaona aliwahurumia na kuwaambia waende wajionnyeshe kwa makuhani nao wakatii sauti ya Bwana. Ni vizuri kuitii sauti ya Bwana kila wakati. Hawa walipokuwa wakienda waliponywa kwa sababu hakuna lolote linalomshinda Mungu wetu. Mmoja wao peke yake ndiye aliyerudi kumshukuru Yesu. Naye alikuwa msamaria. Aliona hakustahili kubarikiwa na Yesu hadi akarudi kumshukuru. Jambo hili likamshangaza Yesu kwa sababu ingawaje wote waliponywa ni mmoja tu alirudi kushukuru. Yesu akamwambia ya kwamba imani yake ndiyo ilimuokoa.
  • 2. MAFUNDISHO: Katika hadithi hii twaweza kujifundisha mambo yafuatayo: 1. Hata sasa Yesu yuko hapa na anaenda akitenda mema. Hata hapo mbeleni ameenda akitenda mema. Ametupa wazazi wetu. Ametupa watoto. Ametupa waume na wake. Ametuponya magonjwa na kutukinga na hatari zote. Hakika ametupa mambo mengi kiasi cha kwamba hatuwezi kuelezea yote. 2. Tunapaswa kila wakati kumwendea Yesu kwa maombi. Tupaaze sauti zetu tumwite Bwana kama vile wale wanaume kumi walivyofanya. Tuombe bila kukoma ili nyumba zetu zisimame na kanisa letu lizidi pia kusimama wima. Naye Yesu ataturehemu. 3. Ni vizuri kuitii sauti ya Mungu. Wenye ukoma hawa walitii walipoambia waende wakajionyeshe kwa makuhani. Basi hata nasi tunaposikia sauti ya Bwana tusifanye mioyo yetu kuwa migumu. 4. Jambo kubwa sana ni kumshukuru Mungu kwa yote aliotutendea. Ni mara ngapi umemshukuru Mungu kwa yale yote aliokutendea? 5. Siku ya mothering Sunday ilianzishwa miaka mingi liyopita ili kuwashukuru akina mama wazazi wetu. Siku hii inaadhimishwa jumapili ya nne wakati wa saumu. Watoto huwashukuru wazazi wao kwa sababu ya kuwazaa na kuwatunza miaka yote. 6. Leo tunashukuru Mungu kwa sababu ya akina mama. Na hatuwezi kwenda mbele ya Mungu mikono mitupu. Kwa hivyo tuliwapa bahasha ili tuweze kumshukuru Mungu. Lakini ningewaomba baada ya service tukawashukuru wazazi wetu kwa njia yoyote. Pengine tuwatembelee na kupelekea kitu. Nanyi waume wetu tufanyieni kitu leo. 7. Jambo la mwisho tunaloona hapa katika somo hili ni kwamba imani ni kitu cha maana sana. Wenye ukoma walipona kwa sababu ya imani. Hata nasi tutatendewa mambo makubwa na Mungu kwa sababu ya imani yetu. Basi nikimaliza nawaomba tumshukuru Mungu na hata akina mama kwa yote waliotutendea.