1. Paper 320/2
Karatasi ya Pili
Tamthilia
Aprili 2017
Saa 3
KABALE DIOCESE JOINT MOCK EXAMS 2017
TAMTHILIA
UGANDA ADVANCED CERTIFICATE OF EDUCATION
Muda: Saa 3
Maagizo kwa watahiniwa:
• Karatasi hii ina sehemu nne; A,B,CH, na D. Mtahiniwa anapaswa
kujibu maswali Matatu Kwa Jumla; swali moja lazima litoke
sehemu D, na mengine mawili ya chaguliwe kutoka sehemu A,B,na
CH.
• Mtahiniwa asichague maswali zaidi ya moja kutoka sehemu moja.
SEHEMU: A
Juliasi Kaizari: William Shakespeare
Ama
1. a). “Kifo cha Kaizari kilazima”. Jadili ukweli wa kauli hii. (alama 18)
b). “Juliasi Kaizari si mfano mzuri kwa viongozi wa leo” Jadili. (alama 15)
2. a). Kwa nini Marulo na Flavi wa hasira kubwa mchezo wa Juliasi Kaizari
unapoanza. (alama 6).
b). Eleza kukutana kwa Kaizari na Mtabiri. (alama 8).
c) . Kisa hiki kinadhihirisha nini kuhusu tabia ya Juliasi Kaizari? (alama 9)
d). Ni mbinu gani zinazotumiwa na Kasio kumshawishi Buruto
kujiunga na mahaini wengine? (alama 10).
1
2. Au
Ngungi Wa Thiong Na Micere Mugo: Mazalendo Kimathi
3. a). Kwa kurejelea tamthilia ya Mzalendo Kimathi ,eleza ni kwa nini
Wafrika walishindwa katika harakati zao za ukombozi. (alama 16)
b). Ukitoa hoja za kuthibitisha jadili mbinu zilizotumiwa na
wazalendo kuhami nchi yao. (alama 17)
4. a). Jadili maudhui yanavyojitokeza katika tamthilia Mzalendo
Kimathi. (alama 17)
b). Taja mafunzo yaliyomo katika tamthilia Mzalendo Kimathi.
(alama 16)
SEHEMU B
Ama
Saidi A.Mohamed: Janga la Werevu
5. a). Jadili mbinu zinazotumiwa na Wananchi kupigania haki zao katika
tamthilia Janga la Werevu. (alama 16)
b). Kwa kuzingatia tamthilia Janga la Werevu, jadili faida ya umoja
katika jamii. (alama 17)
6. a). Uroho wa pesa ndicho chanzo cha migogoro ambayo inatokeya
katika tamthilia ya Janga la Werevu. Jadili. (alama 17)
b). Kulingana na tamthilia ya Janga la Werevu, ni nini chanzo cha
ugonjwa wa Kristy. (alama 16)
Au
Ari Katini Mkachofi: Mama Ee
7. a).“Matatizo yanayokabili harakati za wanawake kujikomboa
yanasababishwa na wao wenyewe.” Jadili ukweli wa kauli hii.
2
3. (alama 18)
b). Jadili namna matatizo hayo yanavyotatuliwa katika jamii yako.
(alama 15)
8. a). “Matatizo ya mwanamke katika ndoa katika tamthilia ya Mama
Ee ndiyo yanayokabili wanawake wengi katika ndoa siku hizi.” Jadili.
(alama 16)
b). Pendekeza hatua zinazoweza kuchuliwa ili kutatua matatizo haya.
(alama 17)
SEHEMU: CH
Ama
Said A.Mohamed: Kivuli kinaishi
9. a). Kwa kutoa mifano mwafaka jadili matatizo yanayokabili
wananchi wa Giningi katika tamthilia Kivuli Kinaishi. (alama 16)
b). Toa mafunzo yanayopatikana katika tamthilia Kivuli Kinaishi.
(alama 17)
10. a) Jadili hadhi ya mwanamke katika tamthilia Kivuli Kinaishi.
(alama 16)
b). Toa mbinu zinazotumiwa na Bi. Kilembwe kuitawala nchi ya
Giningi. (alama 16)
John Ruganda: Mizigo
11 a). Ni mizigo ipi John Ruganda anayozungumzia katika tamthilia ya
Mzigo? Toa angalau mizigo minane. (alama 16)
3
4. b). Fafanua lengo la mwandishi katika kutunga tamthila ya Mizigo.
(alama 16)
12. a) Fafanua jumuyia ya tamthilia ya Mizigo kama inavyojengwa na
mwandish John Ruganda. (alama 16)
b). Mizigo ni kichwa mwafaka cha tamthilia Mizigo.Jadili
(alama 16)
SEHEMU CH:
Ama
Boukheit Amana: Zabibu Chungu
13. “ Ni kweli usemavyo, lakini kuna mila nyingine si za kuungwana. Kama hiyo
ya kuchanguliwa mchumba, mwenzi ambae atakuwa mshauri wako katika
maisha. Sikiza bwana, kuna mila nyingine kuziacha si utumwa kamwe, bali ni
uungwana. Kwa kifupi mila kama hizo ni udhia katika maisha yetu ya sasa,
huwa ni thakili kuzifuata. Dahari hii tuliyonayo ni ngumu,iliyojaa mawimbi ya
majaribu ya kila aina.”
a). Liweke dondoo hili katika muktadha wake. (Alama 6)
b). Ni nani anayesema maneno haya? (Alama 4)
c). Alikuwa akizungumza na nani? (Alama 3)
d). Mhusika huyu anaonyesha sifa gani? (Alama 10)
e). Jadili maudhui yanayojitokeza katika dondoo hili. (Alama 10)
4
5. Au
14. “ Unakumbuka ulipata nishani. Mfanya kazi bora! Mwanamke!
Unakumbuka? Ulijiona wewe ni wewe tu.
Kumbuka!
Unakumbuka uliponunua nyumba hii, bustani hizi, ulijiona umefika. Sasa
aliyekupa vyote hivi amevichua. Vyote!
a). Liweke dondoo hili katika muktadha wake. (Alama 6)
b). Ni nani anayesema maneno haya? (Alama 2)
c). Alikuwa akizungumza na nani? (Alama 2)
d). Kulikuwa kumetokea nini? (Alama 6)
e). Jadili maudhui yanayojitokeza katika dondoo hili. (Alama 8)
f). Ni mbinu gani za kisanaa zinazijitokeza katika dondoo hili? (Alama 9)
MWISHO
5
6. Au
14. “ Unakumbuka ulipata nishani. Mfanya kazi bora! Mwanamke!
Unakumbuka? Ulijiona wewe ni wewe tu.
Kumbuka!
Unakumbuka uliponunua nyumba hii, bustani hizi, ulijiona umefika. Sasa
aliyekupa vyote hivi amevichua. Vyote!
a). Liweke dondoo hili katika muktadha wake. (Alama 6)
b). Ni nani anayesema maneno haya? (Alama 2)
c). Alikuwa akizungumza na nani? (Alama 2)
d). Kulikuwa kumetokea nini? (Alama 6)
e). Jadili maudhui yanayojitokeza katika dondoo hili. (Alama 8)
f). Ni mbinu gani za kisanaa zinazijitokeza katika dondoo hili? (Alama 9)
MWISHO
5