More than Just Lines on a Map: Best Practices for U.S Bike Routes
TOLEO MAALUM MKOA WA TABORA
1. TOWSF ni taasisi isiyo ya kiserikali
inayohudumia wajane na yatima katika
mikoa ya Tabora, Kigoma, Simiyu na
Shinyanga, ikiwa na ofisi zake pia katika
Kijiji cha Usinge, wilayani Kaliua mkoani
Tabora.
Imeanza kazi zake rasmi katika mikoa
hiyo ya Kanda ya Magharibi. Taasisi hii
ina makao yake makuu Mtaa wa Matokeo
Kigogo Luhanga, Dar es Salaam. Imesajiliwa
chini ya kifungu cha 12 (2) cha sheria No.
24 ya mwaka 2002 na kupewa usajili No.
00NGO/00006168. TOWSF imesajiliwa
tangu Februari, 2013.
Malengo ya TOWSF
Mosi, kuhamasisha jamii kutoa misaada ya
kielimu, kijamii na kimaadili kwa watoto
yatima, watoto wa mtaani na wajane. Mbili,
kujenga vituo vya ushauri juu ya mambo
mbalimbali yanayohusu maisha yao ya
kila siku. Na tatu, kuhamasisha wananchi
kushiriki katika shughuli za kijamii ili
kujiletea maendeleo.
Mambo yanayofanywa na taasisi
Mosi, kuhakikisha watoto yatima wote wa
Tanzaniawanasomashulekuanziachekechea
hadi chuo kikuu. Hili linatekelezwa kwa
kufanya yafuatayo 1. Kulipia ada za shule (2)
Kushona sare, (3) Vifaa vya kujifunzia.
Pili, kuhamasisha umma kujua kuwa
malezi kwa watoto yatima ni jukumu lao
kama wanajamii na si sahihi kuwatelekeza.
Tatu, kutoa mafunzo ya ufundi wa nguo
kwa cherehani na ufumaji, na mafunzo ya
ujasiriamali kwa wajane.
Nne, kutoa ushauri kwa makundi
haya ili yaweze kumudu changamoto
zinazowakabili. Ofisi za TOWSF Taasisi hii
imedhamiria kusogeza huduma zake vijijini,
hivyo imepanga kuwa na ofisi katika kila
kanda.
Ofisi Kuu Ofisi ya Kanda ya Magharibi
(Tabora, Shinyanga, Kigoma na Simiyu) .
Ofisi ya Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam,
Pwani na Morogoro). Ofisi ya Kanda ya
Kaskazini (Tanga, Kilimanjaro, Arusha na
Manyara). Ofisi ya Kanda ya Kati (Dodoma
na Singida). Ofisi ya Kanda ya Kusini
(Mtwara, Lindi, na Ruvuma).
Ofisi ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini
(Iringa, Mbeya, Rukwa, na Katavi). Ofisi ya
Kanda ya Ziwa (Mwanza, Mara, Geita na
Kagera).
Ofisi zilizoanza kazi
Ofisi kuu – Mtaa wa Matokeo Kata ya
Mabibo nyumba Na. MTK/408. Ofisi ya
Kanda ya Magharibi – kijijini Usinge Wilaya
ya Kaliua mkoani Tabora. Ofisi hii ipo Kijiji
cha Usinge Wilaya ya Kaliua Mkoa wa
Tabora.
Kazi zilizofanyika tangu kusajiliwa kwa
taasisi hii Februari mpaka sasa.
Kufungua ofisi (mbili) Ofisi Kuu na ofisi
ya Kanda ya Magharibi, Kufanya utambuzi
wa yatima na wajane katika Kata ya Usinge
Wilaya ya Kaliua Mkoa wa Tabora. Kuanza
kuhudumia yatima 200 na wajane 65 kutoka
vijiji vya Usinge, Luganjo, Maboha na Shela.
Kushona sare za shule kwa yatima hao 200
wa shule za msingi.
Mipango endelevu
Ni kuhakikisha taasisi inashirikiana na jamii
za vijijini kuboresha huduma za kijamii
zifuatazo:-
1) Afya itakayookoa vifo vingi vya mama
na mtoto vinavyopelekea kupatikana kwa
yatima wengi. Elimu – Ili kuwasaidia watoto
yatima waweze kuja kujitegemea na kuepuka
kuja kuwa janga la Taifa miaka ya mbele.
Maji- Jamii nyingi za vijijini zinateseka sana
na suala la maji safi ya kunywa.
Taasisi inashirikiana na jamii kuhakikisha
visima virefu vinachimbwa ili kuwaepushia
wananchi wa vijijini na mateso ya kukosa
maji.
Yatima Education Fund
Taasisi hii imezindua mfuko rasmi wa
elimu kwa watoto yatima wa Tanzania
ambao utawawezesha yatima wote kusoma.
Changamoto zilizopo
Uelewa mdogo wa jamii juu ya jukumu
la kuwalea watoto hawa yatima. Fedha za
kuendesha miradi mbalimbali ya taasisi
Ufadhili wa Taasisi.
Ombi kwa jamii
Ieleweke kuwa watoto yatima na wajane ni
watu kama wengine na wanastahili kupata
huduma stahiki. Iunge mkono taasisi
hii kwa hali na mali. Mwenye mchango
wake juu ya makundi hayo anakaribishwa
(TOWSF) misaada yote ya vitu vya kijamii
inapokelewa mfano: Nguo, chakula, sabuni,
mafuta, pesa nk.
Kwa mawasiliano zaidi wasiliana nasi kwa
anuani zifuatazo:- P.O. Box 67620, Dar es
Salaam.
Mob: 0652 – 600700 / 0763 261711.
E-mail: info@towsf.or.tz Website: www.
towsf.
TOWSF: Mkombozi wa yatima
na wajane iliyoanzia Usinge