1. UTANGULIZI
Mwongozo huu umeandaliwa kwa ajili ya wakufunzi ambao wanataka kuendesha mafunzo
shirikishi ya kilimo hifadhi ya mazingira katika ngazi ya vijiji, pia kimeandaliwa kwa namna
ambayo matumizi bora ya ardhi na rasilimali za misitu yatazingatiwa.
Mafunzo haya yatatolewa kwa wakulima wadogo wadogo walioko kwenye eneo la Mradi hasa
wale waliojiunga kwenye vikundi vya shamba darasa na wadau mbalimbali wanaonufaika kwa
namna moja au nyingine na Mradi wa CCAP. Mafunzo haya yataongeza uelewa wa wakulima
kuhusu kilimo hifadhi na yatawawezesha wananchi kutekeleza kwa vitendo zana nzima ya
kilimo hifadhi kwenye mashamba yao.
Shughuli hii inatekelezwa chini ya Mradi wa Mabadiliko ya Tabia nchi, kilimo na
kupunguza umasikini ( CCAP) ambao unatekelezwa kwa ushirikiano wa mashirika matano
ambayo ni MJUMITA, MVIWATA, TFCG, Action Aid na TOAM. Mradi huu una lengo la
kupunguza umasikini miongoni mwa wakulima wadogo wadogo wanaolima mashamba yenye
ukubwa wa hekta 2 Tanzania na kuwajengea uwezo wa kukabiliana na kuhimili mabadiliko ya
tabianchi ikiwa ni pamoja na kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa kwa kuboresha njia za kilimo.
MPANGILIO WA MUONGOZO WA MAFUNZO
Muongozo huu umegawanyika katika sehemu kuu nne, nazo ni:-
1. Utangulizi
2. Mabadiliko ya tabia nchi
Baada ya mafunzo, washiriki watakuwa wameweza kuelezea yafuatayo;-
o Mabadiliko ya tabianchi yanamaanisha nini
o Mabadiliko ya tabianchi yanatokeaje
o Ushahidi wa mabadiliko ya tabia nchi
o Sababu za mabadiliko ya tabia nchia
o Athari zake
3. Kilimo rafiki wa mazingira kwa chakula na kipato
Baada ya mafunzo, washiriki watakuwa na uwezo wa kuelewa:-
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
2. o Maana ya kilimo rafiki wa mazingira
o Umuhimu wa kilimo rafiki wa mazingira
o Kanuni za kilimo rafiki wa mazingira
o Mbinu/hatua za kufuata katika kilimo rafiki wa mazingira
o Faida ya kilimo rafiki wa mazingira
o Changamoto
4. Udongo
Baada ya mafunzo washiriki watakuwa wamefahamu
• Maana ya udongo
• Umuhimu wa viumbe wanaoishi ardhini
• Udongo wenye rutuba ukoje
• Mbinu za kurutubisha udongo
5. Utengenezaji wa mboji
Baada ya mafunzo washiriki watakuwa wamefahamu
• Maana na umuhimu wa mboji
• Vifaa visivyofaa kutumiwa wakati wa kutengeneza mboji
• Vitu vinavyofaa kutumiwa wakati wa kutengeneza mboji
• Namna ya kutengeneza mboji
• Wadudu wenye manufaa na mazingira yafaayo kwa utengenezaji wa mboji
• Muda wa kukomaa na matumizi ya mboji
6. Hifadhi ya maji
Baada ya mafunzo washiriki watakuwa wanaelewa:-
• Umuhimu wa maji
• Namna ya kuhifadhi maji ardhini
• Kuvuna maji
7. Kuundwa kwa Vikundi vya shamba darasa
• Maana na umuhimu wa kikundi
• Kutofautisha kati ya kikundi na mkusanyiko
• Mambo ya kuzingatia wakati wa kuunda kikundi kilicho imara
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
3. • Kazi za kikundi
• Umuhimu wa kuwa na uongozi wa kikundi na sifa za uongozi
• Jinsi ya kuandaa rasimu ya katiba ya kikundi
• Kanuni za katiba bora
• Zana ya mtandao
• Namna ya kuwaunganisha wanakikundi na mitandao ya MJUMITA na MVIWATA
MADA 1: MABADILIKO YA TABIANCHI
1.1 Mabadiliko ya tabia nchi yanamaanisha nini?
Tabia nchi kwa kawaida hufafanuliwa kama wastani wa hali ya hewa, hivyo tabia nchi na
hali ya hewa huingiliana japo ni vitu tofauti. Mabadiliko ya tabia nchi ni mabadiliko ya muda
mrefu ambayo yametokea katika maeneo mbalimbali ya dunia. Mabadiliko haya huweza
kupimwa kwa kuzingatia hali ya hewa kama vile kiwango cha joto na baridi, mvua na ukame.
1.2 Mabadiliko ya Tabia nchi yanatokeaje?
Mabadiliko ya tabia nchi hutokea wakati ambapo hali ya hewa katika eneo fulani hubadilika
katika kipindi cha muda fulani (mfano baada ya miaka 10). Mabadiliko hayo hutokea wakati
miale ya jua inapokuja moja kwa moja duniani.
Mabadiliko ya tabia nchi ni tishio kwa maendeleo kwa sababu huathiri afya zetu, makazi,
miundo mbinu, kilimo na mfumo wa ekolojia. Pamoja na hayo, mabadiliko ya tabia nchi
husababisha kutetereka kwa hali ya maisha katika maeneo mbalimbali ya dunia.
1.3 Ushahidi wa mabadiliko ya tabia nchi.
Ushahidi wa mabadiliko ya tabia nchi ni kuwepo kwa mafuriko na ukame katika maeneo
mbalimbali nchini na dunia nzima. Kwa upande wa Tanzania tumeshuhudia mafuriko hayo
wilayani Kilosa na ukame Mkoani Manyara.
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
4. 1.3.1 Milipuko ya magonjwa
Ugonjwa kama malaria umejitokeza katika maeneo ambayo hapo awali haukuwepo. Katika
mkoa wa Njombe ambao uko nyanda za juu kwenye baridi, ugonjwa wa malaria haukua tatizo
katika wilaya za Njombe na Mafinga. Kutokana na mabadiliko ya tabia nchi, joto limeongezeka
na kusababisha kuwepo na makazi ya mbu wanaosababisha malaria katika maeneo hayo.
1.3.2 Ukame
Kutokana na ukame unaosababishwa na mvua zisizokuwa na mpangilio, imepelekea kupungua
kwa mavuno. Mvua zisizoaminika ni mojawapo ya madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabia
nchi. Haya yote yamepelekea watu wengi duniani kukosa chakula na hatimaye wengine kufariki
kwa sababu ya njaa.
Kuyeyuka kwa barafu katika vilele vya milima (mfano Mlima
Kilimanjaro)
Kuyeyuka kwa barafu katika vilele vya milima ni kutokana na kuongezeka kwa kiwango cha
joto. Kiwango cha joto kinaongezeka kutokana na kuharibika kwa tabaka la ozone lililopo angani
ambalo kazi yake ni kupunguza miale ya jua inayokuja duniani. 80% yatheluji ya mlima
Kilimanjaro , ambao ni mlima mrefu zaidi katika bara la afrika imetoweka kwa kipindi cha tokea
mwaka 1912.
1.3.3 Kuongezeka kwa kina cha bahari
Kuongezeka kwa kina cha bahari ni ushahidi wa kuwepo kwa
mabadiliko ya tabia nchi. Hivi leo kuna pwani au fukwe za bahari
ambazo zimeanza kutoweka kutokana na kuongezeka kwa kina cha
bahari. Haya yote ni matokeo ya mabadiliko ya tabia nchi.
1.4 SABABU ZA MABADILIKO YA TABIA NCHI
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
5. Mabadiliko ya tabia nchi yamesababishwa na vitu ama vitendo mbalimbali ambavyo
vimechangia kwa sehemu kubwa uharibifu wa mazingira. Vitendo vilivyochangia uharibufu wa
mazingira na kusababisha mabadiliko ya tabia nchi ni pamoja na:-
1.4.1 Kilimo cha Kuhamahama
Mabadiliko ya tabia nchi kwa namna moja au nyingine yanasababishwa na kilimo cha kuhama
hama. Wakulima wadogo wadogo walio wengi Tanzania wanalima kilimo cha kuhama hama
ambapo shughuli hiyo hupelekea kufyekwa kwa misitu mingi katika maeneo ambayo mashamba
mapya hufunguliwa. Katika shughuli hii, miti na uoto wote uliopo juu ya uso wa ardhi
unaosaidia kufyonza hewa ukaa huaribiwa. Hewa hii hukusanyika angani na kuharibu tabaka la
ozone na kusababisha ongezeko la joto duniani na hivyo kutokea mabadiliko ya tabia nchi
1.4.2 Uchomaji moto wa mabaki ya mazao shambani
Shughuli za uchomaji moto mabaki ya mazao shambani huambatana na moshi unaokusanyika
angani na kuchangia kuharibika kwa tabaka la ozoni na kusababisha mabadiliko ya tabia nchi.
1.4.3 Moshi kutoka viwandani na kwenye magari
Leo hii kuna idadi kubwa sana ya viwanda na magari duniani kote ukilinganisha na miaka ya
nyuma. Moshi kutoka viwandani na kwenye magari unachangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la
mabadiliko ya tabia nchi. Moshi huu huharibu tabaka la ozone angani ambalo kazi yake ni
kupunguza ukali wa miale ya jua ifikayo duniani na hivyo husababisha ongezeko la joto duniani.
1.4.4 Uchomaji mkaa usio endelevu
Uchomaji mkaa ni mojawapo ya shughuli zinazofanywa na mwanadamu ambazo zinachangia
kwa kiasi kikubwa katika mabadiliko ya tabia nchi. Uchomaji wa mkaa huambatana na ukataji
wa miti na uchomaji wa magogo. Shughuli hii huharibu tabaka la ozone na hivyo kuongezeka
kwa kiwango cha joto duniani.
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
6. Mchoro 1: Uandaaji wa tanuru Mchoro 2: Utengenezaji wa mkaa
kwa ajili ya mkaa husababisha hewa ya ukaa
1.4.5 Ukataji miti hovyo
Mchoro 3: Ukataji wa miti kwa matumizi ya kuni Mchoro 4: Ukataji wa miti kwa ajili
ya kujengea
Kwa kawaida miti hufyonza hewa ukaa. Kwa maana hiyo, miti ikikatwa hovyo hewa ukaa
haitafyonzwa tena badala yake itaenda kuharibu tabaka la ozone lililoko angani ambalo kazi
yake ni kupunguza ukali wa miale ya jua. Baada ya uharibifu huo kiwango cha joto duniani
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
7. huongezeka kwa kiasi kikubwa na hivyo kusababisha madhara mengi kama vile ukame na
ukosefu wa mvua.
1.4.6 Uchomaji wa misitu
Uchomaji wa misitu unaosababishwa na shughuli mbalimbali kama vile urinaji wa asali,
uwindaji wa wanyama na uchomaji misitu kwa imani potofu, huchangia kuongezeka kwa hewa
ukaa angani ambayo huadhiri tabaka la ozoni na kusababisha ongezeko la joto duniani. Mfano:
Katika maeneo mengi Tanzania watu wanaamini kwamba wakichoma moto na kusafiri umbali
mrefu aliyechoma moto ataishi muda mrefu.
1.4.7 Uchimbaji wa madini.
Uchimbaji wa madini ni shughuli inayoambata na kubadili maeneo ya misitu kuwa katika
matumizi mengine. Katika shughuli hii, miti na uoto wote uliopo juu ya uso wa ardhi unaosaidia
kufyonza hewa ukaa huaribiwa. Hewa hii hukusanyika angani na kuharibu tabaka la ozone na
kusababisha ongezeko la joto duniani na hivyo kutokea mabadiliko ya tabia nchi.
1.4.8 Ufugaji wa mifugo
Mifugo mingi ikifugwa katika eneo dogo la malisho huharibu uoto wa asili ikiwa ni pamoja na
nyasi, vichaka na miti michanga ambayo ingesaidia kunyonya hewa ukaa
MADA 2: KILIMO RAFIKI WA MAZINGIRA KWA CHAKULA NA KIPATO
2.1 Maana ya Kilimo rafiki na mazingira/kilimo endelevu.
• Mfumo huu ni ule unaotumia mbinu mbalimbali zinazoendelea kulinda afya ya
udongo, maslahi ya kimazingira, wanyama na binadamu.
• Kilimo hai na hifadhi ya mazingira kinatuwezesha kuzalisha chakula salama bila
kuathiri matumizi ya ardhi kwa vizazi vilivyopo na vijavyo .
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
8. • Kilimo hiki kinahimiza uzalishaji wa mazao kwa kutumia samadi na mboji na
udhibiti wa wadudu na magonjwa kwa kutumia njia za asili.
• Kilimo hiki hakitumiii madawa na mbolea toka viwandani au hutumika kwa
kiwango kidogo sana pale inapohitajika na kinapinga matumizi ya viwatilifu
vyenye sumu na mbegu zenye vinasaba na shughuli zozote zinazopelekea
uharibifu wa udongo , maji na maliasili zinginezo.
Inadaiwa kuwa Kilimo hai na hifadhi ya mazingira ni jibu la matatizo yanayoathiri
mazingira kutokana na uendelevu kiuchumi, rafiki katika matumizi ya malighafi na
hifadhi ya mazingira na rasilimali, chenye kukubalika katika jamii, na kumudu ushindani
wa kibiashara. Mafunzo haya yatajikita zaidi katika kuelezea mfumo wa kilimo hai na
hifadhi ya mazingira kama njia itakayowawezesha wananchi kukabiliana na mabadiliko
ya tabianchi.
2.2 Umuhimu wa Kilimo hai na hifadhi ya mazingira
• Ni kilimo kinachozingatia njia zote za kilimo bora. Mfano kilimo cha makinga maji,
mazao funika, mseto, mzunguko na kutifua eneo la kupanda tu.
• Ni mfumo unaohusisha matumizi ya udongo na mazao kwa utaratibu ambao hupunguza
mmomonyoko wa udongo mashambani.
• Ni mfumo wa ukulima unaowezesha wakulima kupata matokeo bora kutoka kwenye
rasilimali yoyote wanayoweza kupata.
• Kanuni za kilimo hifadhi zinawalenga wakulima wote (mkono, plau au trekta).
• Kilimo hifadhi hakihusiani na aina gani ya mazao yanafaa kwa viwango tofauti vya mvua
au udongo, mbolea kiasi gani itumike kwa mazao haya n.k.
2.3 Kanuni na misingi ya kilimo rafiki wa mazingira
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
9. Kilimo rafiki wa mazingira ni kilimo kinachozingatia mchanganyiko wa kanuni na misingi
mbalimbali ya mbinu za kilimo bora. Mfumo huu huzingatia mzunguko wa virutubisho vya
mimea kwa kufuata kanuni kuu nne ambazo ni:
1. Jiandae mapema baada ya kuvuna
2. Kutifua udongo kwa kiwango kidogo au kutotifua kabisa
3. Kufunika udongo muda wote kutochoma/masalia ya mazao baada ya mavuno
4. Kilimo cha mzunguko au mbadilishano wa mazao na ya jamii ya mikunde/mazao
5. Kilimo mchanganyiko na miti/wanyama
2.3.1 Kutifua udongo kwa kiwango kidogo au kutotifua kabisa
Kutifua ardhi ni pamoja na kufungua, kugeuza, na kuchanganya udongokwa kutumia
jembe, plau, na vifaa vinavyokokotwa na maksai au trakta. Tunapolima kwa kutifua
ardhi mara nyingi tunasababisha ardhi kutoa hewa ukaa ambayo mara nyingi huhifadhiwa
ardhini, vilevile muundo wa udongo ambao hurahisha maji kuingia kwa urahisi kwenye
udongo huharibika na hivyo kusababisha mmomonyoko wa udongo.
Kulima kwa uangalifu kwa kutifua udongo kwa kiwango kidogo au kutotifua kabisa kunaongeza
uwezo wa ardhi kuhifadhi maji,kuingiza hewa, kurahisisha kutiririka maji, kupata joto na
kuhifadhi hewa ukaa ndani ya udongo.
Hii hufanyika kwa kupanda moja kwa moja kwenye udongo bila kutifua au kuchimba mashimo
(beseni) ya kupandia bila kulima. Kilimo hiki kisichohitaji kutifua ardhi namavuno yake ni
mazuri kabisa.
Faida za kutifua udongo kwa kiwango kidogo au kutotifua kabisa
1. Kulainisha na kulegeza udongo ili mizizi ya mimea ipenyeze kwa urahisi
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
10. 2. Kuingiza hewa, naitrojeni na oksijeni kutoka angani
3. Kuchangamsha viumbe hai ardhini vifanye kazi
4. Kuongeza uwezo wa maji wa kupenyeza ardhini
5. Kuongeza uwezo wa maji wa kupenyeza ardhini
6. Kupunguza unyaufu wa ardhi
7. Kudhibiti wadudu ardhini na magugu
8. Kusaidia kuchanganya masalia ya mazao pamoja na mbolea ardhini
9. Kutayarisha shamba kwa kuotesha na kusia mbegu
10. Kurekebisha ugumu unaosababishwa na shughuli mbalimbali juu ya ardhi
Mfano wa mfumo wa kilimo cha kutokutifua au kutifua ardhi kidogo tu ( Kilimo
Hifadhi);Zambia, Chololo kondoa.
Ukanda wa Pwani wakulima hufanya yafuatayo;
• Wanakata uoto katika usawa wa ardhi
• Kufuata kontua, umbali wa kuotesha mazao udongo unatifuliwa
• Samadi inawekwa katika mistari iliyolimwa
• Mazao yanaoteshwa katika mistari hiyo
• Magugu katikati ya mistari yanakatwa mara kwa mara na ni matandazo
• Mfumo unaweza kutumia mikunde kama zao la kufunika ardhi, kadhalika jimbo hilo
mahindi yanaoteshwa kwenye shamba lenye masalia ya msimu uliotangulia.
• Mahindi yanaoteshwa ndani ya matandazo
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
11. • Mwezi 1 hadi 2 baadaye maharage yanaoteshwa
• Mahindi yakishavunwa masalia hutandazwa shambani na maharage huendelea kukua.
• Maharage hayo huandaa shamba tayari kwa kuotesha zao jingine la mahindi
• Kwa kutumia mtindo huu mahindi na maharage huvunwa mara mbili kila mwaka na kutoa
mavuno mazuri.
2.3.2 Kufunika ardhi muda wote
Ili Kuukinga udongo kutokana na jua kali na mvua kubwa unatakiwa kuufunika udongo kwa
kutumia matandazo, kuacha masalia ya mazao au kupanda mazao ya kufunika shambani. Kwa
njia nyingine tunazuia mmomonyoko wa udongo na kuhifadhi unyevu.
2.3.2.1 Matandazo
Kuweka matandazo ni kazi ya kufunika udongo wa juu kwa kutumia magugu, masalia ya mazao
ya kilimo na misitu, majani, matawi, vijiti, na mabua.Matandazo na wakati wa kutandaza
hutegemea mazingira na mbinu za kilimo. Matandazo huongeza kasi ya kazi za viumbe hai ndani
ya ardhi, huboresha udongo ili maji yaweze kunywea ndani, na hupunguza mmomonyoko.
Matandazo yanapooza tunapata mboji inayoshikiza sehemu za udongo vizuri ili zisichukuliwe na
maji. Matandazo hutoa chakula cha wadudu rafiki waishio udongoni.
2.3.2.2 Faida za Matandazo
• Kuukinga udongo na mmomonyoko wa upepo na maji.
• Kuboresha uwezo wa maji kupenyeza ndani ya udongo, ili kudumisha unyevu na kuzuia
unyaufu
• Kulisha na kulinda viumbe hai ndani ya ardhi
• Kuzuia magugu
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
12. • Udongo haupati joto kali
• Matandazo ni chanzo cha virutubisho vya mazao
• Kuongeza mboji ardhini
Zingatia:
• Kila inapowezekana ni vyema kusambaza matandazo shambani kabla au mara tu msimu wa
mvua unapoanza. Hicho ni kipindi ambapo ardhi huweza kuathirikasana. Inafaa kuwekea
matandazo miche ya mboga ikishapata nguvu na kujishikiza vizuri na udongo.
• Kadhalika matandazo yawekwe kwa kiasi kidogo tu hasa pale ambapo mazao hayajaota.
Kwenye shamba la mazao ya kudumu, matandazo yawekwe mara baada tu ya kutifua ardhi.
Matandazo huweza kutandazwa katikati ya mazao, kuzungushia mazao ya miti au kwenye
shamba lote.
• Endapo matandazo yanachelewa kuoza, kinyesi cha kuku kinatandazwa juu yake
2.3.2.3 Kuacha masalia ya mazao
Njia nyingine ya kufunika udongo ni kutumia masalia ya mazao, hii hufanyika pindi mkulima
anapomaliza kuvuna mazao ya msimu uliopita.Masalia ya mazao kama mahindi, maharage,
mtama, alizeti yakatwe na kulazwa juu ya udongo ili kuzuia Matone ya mvua na jua kupiga
ardhini moja kwa moja.
2.3.3 Mzunguko wa mazao
• Upandaji wa mazao yanayochangamana vizuri kwenye shamba moja na kufanya mzunguko
wa mazao msimu hadi msimu. Kuna sababu nyingi za msingi za kufanya kilimo cha
kubadilisha mazao na yale aina ya mikunde kama vile soya, maharagwe, kunde, choroko,
mbaazi na mengineyo.
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
13. • Kilimo hiki cha kubadilisha mazao na ya jamii ya kunde hupunguza matumizi ya mbolea za
viwandani mashambani (na hivyo kuokoa matumizi zaidi ya pesa pia!).
• Mazao aina ya mikunde hurutubisha udongo kwa kutumia hewa ya naitrojeni kutoka angani
na kuibadilisha na hivyo kufanya mimea mingine isiyo jamii ya kunde ifaidike vile vile.
• Mbaazi hutumia mizizi yake mirefu kuingia chini kabisa ya ardhi na kuchimbua virutubisho
aina ya fosforasi, huvileta virutubisho hivyo juu ya ardhi na kufanya mimea yenye mizizi
yenye kina kifupi itakayopandwa kwenye mbadilishano msimu unaofuata kunufaika nayo.
• Mazao aina ya kunde yanayokomaa mapema ni chanzo kizuri cha protini kwa familia kwa
mwezi Februari, wakati ambao unahitaji zaidi kwa uhakika wa chakula kwenye familia.
• Inawezekana kuvuna mara mbili kwa mazao yanayokomaa mapema katika msimu mmoja.
Mazao jamii ya mikunde yanapaswa kupandwa angalau theluthi moja ya ukubwa wa shamba
unalolima katika utaratibu wa kubadilishana mazao kila mwaka.
• Mimea ya mbolea za kijani inaoteshwa mara baada ya kuvuna zao kuu.
• Ni vyema kuotesha kwa kukinga mitelemko mikali kupunguza kasi ya maji ya mvua
inayotelemka milimani. Kwa yale mazao yasiyofunika ardhi mapema inafaa kuotesha zao
kama alfalfa au maharage yatakayofunika ardhi mapema.
• Faida yake ni kwamba kilimo hiki hupunguza madhara ya wadudu na magonjwa.
2.3.4 Kilimo cha kuchanganya mazao na miti
• Miti kama vile Mkondachao (Faidherbia albida) yaweza kuchukua hewa ya naitrojeni
iliyoko angani na kuibadilisha kuwa rutuba ifikapo ardhini na kuifanya mimea mingine
kunufaika nayo.
• Unaweza kupanda miti iongezayo rutuba na mboji kwenye udongo ili kuongeza
uzalishaji wa mazao. Miti kama mkondachao yaweza kupandwa nafasi ya mita10 kwa10
na unaweza kupata miti 40 kwa ekari.
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
14. • Miti ya mkondachao inayo sifa moja ya pekee; hupukutisha majani yake kipindi cha
mvua badala ya kipindi cha kiangazi kama inavyofanya miti mingine. Hivyo basi hali
hiyo inakuwezesha kupanda mazao mbalimbali chini ya mwamvuli wa miti hiyo pasipo
kuathiri ufanisi wa mazao hayo kwa vile hapawi na kivuli.
2.4 Hatua za kufuata katika kilimo hifadhi
2.4.1 Acha masalia ya mazao shambani- usiyachome
Palizi la magugu la mara kwa mara ni muhimu sana katika Kilimo Hifadhi. Jinsi unavyoacha
masalia mengi shambani ni vizuri zaidi. Masalia unapoyaacha shambani hurutubisha udongo,
yanadhibiti upotevu wa maji ya mvua na yanaruhusu maji kunywea ndani ya udongo. Unapoacha
masalia shambani kila mwaka, yanaboresha udongo. Mchwa wanayashambulia na
kuyachanganya na matamahuluku kwenye udongo. Masalia yanavyokua mengi ndivyo mchwa
wanavyoyashambulia na hatimaye hawawezi kushambulia mazao yako shambani.
2.4.2 Andaa mashimo ya kupandia ya kudumu
Wakati unapochimba mashimo ya kupandia badala ya kuutibua udongo husaidia kupunguza
matumizi ya fedha na muda. Mashimo ya kupandia ya kudumu yanavuna maji ya mvua za awali
na hivyo kurahisisha uotaji wa mbegu na kuboresha uchipuaji mzuri wa mazao yako shambani.
2.4.3 Panda mbegu mapema
• Anza matayarisho ya shamba mapema mara tu baada ya kumaliza kuvuna, ili uweze
kusambaza uzito wa kazi zako kwa miezi mingine kabla ya kuanza kwa msimu mwingine
wa kupanda.
• Jinsi unavyowahi kuandaa shamba lako mapema,ndivyo unavyoweza kuwahi kupanda
mara tu baada ya mvua za kwanza za kupandia kunyesha.
• Upandaji mbegu wa mapema ni muhimu kwa sababu mvua hizo za awali husaidia mmea
katika uotaji wake/upevukaji wake kutokana na naitrojeni inayoachwa na viumbe hai wa
udongoni.
2.4.4 Wahi kupalilia mara kwa mara msimu wote
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
15. • Palizi la mapema na la mara kwa mara katika mwaka mzima ni jambo muhimu sana
katika Kilimo Hifadhi.
• Uotaji wa magugu shambani utakuwa unapungua baada ya muda fulani kutokana na
palizi la mara kwa mara.
• Palizi ni sharti lifanyike ndani ya wiki kati ya nne na sita baada ya mbegu kuota
shambani wakati magugu yatakuwa yamefikia kimo cha sentimeta 2.5.
• Ni muhimu uendelee kufanya palizi hata wakati mazao yanapokuwa yamekomaa hata
baada ya mavuno, ili kuyadhibiti kabisa magugu yasizalishe mbegu na kuzipukutisha
shambani, vinginevyo yatakuongezea kazi ya ziada ya palizi kwa mwaka ufuatao.
2.5 Faida ya kilimo hai na hifadhi ya mazingira
2.5.1 Huhifadhi udongo na kudumisha rutuba ya ardhi
2.5.2 Hupunguza uchafuzi wa maji kwenye mito, maziwa na chini ya ardhi.
2.5.3 Hulinda bioanuai.
2.5.4 Hudumisha aina mbalimbali za uoto wa asili.
2.5.5 Hutunza vizuri mifugo.
2.5.6 Matumizi ya malighafi mbadala, na nishati asilia.
2.5.7 Hakuna masalia mengi ya viuatilifu kwenye vyakula.
2.5.8 Hakuna vichochezi na madawa katika mazao ya mifugo.
2.5.9 Mazao ya thamani bora zaidi; (mwonjo na hifadhi).
2.6 Changamoto za kilimo hifadhi na mazingira
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
16. 1. Woga wa wakulima kuhusu kushukuka kwa mavuno kunakosababishwa na mabadiliko
ya mavuno
2. Upatikanaji wa aina za mbegu zinazofaa
3. Gharama za mbegu
4. Upatikanaji wa maji
5. Mahitaji ya nguvu kazi
6. Matumizi ya ziada kutokana na mazao mengine ya pembeni
7. Uhakika wa chakula
MADA 3: UDONGO
3.1 Udongo ni nini?
Udongo ni tabaka la juu ya ardhi linalosaidia ukuaji wa mimea. Udongo ni mchanganyiko wa
miamba iliyopasuka, madini, maji, hewa, wadudu na wanyama wadogo na wakubwa walio hai
na waliokufa, masalia ya mimea na mboji.
Kuna aina kuu tatu za udongo katika maeneo yetu ambazo ni kichanga, mfinyazi na tifutifu.
Ustawi wa zao fulani hutegemeana na aina ya udongo ulioko katika eneo hilo. Udongo wa aina
ya tifutifu ndio unaofaa zaidi kwa ajili ya kilimo. Udongo wa kichanga hupoteza maji kirahisi na
hivyo haufai kwa kilimo. Hata hivyo udongo wa mfinyanzi hutuwamisha maji na kusababisha
mizizi kushindwa kupumua na kusababisha mimea isiyotaka maji mengi kama mahindi na
maharage kufa.
• Udongo ni hitaji muhimu kuliko mengine katika kilimo na mkulima anayo mamlaka
makubwa juu yake. Udongo una uhai kwa sababu ni makazi ya mimea, wanyama na
viumbe vingine vyenye mahusiano nao. Udongo una yabisi, mboji na nafasi wazi.
• Udongo wenye ujazo wa kijiko cha chai huweza kuwa na mamilioni ya viumbe. Baadhi
hutokana na mimea na wanyama. Viumbe vingine huonekana kwa macho kama minyoo,
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
17. buibui, konokono, jongoo na mchwa. Viumbe muhimu sana ardhini ni bakteria, fangi na
protozoa.
• Wakulima wengi wanadhani kuwa viumbe wanaoishi ndani ya ardhi husababisha
madhara na kufikiria tu namna ya kuwaua. Ukweli ni kwamba ni wadudu wachache sana
wanaodhuru mazao. Viumbe wengi ndani ya udongo ni wa manufaa makubwa na
hurutubisha udongo.
3.1 Umuhimu wa viumbe wanaoishi ardhini:-
• Kuozesha mabaki na kutengeneza mboji.
• Kuchanganya masalia ya mazao ndani ya sehemu za ardhi na kuimarisha udongo.
• Kuchimba vinjia na hivyo kurahisisha mizizi kupenya na kuingiza hewa ardhini.
• Kusaidia upatikanaji wa virutubisho ardhini.
• Kuzuia wadudu na magonjwa yanayoathiri mizizi ya mimea.
• Minyoo ni alama ya udongo wenye rutuba, wana kazi nyeti ardhini mfano kuyeyusha
masalia ya viumbe hai, kusaidia kuchanganya masalia na sehemu za udongo ili
kuuimarisha
• Njia wanazozichimba ndani ya ardhi, zinarahisisha kupenyeza hewa na maji, hivyo
kupunguza mmomonyoko wa udongo na maji kusimama juu ya ardhi.
• Minyoo wanahitaji masalia hai, joto la kiasi na unyevu wa kutosha. Husitawi vizuri
ndani ya udongo wenye matandazo. Kilimo cha mara kwa mara na matumizi ya
viuatilifu huathiri sana idadi ya minyoo ardhini.
3.2 Udongo wenye rutuba unategemea kuwa na vitu vifuatavyo;
• Kina cha udongo: Kuwepo kwa ujazo/kina cha udongo wa kutosha unaotumiwa na
mizizi ya mimea.
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
18. • Upatikanaji maji: uwepo wa unyevu wa kutosha kwa kipindi kirefu.
• Urahisi wa maji kupita: Uwezo wa kupitisha maji kwa urahisi.
• Hewa: Hewa ya kutosha inahitajika kuwepo kwa afya ya mizizi na maisha hai ya udongo.
• pH Uchachu: Udongo hauna tindikali au chumvi nyingi.
• Madini: upatikanaji wa virutubisho kutoka mwamba asilia, na muundo wa udongo.
• Mboji: Kuwepo kwa kiasi cha kutosha cha mboji inahusiana vizuri na uwezo wa udongo
kushika virutubisho, maji na maisha ya udongo na muundo wa udongo.
• Viumbe hai kwenye udongo:Kuwepo kwa viumbe hai kwenye udongo husaidia upatikanaji
wa virutubisho, kushikilia maji, muundo na afya ya udongo, na kuyeyushwa kwa mboji ardhini.
Endapo udongo utakosa baadhi ya vitu vilivyotajwa hapo juu hali ya udongo haitafaa kwa
ukuaji wa mimea. Mifano ni kutuama maji, uchachu, udongo mgumu na uhaba wa virutubisho,
unaosababisha upungufu mkubwa wa mavuno.
3.3 Mbinu za Kurutubisha udongo
Wakulima wanaweza kuboresha rutuba ya udongo kwa kuzingatia njia zifuatazo:
1. Kuukinga udongo kutokana na jua kali na mvua kubwa kwa kuufunika na matandazo,
mbolea ya kijani au mazao ya kufunika. Kwa njia nyingine tunazuia mmomonyoko wa
udongo na kuhifadhi unyevu.
2. Kilimo mseto na mzunguko wa kufaa wa mazao ya msimu unadumisha rutuba ya
udongo.
3. Tifua udongo ipasavyo ili kudumisha rutuba na ubora wake kwa kuzuia mmomonyoko
na udongo kugandamana.
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
19. 4. Kuwa na mpangilio mzuri wa virutubisho kwa kutumia mbolea za asili kulingana na
mahitaji ya mazao kama samadi na mboji
5. Kuainisha malisho na hifadhi ya viumbe hai walio ardhini, kwa kuongeza masalia ya
mimea tunawezesha viumbe hai wenye faida kuishi na kufanya kazi.
MADA 4: KUTENGENEZA MBOJI
4.0 Mboji ni nini?
Mboji ni sehemu ya viumbe (mabaki ya mimea na wanyama (matamahuruku)) ambayo
imeozeshwa kwa muda mrefu ili kusazwa na viumbe vidogo vidogo. Sehemu za vitu kama
majani, matunda na mabaki ya mboga hutengeneza mbolea ya mboji. Mboji iliyoiva hubadilika
rangi na kuwa ya hudhurungi, tifutifu na hunukia vizuri. Mboji ni rahisi kutengeneza, gharama
zake ni za chini sana na inafaa mno kuongezwa kwenye udongo ili kuinua mazao ya shamba.
Mboji iliyotunzwa vyema huwa na rutuba nzuri kwa mimea inapotumiwa shambani. Mboji
huchemka hata kiasi cha kuua magonjwa ya mimea na mbegu za magugu.
Majani makavu ya ndizi ni mazuri kwa kutunza vifaa vya mbolea na kuweka ukavu. Hali hii
huwa huzuia kupotea kwa maji kabla ya kujenga lundo la mboji na wakati mbolea inapokuwa
inaiva.
4.1 Vifaa visivyofaa kuwekwa kwenye mboji
• Sehemu za mimea ambazo zimenyunyiziwa dawa ya kuwaua wadudu (viuatilifu) na
magugu.
• Vipande vya nyama kwa sababu vinavutia panya na wadudu wengine.
• Vifaa vilivyo na ncha kali kama mwiba ambavyo vyaweza kujeruhi mikono na miguu.
• Magugu ambayo yanarudiarudia kila mwaka. Magugu kama hayo huuliwa kwa kuanikwa
kwenye jua kali ili yakauke baadaye huchomwa ili yasienee na jivu lake laweza
kuongezwa kwenye lundo la mbolea.
• Vitu visivyo kua na uhai kama plastiki na chuma.
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
20. 5.2 Vitu ambavyo vyaweza kutumiwa kutengeneza mboji
5.2.1 Vifaa vya nyumbani
• Maganda ya matunda
• Jivu la kuni
• Taka taka za kufagia
5.2.2 Shambani
• Mabaki ya mimea baada ya kuvuna, katakat vitu vigumu, kama ni vigumu
nyunyizia maji. Vitu vigumu huoza pole pole. Usitumie vile vilivyowekwa
dawa juzijuzi
• Majani makavu/ yaliokauka
• Mimea/majani ya kijani au mabichi, kata kata kama ni makubwa. Mimea
jamii ya mikunde hupendekezwa
• Magugu, katakata kama ni makubwa. Usitumie mizizi ya magugu ama
mbegu za magugu
5.2.3 Asili
• Samadi kutoka kwa mifugo na mabaki ya mimea ni nzuri sana katika
kutengeneza mbolea hai na ina rutuba nzuri sana
• Mkojo, ni vigumu kukusanya mkojo ila hupatikana kwenye zizi la
ng’ombe. Nyunyuzia kwenye biwi/lundo la mbolea kwa kiwango
kidogo. Mkojo hufanya mbolea kuoza haraka
• Udongo, tumia udongo kama sentimita 10 kutoka tabaka la juu ya
shamba. Hutumika kufunika Biwi/lundo la mbolea.
• Magugu ya baharini (Mwani) Yafaa yakaushwe na hutumiwa na
majani yaliyo kauka yana madini muhimu kwa wingi
4.3 Namna ya kutengeneza mboji ya mimea
Kusanya vitu na vifaa vinavyohitajika katika utengenezaji wa mboji ambayo ni;
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
21. • Majani mengi mabichi/kijani na makavu. Majani jamii ya mikunde ni mazuri sana kwani
hutengeneza kirutubishi cha naitrojeni (N) kwa wingi.
• Mabua ya mahindi au vitawi vya miti
• Udongo wa kawaida wa juu
• Mboji ya zamani
• Majivu au vumbi la mkaa
• Maji
4.3.1 Hatua za kufuata
1. Chagua sehemu karibu na eneo ambalo mboji itaenda kutumika na ambapo kuna
hifadhi ya kutosha kukinga dhidi ya upepo, jua na mvua.
2. Katakata majani yawe madogo madogo ili yaweze kuoza haraka.
3. Tengeneza msingi kama mita sita (6) urefu na upana wake mita 2 kwa kutumia majani
magumu kama matawi/vijiti. Hii itahakikisha maji yanatiririka na hewa ina zunguka
vizuri. Hakikisha kuna nafasi ya kutosha kufanyia kazi kwenye biwi bila kulikanyaga.
4. Weka sentimita 10 ya majani ambayo hayaozi haraka kwa mfano mabua vya mahindi
au mimea mibichi/kijani.
5. Weka sentimita 10 ya vifaa ambavyo huoza haraka kwa mfano maganda ya mboga na
matunda.
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
22. 6. Weka sentimita 2 ya samadi (mbolea-hai ya wanyama), mabaki ya mbolea ya zamani
kama yaweza kupatikana.
7. Weka udongo wa juu sentimita 10 kutoka kwenye shamba ambalo hulimwa.
8. Majivu na mkojo vyaweza kunyunyuziwa juu ili kufanya biwi/lundo kuoza haraka.
9. Nyunyizia maji kwenye biwi mpaka lilowe.
10. Rudia mpangilio huu kuanzia namba nne (4) mpaka lundo lifike mita moja (1.m) hadi
moja na nusu (1.5m) kwenda juu isipokuwa vijiti/matawi ya kwanza.
4.3.2 Zingatia
• Biwi/lundo cha mboji kinatakiwa kifunukwe ili kupunguza/kuzuia mvuke ama mvua
nyingi ambayo hubeba rutuba kutoka kwenye mbolea. Weka gunia, nyasi ama matawi ya
migomba yaliyokauka.
• Kila tabaka/kunjo/safu yafaa kupangwa kuanzia kwenye ukingo ili lundo la mbolea
lisiporomoke.
• Namna nyigine ya kuzuia lundo kuporomoka ni kwa kuweka vipande vya mbao kando ya
biwi. Wavu wa nyuzi za chuma utafanya biwi kukauka.
• Katika sehemu zenye ukavu mwingi. Mianzi iliyo na mashimo husaidia kufanya hewa
kuingia na kuzunguka kwa urahisi
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
23. 4.4 Wadudu wenye manufaa na mazingira yanayohitajika kwenye Biwi
4.4.1 Wadudu ambao husaidia kufanya biwi kuoza
Viumbe wengi wanaohusika na kazi hii ya kuoza ni wadogo hawaonekani kwa macho matupu.
Ila viumbe hawa huhitaji maji, hewa na vipande/sehemu ya viumbe wengine ambazo kwao ni
chakula. Viumbe hawa hula vipande hivyo na hutoa hewa ya carbon dioxide, maji na joto.
4.4.2 Hatua 3 kubwa za biwi kuoza
Kuna hatua tatu kubwa wakati biwi linapooza;
1. Hatua ya kupanda joto
2. Hatua ya kupoa/kuwa baridi
3. Hatua ya kukomaa.
4.4.2.1 Hatua ya kupanda joto
Wakati ya hatua ya kupanda joto, joto hufikia kiwango cha juu sana katikati mwa biwi. Uzuri
wa joto hili ni kwamba magonjwa yaliyokuwa kwenye viungo vya biwi na mbegu za magugu
huchomwa hadi kufa. Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai
uyoga (fungi) huwa na faida nyingi kwa sababu kazi yake ni kuzisaga nyuzi ngumu ambazo
zimo kwenye viungo vya mimea au majani.
4.4.2.2 Hatua ya kukomaa
Kwenye hatua ya tatu, ‘hatua ya kukomaa’ viumbe wakubwa kama mchwa na nyungunyungu
husaidia kusaga na kuchanganya mbolea. Hali ya anga ikiwa na joto jingi viumbe hawa hufanya
kazi haraka kuliko wakati ambapo hali ya anga ni baridi. Aina ya viungo vilivyotumika
kujenga/kukuza biwi na ukali/uchungu (pH) wa udongo pia huathiri kiwango cha mbolea kuoza.
4.4.3 Mazingira yanayohitajika kwenye biwi
Biwi huhitaji vitu vitatu: hewa, maji na joto.
• Hewa
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
24. Viumbe wadogo kwenye biwi huhitaji hewa ili waweze kuishi. Hewa ya carbon dioxide (CO2)
ambayo imetolewa na wadudu hawa huhitaji kutolewa nje. Ikiwa hewa safi itakosekana, viumbe
wengine wasiohitajika huingia na kutoa harufu mbaya na pia kufanya mbolea isioze haraka.
• Maji
Kazi ya viumbe wadogo huwa polepole ikiwa biwi ni kavu. Aidha ikiwa biwi litalowa maji basi
viumbe wadogo watakufa na kufanya biwi kuwa na uchachu badala ya kutengeneza mbolea.
Hivyo basi kukagua kiwango halisi cha maji huhitaji ujuzi fulani.
• Joto
Biwi hutoa joto wakati linaoza. Lundo likiwa na joto jingi viumbe wadogo hutoka, kisha huweza
kurudi pindi linapopoa. Muhimu kuhakikisha kuwa joto halizidi sana ili kuweza kuwa na mboji
nzuri yenye virutubisho.
4.5 Matunzo ya Biwi
Ili kupata mbolea nzuri, biwi linapojengwa yafaa lishughulikiwe kwa utaratibu. Biwi hilo
litahitaji maji, kupinduliwa, joto na muda unaofaa wa kukomaa.
4.5.1 Maji
• Wakati wa kiangazi biwi/lundo la mboji huhitaji kumwagiliwa maji kila wiki. Maji katika
lundo la mbolea hupimwa kwa kuweka fungu dogo la nyasi na kulitoa baada ya dakika
tano. Nyasi isipoonyesha majimaji au unyevu itabidi maji yamwagwe kwenye lundo hilo
• Kuna njia kadha za kuzuia mvuke kuinuka kutoka kwenye biwi, hali kadhalika kiwango
cha maji yanayomwagiliwa:
• Funika lundo kwa majani ya ndizi ama nyasi.
• Funika lundo kwa udongo.
• Lundo lisigeuzwegeuzwe
• Biwi likilowa maji itabidi kifunuliwe na kuachwa kikauke kwenye jua kabla ya kujengwa
tena.
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
25. 4.6 Kupindua/kugeuza
• Katika muda wa wiki tatu (3) baada ya kujenga/kukuza biwi/lundo ukubwa wake
utakuwa umepungua sana.
• Kupindua biwi uhakikishe ya kwamba majani yaliyo kando yameoza pia hewa safi
imerejeshwa.
• Kupindua biwi huchanganya majani yaliyotengenezwa na kukijenga upya. Majani
yalivyo kando huwekwa katikati, ikiwa kuna ukavu, maji mengi na majani/viungo vikavu
huongezwa.
• Kupindua kunatikiwa kufanyike kila baada ya wiki tatu.
• Hali ya joto na kiwango cha maji yafaa kupimwa siku chache baada ya kupinduliwa.
• Kupinduliwa kwa mara ya tatu kutahitajika ikiwa viungo havitakuwa vimeoza kikamilifu.
• Mbolea yaweza kutengenezwa bila kupinduliwa ila viungo vilivyo kando havitaoza.
Mbegu za magugu na viungo na magonjwa ya mimea hayatakufa.
• Viungo vilivyobaki hutengwa na kutumiwa kwenye biwi lingine. Japokuwa kugeuza
hakuna lazima, kunapendekezwa ili kupata mbolea nzuri.
4.6 Muda wa kukomaa na matumizi ya mboji
4.6.1 Muda wa kukomaa
• Lundo la mbolea yafaa liachwe likomae baada ya joto kupoa. Mbolea yaweza kutumiwa
mara tu viungo vya kwanza vinapokosa ama vinapopoteza utambusho, na rangi yake
ikageuka kuwa nyeusi na harufu ikawa ya kuvutia.
• Hata wakati huu mbolea yahitaji kufunikwa ili isilowe kwa maji ya mvua ama kukauka
kwa ajili ya jua bali ibakie na unyevunyevu. Mboji ikikawia muda mrefu kabla ya
kutumiwa, hupoteza rotuba na wanyama wadogo huifanya makazi yao.
4.6.2 Matumizi ya mboji
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
26. • Umuhimu mkuu wa mboji ni kuongeza mazao ya shamba kwa kusaidia udongo kushikilia
maji kwa muda mrefu na kufanya udongo kuwa na afya bora. Pia mbolea hufanya
udongo kushikamana hivyo hupunguza mmomonyoko wa udongo.
• Mbolea hutumiwa mara nyingi kwenye shamba lililoko karibu nyumbani na mbali na
nyumba. Wakati shamba huandaliwa kwa kupanda mbegu, mbolea huchanganywa
kwenye udongo wa juu. Mbolea haifai kuwekwa ndani ya udongo kiasi cha kwamba
mizizi ya mimea haitaifikia.
• Njia bora ni kuweka mbolea kidogo kwenye shimo ambamo mmea utapandwa. Kwenye
sehemu za ukame, mitaro huchimbwa kisha mbolea ikawekwa ambamo maji
hukusanyika na kutumiwa na mimea.
• Hupunguza magonjwa na wadudu waharibifu wa mimea yalioko udongoni hivyo basi
mimea huwa na nguvu, afya na hustahimili magonjwa na wadudu waharibifu.
• Mbolea vunde pia yaweza kutumiwa ili kufunika udongo usipoteze maji mengi. Mbolea
ambayo haiko tayari hasa kutumika kwa kazi kama hii iwekwe udongoni ili iendelee
kuoza na kuchanganyika kwenye udongo. Mbolea inapotumika kwa kuzuia maji kwenye
udongo, yafaa ifunikwe kwa majani madogo (matandazo). Hii itazuia mbolea isipoteze
rotuba kwa sababu ya joto jingi na miale ya jua.
• Mboji pia hutumika kukuza miche na hata kwa kuwalisha samaki.
MADA 5: HIFADHI YA MAJI
• Uhaba wa maji kwenye shughuli za kilimo katika nchi za tropiki ni jambo la kawaida.
Zipo sehemu ambazo ni budi kumwagilia ili mavuno yaweze kupatikana. Hata katika
maeneo yale yanayopata kiasi kikubwa cha mvua, mazao yanapungukiwa maji kipindi
cha kiangazi.
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
27. • Kilimo hai kinalenga kutumia kwa uendelevu rasilimali za asili zinazopatikana
mashambani. Kupatikana, kuvuna, na kuhifadhi maji ni mada muhimu kwa wale
wanaohimiza Kilimo hai na hifadhi ya mazingira.
• Kwenye mfumo wa kilimo cha kawaida tunatumia huduma za umwagiliaji kukabiliana na
upungufu wa maji. Kwa Kilimo hai na hifadhi ya mazingira mkulima anaweka
kipaumbele upatikanaji na upenyezaji maji ndani ya ardhi.
5.1 Uhifadhi wa maji ardhini
• Kipindi cha kiangazi kuna aina za udongo zinazoweza na zisizoweza kuipatia mimea
maji.
• Udongo mfinyanzi unaweza kuhifadhi maji mara tatu zaidi ya kile kiasi
kinachohifadhiwa na udongo kichanga.
• Kazi ya kuhifadhi maji ardhini inapunguza gharama za kumwagilia.
5.2 Namna ya kuhifadhi maji ardhini
• Wakati wa kiangazi mazao yanategemea unyevu kutoka ardhini. Uwezo wa udongo wa
kunyonya maji hutegemea mpangilio wa sehemu za udongo na kiasi cha mboji kilicho
ndani yake.
• Mboji kama spongi ni ghala ya maji. Udongo wenye mboji, unaweza kuhifadhi maji kwa
muda mrefu zaidi. Tunaweza kuongeza mboji mashambani kwa njia za samadi,mbolea
vunde, matandazo, na mbolea za majani.
• Matandazo yanapunguza unyaufu wa maji ardhini. Huuwekea udongo kivuli kutokana na
jua pamoja na kulinda ardhi isipate mno joto.
• Kulima kijuu juu au kuparua huzuia kukauka kwa udongo wa chini.
• Kuondoa magugu kunapunguza maji yanayopotea kupitia majani ya mimea hiyo.
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
28. 5.3 Kuvuna maji
• Wakati wa mvua kubwa, kiasi kidogo sana cha maji kinanywea ardhini. Sehemu kubwa
ya maji huwa inatiririka kama mkondo na huenda mbali bila kutumiwa na mimea.
• Ili kuvuna kiasi kikubwa cha maji ya mvua na kuyaingiza ardhini, hatuna budi kuongeza
uwezo wa udongo wa kunyonya maji. Udongo wa juu unapaswa kuwa na mpangilio
mzuri na nafasi wazi (pores and cavities) zinazosababishwa na minyoo.
• Mazao ya kufunika ardhi pamoja na matandazo huboresha mpangilio wa sehemu za
udongo. Tena hupunguza kasi ya mtiririko wa maji juu ya ardhi na kuyafanya yanywee
ndani yake.
• Kwenye mitelemko matuta ya kukinga maji, yanayasaidia yanywee ardhini hasa mitaro
inayotuamisha maji.
• Visahani vya kuzungukia miti hufanya kazi hiyo hiyo.
• Kwenye mashamba ya tambarare tunaweka mazao ndani ya mashimo (planting pits).
• Mitego hii ya maji inapofunikwa na matandazo inaleta faida kubwa. Ziada ya maji
kipindi cha mvua huweza kutumika wakati wa kiangazi.
• Njia nyingi za kuhifadhi maji zinahitaji nguvu kazi na gharama kubwa.
Tunapohifadhi maji ndani ya bwawa,tunaweza kufuga samaki ingawa maji huzama
ardhini au kunyauka kuelekea angani kama mvuke.
• Vile vile tunaweza kutengeneza matangi ya kuhifadhi maji. Ni vyema kupima na kuamua
endapo tunahitaji kutengeneza chombo cha kuhifadhi maji kwa kulinganisha matumizi,
mapato, na/au kupunguza eneo la kilimo ili kuweka hiyo huduma ya kuhifadhia maji.
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
29. MADA 6: DHANA YA VIKUNDI
6.0 UUNDAJI WA KIKUNDI
6.1 KIKUNDI NI NINI?
• Ni idadi maalumu ya watu waliokubaliana/waliungana wenye lengo na nia ya
kukusanya nguvu, rasiliamali, na mawazo yao ili kutatua changamoto
zinazowakabili katika mazingira yao.
• Ni watu kadhaa walioungana pamoja kufikia lengo maalumu la pamoja la
maendeleo ya kiuchumi,kijamii na kisiasa.
• Ni idadi ya watu wenye nia,mwelekeo na lengo moja kufanya shughuli fulani ya
kijamii na kiuchumi.
6.2 UMUHIMU WA KIKUNDI
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
30. Kikundi huwaunganisha wakulima na:
• Masoko
• Asasi za kifedha
• Watoa huduma za kilimo
• Kuwa na uwezo wa kupanga bei za mazao yao
• Kuwa na sauti ya pamoja
• Kufanya kazi kwa juhudi(kazi kubwa bila maumivu)
• Kufanya kazi kwa kushirikiana
• Kuwa na vikao vya mara kwa mara
6.3 AINA ZA VIKUNDI
Kuna aina kuu mbili za vikundi
• Vikundi vyenye malengo ya kiuchumi (ujasiliamali)
• Vikundi vyenye malengo ya kijamii(utoaji wa huduma)eg UKIMWI
6.4 TOFAUTI KATI YA KIKUNDI NA MKUSANYIKO
KIKUNDI MKUSANYIKO
→ Sifa maalumu huwekwa hakuna sifa maalumu.
→ Idadi maalumu ya watu hakuna idadi maalum ya watu
→ Kuna uongozi hakuna uongozi
→ Mipango endelevu hakuna mipango
→ Sheria +taratibu hakuna sheria/taratibu
→ Mda maalum hakuna mda maalumu
→ Utunzaji wa kumbukumbu hakuna taarifa inawekwa
Ni bora mbaki 10 wenye msimamo kuliko 30 wasiofuta taratibu za kikundi.
6.5 SIFA KUU ZA WANAKIKUNDI
• Kufahamiana(historia ya kazi, ukweli, utendaji)
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
31. • Kupendana(kutakiana maendeleo)
• Kushibana(utayali wa kusaidiana)
• Kuaminiana(kutokuwa tayari kuangusha wenzio)
• UMOJA
• Mkulima ,mwenye mashamba anayoyalima karibia kila msimu(wenye mafanikio na
wa ngazi ya chini)
• Wanao kubalika na wana kijiji wenzake
• Angalau wajue kusoma na kuandika
• Wanao ruhusu wenzake kujifunza kutoka kwake
• Jinsia zote ziwepo(ke na me)
• Awe tayari kujifunza na kupokea ushauri
• Upatikanaji wao uwe wa uhakika
• Kuanzia miaka 18 mpaka 45
• Mkazi wa mda mrefu kitongojini na kjijini kwa ujumla
• Awe tayari kufanya alichoona na kufundisha wengine
• Awe tayari kutumia sehemu ya shamba lake kufundishwa na kufundishia wengine
siku zijazo
• Wawe tayari kufanya shughuli za kikundi bila kutegemea
posho/malipo ya Fedha.
• Wawe na ari ya kujiendeleza kwa kufuata mbinu walizojifunza.
• Wawe tayari kufanya kazi kwa pamoja kwenye kikundi
• Wanaopendana na kujaliana.
Zingatia:
Watakao chaguliwa wana jukumu la kubadili mfumo wa ulimaji/kilimo hapo kitongojini baada
ya kujifunza KILIMO HIFADHI, HIVYO WASIANGUSHE MRADI NA KIJIJI .
6.6 JINSI YA KUANZISHA VIKUNDI
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
32. 6.6.1 VIKUNDI VINAANZAJE?
Uzoefu unaonyesha vikundi vinaweza kuanzishwa kwa njia tofauti
i. Semina,warsha na ziara za mafunzo ya kubadilishana uzoefu na ujuzi maeneo
mengine.
ii. Mashirika,wanasiasa, kwa kutaka kufanikisha mipango maalumu huanzisha
vikundi ili kurahisisha utekelezaji.
iii. Vikundi vinaweza kuundwa kutokana na tatizo au hitaji maalumu la wenyeji.
iv. Kikundi kinaweza kuzaliwa kutokana na wazo la mtu mmoja.
6.6.2 MAMBO/VIGEZO VYA KUZINGATIA KABLA YA UUNDAJI KIKUNDI IMARA.
• Kuwepo na sababu/lengo la kuanzisha kukundi
• Kuwepo na matokeo yatakayowanufaisha au kuwavutia
• Kuwe na haja mfano elimu, soko au mtaji
• Kuwe na kazi
• Wanachama wote wawe na nia/lengo moja
• Wanakikundi wawe ni watu wa tabia,tatizo,shughuli,mtizamo mmoja
• Wanachama lazima wawe wakazi wa eneo husika.
• Viongozi wasitoke kwenye familia moja.
• Wanachama wote wawe na mtazamo chanya juu ya kikundi
• Idadi ya wanakikundi isiwe kubwa wala kidogo sana.Mtu asilazimishwe kuingia kwenye
kikundi na awe huru kutoka(muungano uwe wa hiari)
• Kikundi kiwe na uhuru na kuamua mambo yake (kisijihisi ni cha mradi au mradi au
mtaalamu,kitalemaa kimawazo)
6.6.3 JINSI YA KUANZISHA KIKUNDI
i. Hakikisha msukumo wa kuanzisha kikundi unatoka ndani ya wahusika ,wazo laweza
toka nje.
ii. Kikundi kiwe na watu wachache (20-30)_Hurahisisha kufahamiana na kuaminiana.
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
33. iii. Hakikisha utengenezaji wa malengo,katiba,kanuni,jina la kikundi unahusisha walengwa.
iv. Pendekeza viongozi wa vikundi watakavyo patikana(m/kiti,msaidizi na katibu)
mwanachama aelewe sifa za kiongozi bora.
v. Tengeneza katiba kulingana na malengo ya kikundi.
vi. Kuwe na sheria na kanuni za kikundi na kila mwanakikundi awe anazijua ili akikiuka
aonywe(kuhudhuria vikao,kutoa mchango,kusaidiana katika matatizo)
vii. Tengeneza katiba ya kikundi.siku nzuri/huru kwa wote kuhudhuria.
6.7 KAZI ZA KIKUNDI
I. KUPANGA NA KUWEKA MALENGO
Hii ni kazi ya wanakikundi wote
Inabidi ifanyike mara kwa mara
Uzoefu wa wanakikundi wa mazingira yao uzingatiwe
II. KUTATUA TOFAUTI ZA MAWAZO
Kila penye watu wengi pana mawazo mengi yanayotofautiana
Ni vipi kutofautiana bila uhasama
Ni vipi kufika muafaka
Ni vipi mawazo tofauti yanaweza leta umoja
III. KUTAFUTA VITENDEA KAZI
Ili kufanikisha malengo vinahitajika
Fedha
Utaalamu/Ushauri
Nguvu za mikono
Pembejeo
Huduma nyingine(usafiri)
IV. MATUMIZI BORA YA VIFAA VYA KAZI
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
34. Vitendea kazi vizuri vikipatikana muhimu vitumike ipasavyo ili kufikia malengo ya kikundi. Iwe
majengo, pembejeo, duka, nguvu za watu n.k.
Lazima ziratibiwe vizuri,kuwe na kumbukumbu nzuri na uwasilishaji wa mahesabu.
V. KUTOA HUDUMA KWA WANAKIKUNDI
Mradi na viongozi inabidi kutoa huduma fulani fulani kwa wanakikundi; Kutafuta
ushauri,masoko,mikopo,pembejeo n.k. Kikundi kisipotoa huduma hizo wengine hawatapata
hamasa ya kujiunga kwenye kikundi.
VI. KUTETEA HAKI ZA WANAKIKUNDI
Jukumu mojawapo la kikundi ni kujenga uwezo na kujiamini kwa wanakikundi ili waweze
kutetea maslahi yao pale inapobidi. Ili kuleta mafanikio kikundini mara nyingine inabidi
kupingana na sera za watu/makundi mengine
6.8 UONGOZI
6.10.1 Kiongozi ni nani?
Kiongozi ni mtu/mwanakikundi
- Anayechaguliwa na wenzake
- Ndiye msimamizi wa sheria na taratibu za kikundi na kuhakikisha kwamba rasilimali zao
ziko salama na lengo la kikundi linafikiwa
- Uongozi una jukumu la kutufikisha pale tulipokubaliana tufike.
6.10.2 Sifa za kiongozi
- Mwajibikaji – Awe na uwezo wa kuwatumikia watu wengine kadri ya mahitaji yao
- Muwazi – Wambie watu ukweli hata kama unauma
- Mkweli – usiwaahidi watu uongo
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
35. i. Mwenyekiti
- Kazi zake ( Ndiye msimamizi mkuu wa shughuli zote za kikundi)
- Sifa (awe mpigania haki za watu wengine na asiwe mwepesi kudhurumu haki za
Watu.
ii. Katibu
- Kazi zake (kutunza kumbukumbu)
- Sifa (ajue kuandika vizuri na haraka)
iii. Mweka hazina
Taratibu zifuatwe msisubiri kumlaani mtu leo na mbinguni
6.10.3 JE WEWE NI KIONGOZI??
K---- Kubali kushauriwa
I---- Ielewe hali ya mahali ulipo
O----Ondoa upendeleo
N----Nena kauli thabiti na zinazotekelezeka
G----Gawa Majukumu
O----Onesha mifano kwa matendo(onesha njia)
Z---- Zuia mipasuko na Migawanyiko.
I---- Inua kiwango cha utendaji wa majukumu(inua unaowaongoza)
6.10.4 UCHAGUZI
- Viongozi wa kikundi watachaguliwa kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa na
kikundi. Katiba ieleze waziwazi ni uongozi wa kikundi utafanyika.
- Wanakikundi wapendekeze ni aina gani ya uchaguzi utafanyika ili kuwapata viongozi
wao kwa mfano Kura – siri, kupendekezwa, kuteuliwa
Wanakikundi wachague mfumo wa kuchagua
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
36. 6.10.5 KATIBA (roho ya kikundi)
Kila kikundi kinatakiwa kutengeneza katiba yake itakayowaongoza katika utekelezaji wa
shughuli zao za kila siku. Katiba ni muongozo wa kimsingi ambao haki, majukumu na wajibu wa
wanachama hulindwa na kuhifadhi.
6.10.5.1 Wajibu/Umuhimu wa Katiba katika kikundi
1. Inahamasisha usawa miongoni mwa wanakikundi
2. Huelekeza umuhimu, majukumu na wajibu wa vyombo vyote
3. Hulinda shughuli za kila siku na shughuli za kikundi pia husema nini kifanyike na
nini kisifanyike
4. Hufafanua malengo ya kikundi
5. Huongeza uwajibikaji wa uwazi
6. Huhamasisha ushirikiano kwa wanachama wote kwa kuwa huelezea kwa wajibu
na majukumu ya kila mwanachama na viongozi
7. Husaidia kupunguza kutoelewana/ugomvi kwa kuweka njia ya kutatua
6.10.5.2 Njia za kuandaa rasimu ya katiba
Uundaji wa katiba hufanywa tofauti kwa kila kikundi, baadhi yao husaidiwa na
mwanasheria kwa gharama za wanakikundi na nyingine hufanywa na wanakikundi
(kamati) iliyoidhinishwa na mkutano mkuu. Kamati hii huitajika kuundwa na watu
wenye uelewa wa masuala ya kisheria. Baada ya kamati kumaliza kuandaa rasimu
ya katiba, wanachama hujadili katika mkutano mkuu na kuifanyia marekebisho.
Baada ya ushauri wa wadau kujumuisha , toleo la mwisho huandaliwa na
kudhibitishwa na mkutano mkuu.
6.10.5.3 Kanuni za katiba bora
a) Ushirikishwaji
b) Isiyopendelea
c) Isiyobadilika
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)
37. d) Rahisi
e) Imara
KILIMO HAI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
MUONGOZO WA MAFUNZO UMEANDALIWA NA JEROME ERNEST NA ELIDA FUNDI ( MJUMITA)