2. YALIYOMO
Utangulizi
Hali ya hewa, Udongo
Utayarishaji wa Shamba
Mbegu
Upandaji
Mbolea
Upaliliaji na Unyevu
Magonjwa
Wadudu
Uvunaji, Soko
01
02
03
04
05
06
07
08
09
10
3. UTANGULIZI
01 WWW.KILIMOMAX.COM
• Karoti ni zao la mbogamboga ambalo ni zao la
mizizi, kwa kawaida hupatikana katika rangi ya
machungwa, nyekundu, na njano.
• Karoti hutumika sana kwa ajili ya kuongeza
radha kama kiungo kwenye mboga au kwenye
kachumbari.
• Pia zina faida kubwa katika mwili kwa kuupatia
vitamini A na C pamoja na madini ya chuma
hasa pale mtu atafunapo.
4. • Karoti zinahitaji hali isiyokuwa na joto sana,
wala baridi sana, kati ya nyuzi za degree 15
mpaka 27 za sentigredi.
• Kama ukanda wa pwani una joto kali,
inatakiwa karoti zilimwe miezi ya majira ya
baridi.
• Karoti zinazotoka mazingira ya baridi huwa na
radha nzuri pamoja na harufu nzuri.
• Udongo wa kichanga chepesi na tifutifu ndio
unafaa katika kilimo cha karoti,
• Udongo wa mfinyanzi na udongo mzito
hudumaza mazao
HALI YA HEWA NA UDONGO
02 WWW.KILIMOMAX.COM
15°C - 27°C
5. • Karoti zinahitaji shamba lilimwe kwa trekta,
ng”ombe au jembe la mkono kwa kina cha
sentimita 30 hadi 45 kwenda chini ya ardhi.
• Mkulima anatakiwa kuandaa matuta yenye
mwinuko wa kimo cha sentimita 28-40
kwenye shamba, na upana wa mita 1, pia mita
1.5 umbali wa tuta moja hadi linguine.
• Kwa maandalizi mazuri tengeneza mifereji
midogo ya kusiha mbegu za karoti yenye
umbali wa sentimita 15-20. , mifereji minne
kwa tuta.
UTAYARISHAJI WA SHAMBA
03 WWW.KILIMOMAX.COM
6. MBEGU
04 WWW.KILIMOMAX.COM
• Jinsi ya kujua mbegu nzuri zenye uwezo wa
kukua bila wasiwasi,
• Mbegu zenye uwezo wa kuota hutoa harufu
kali unapozifikicha,
• Zilizopoteza uwezo wa kuota huwa hazitoi
harufu yoyote,
• Ili mbegu zoite haraka ziloweke katika maji
kwa muda wa saa 24,
• Baada ya hapo changanya mbegu hizo na
mchanga, kwa kiasi kinacholingana ili kupata
mtawanyiko mzuri wa mbegu wakati wa
kupanda /kusia.
7. Chantenay
Red Core
Nantes
AINA ZA MBEGU
05 WWW.KILIMOMAX.COM
Aina hii inapatikana maeneo
mengi na inalimwa sana hapa
Tanzania. Inakuwa kwa haraka
na inapendwa na watu
kutafunwa kwani ladha yake ni
tamu sana.
Hii pia ina ladha nzuri nainataka
kufanana na Nantes lakini mizizi
yake ni dhaifu ukilinganisha na
Nantes.
Oxheart
Karoti za Oxheart ni fupi na
nene. Huvunwa baada ya muda
mfupi kulinganisha na aina
zingine.
8. 2. Weka mbegu katika chupa ya milimita 100 na toboa
kidogo mfuniko, baada ya hapo sia mbegu katika mifereji
ya kupandia kwa kutikisa chupa yenye mbegu, ndipo,
funika mbegu kwa kutumia mboji au mchanga, ukimaliza
nyunyizia maji ya kutosha
3. Funika tuta na plastiki nyeusi, hatua nyingine
kandamiza plastiki kwa pembeni na kwa mabonge ya
udongo ili isipeperushwe na upepo.
UPANDAJI
06 WWW.KILIMOMAX.COM
• Inahitajika uoteshe kwenye kitalu ndipo uhamishie
shambani
9. 5. Baadae ondoa plastiki mara moja pindi utakapoona
mbegu moja tu iliyoota. Usicheleweshe kuondoa plastiki
husababisha miche iliyoota kufa kwa kuunguzwa na joto
lililo katika plastiki. Hapo tayari kwa kupanda shambani
6. Upandaji wa moja kwa moja shambani katika matuta au
sesa. Kiasi cha kilo 8 za mbegu kinatosha kupandwa
kwenye hekta moja.
UPANDAJI...
07 WWW.KILIMOMAX.COM
4. Mbegu huota baada ya siku 3-5 kutegemeana na hali ya
hewa, Inakupasa kukagua shamba mara tatu kwa siku
10. MBOLEA
08 WWW.KILIMOMAX.COM
• Weka mbolea aina za asili (samadi au mboji)
mwanzoni,
• Ila kama haukutumia mbolea ya samadi au
mboji, weka mbolea ya S/A Kilogramu 100
kwa hekta kama haukutumia mbolea za
asili,uKama ulitumia mbolea za asili basi weka
kilogramu 50 kwa hekta,
• Kisha tumia NPK wiki sita baada ya kupanda,
• Matumizi ya mbolea za maji yafanyike kila
baada ya wiki mbili kutegemeana na mahitaji.
NPK
11. 2. Kwa kung”olea kwa mkono, jembe na njia
nyinginezo za kupalilia
3. Kwenye udongo hakikisha kuna unyevu wa
kutosha kama sio kipindi cha mvua inatakiwa
umwagilie shamba lako kwa wiki mara mbili.
UPALILIAJI NA UNYEVU
09 WWW.KILIMOMAX.COM
• Ili kupata mavuno mengi palilia shamba mara
kwa mara ili kuhakikisha shamba halina
magugu na nyasi.
13. MADOA JANI (LEAF SPOT)
11 WWW.KILIMOMAX.COM
• Ugonjwa huu husababishwa na ukungu , na hutokea
wakati karoti zina urefu wa sentimita 13 mpaka 15,
• Hushambulia majani na kuyafanya yawe na madoa
yenye rangi nyeusi iliyochanganyika na kijivu au
kahawia.
• Sehemu zinazozunguka madoa haya hubadilika rangi
na kuwa njano.
• Ugonjwa ukizidi majani hukauka,
• Zuia ugonjwa huu kwa kunyunyizia dawa za ukungu
kama vile Dithane-M 45, Blitox,Copperhydroxide
(kocide), Cupric Hydroxide (Champion), Copper
Oxychloride, Antrocol, Topsin M-70% na Ridomil
14. KUOZA MIZIZI (SCLEROTINIA ROT)
12 WWW.KILIMOMAX.COM
• Ugonjwa huu husababishwa na ukungu, pia
hushambulia mizizi na majani.
• Dalili zake ni kuoza kwa mizizi na majani, baadaye
sehemu hizi hufunikwa na uyoga mweupe
• Kwenye uyoga huu huota siklerotia kubwa zenye rangi
nyeusi.
ZUIA
• Epuka kustawisha karoti kwenye maeneo
yaliyoshambuliwa na ugonjwa huu,
• Nyunyizia dawa za ukungu kama vile Dithane M-45,
Blitox, Topsin-M 70% na Ridomil.
15. MADOA MEUSI (BLACK LEAF SPOT)
13 WWW.KILIMOMAX.COM
• Huu pia ni ugonjwa wa ukungu unaoshambulia majani
na mizizi,
• Majani yaliyoshambuliwa huwa na rangi ya manjano
ambayo baadaye hubadilika na kuwa kahawia,
• Mizizi huwa na madoa meusi yaliyodidimia,
• Ugonjwa huu unaweza kuzuiwa kwa kutumia mbegu
zilizothibitishwa kitaalamu, kubadilisha mazao na
kuepuka kujeruhi karoti wakati wa kupalilia na kuvuna
au kusafirisha.
17. MINYOO FUNDO (KNOT NEMATODES)
15 WWW.KILIMOMAX.COM
• Minyoo hii hushambulia mizizi na kuifanya iwe na
vinundu,
• Hali hii husababisha mmea kudumaa na kupunguza
mavuno,
• Minyoo fundo huweza kuzuiwa kwa kupadilisha mazao,
• Baada ya kuvuna usipande mazao ya jamii ya karoti au
mazao yanayoshambuliwa na wadudu hawa,
• Unaweza kupanda mazao ambayo hayashambuliwi na
minyoo fundo kama vile mahindi,
• Pia hakikisha shamba ni safi wakati wote.
18. INZI WA KAROTI
• Mashambulizi hufanywa na funza ambaye hutoboa
mizizi
• Ili kuzuia wadudu hawa tumia dawa kama vile
Dichlorvos, Sapa Diazinon na Fenvalerate
• Pia badilisha mazao
• Na wakati wa kupalilia pandishia udongo kufunika
mizizi.
16 WWW.KILIMOMAX.COM
19. KAROTI KUWA NA MIZIZI MINGI (FOLKING)
17 WWW.KILIMOMAX.COM
• Hii hutokea kama karoti zimepandwa kwenye udongo
wenye takataka nyingi na usiolainishwa vizuri,
• Vile vile utumiaji wa mbolea za asili zisizooza vizuri
unaweza kusababisha karoti kuwa na mizizi mingi,
• Hali hii inaweza kuzuiliwa kwa kulainisha udongo vizuri
na kutumia mbolea za asili zilizooza vizuri.
20. UVUNAJI
18 WWW.KILIMOMAX.COM
11-13 15-25
• Karoti hukomaa baada ya wiki 11 mpaka 13 kutoka muda ilipokuwa
imepandwa kulingana na hali ya hewa ya eneo ilipolimwa.
• Tani 15 hadi 25 za karoti huvunwa katika hekta moja.
WEEK
S
TONS
21. SOKO
19 WWW.KILIMOMAX.COM
• Karoti inatumika sana na watu mbalimbali,
• Tafuta soko pale unapoona karoti zako zimekaribia
kukomaa,
• Ulizia wanunuzi ni bei gani wataweza kuchukua pia
kiasi gani watachukua.