Language : swahili
Hebu sote tukubaliane ya kwamba kwa namna moja au nyingine Kanisa limeliacha fundisho la uzima, na matokeo yake yanaonekana katika maisha ya watu wa Mungu.
Viongozi wengi wameathiriwa na mafundisho ya mafanikio ya miaka ya hivi karibuni, na wanatafuta kujinufaisha wenyewe. Wengine hawatambui ya kwamba injili ya Msalaba ndiyo nguvu ya Mungu itakayowafikisha Wakristo katika utu uzima rohoni.
Umefika wakati tuyazungumzie mambo fulani ya msingi waziwazi, ili Wakristo watambue ya kwamba Bwana ana mambo mazuri zaidi kwa ajili yao, makusudi watembee katika uhuru na katika ushindi!