Unlocking the Power of ChatGPT and AI in Testing - A Real-World Look, present...
Dada yangu sura y1
1. DADA YANGU SURA YA ..1..
By Adela Dally Kavishe in UWANJA WA SIMULIZI · Edit Doc
Mapenzi ni kitu ambacho kimechukua nafasi kubwa sana katika maisha ya watu
kote duniani. Mapenzi haya yanaweza kuleta furaha sana endapo mtu atampata
mtu sahihi ambaye atakuwa ni muwazi, mwenye mapenzi ya kweli na kuheshimu
uhusiano huo. Lakini mapenzi yanaweza kuleta karaha au kukosa amani kabisa
kama kutakuwa na migogoro ambayo unakuta inasababishwa na kukosa uaminifu
na kuleta ugomvi kati ya wawili wapendanao. Mapenzi haya yanaweza
yakasababisha ndugu kugombana, marafiki kukosana na hata kuuana.
*****
Eliza na Upendo ni wasichana warembo waliozaliwa katika familia ya kitajiri
mkoani Morogoro. Wasichana hawa waliishi katika maisha ya kifahari kutokana na
Baba yao Mzee Bondi kuwa na uwezo mkubwa sana kifedha. Mzee Bondi
aliwapenda sana mabinti zake na alipenda wasome kwa bidii ili baadaye waje
kuwa na maisha bora. Eliza na Upendo walisoma katika hali nzuri sana hadi
kufikia elimu ya chuo, ambapo Upendo alikuwa akisoma Chuo Kikuuu cha Dar es
salaam na Eliza Chuo cha Uhasibu Arusha. Kutokana na masomo walitengana na
kuonana mara chache kipindi cha likizo.
Baadaye Eliza na Upendo walijikuta wakijiingiza katika uhusiano wa kimapenzi
wote wawili kwa kijana mmoja mtanashati aliyeitwa James bila kujijua. Uhusiano
wa kimapenzi kwa mwanamume mmoja ulileta migogoro katika familia yao.
*********
Baada ya kumaliza Kidato cha Sita Upendo alipangiwa kwenda kuendelea na
masomo ya Chuo Mkoa wa Dar es salaam. Baba yake alifurahi sana na kumuahidi
kuwa angempa zawadi nono kama angefanya vizuri akiwa Chuo. Kabla ya
kujiunga na chuo Upendo alifanyiwa sherehe kubwa ya kumpongeza, ambayo
2. ilihudhuriwa na watu wengi sana ndugu jamaa na marafiki. Wakati huo mdogo
wake Eliza alikuwa Kidato cha Sita kwani walipishana mwaka mmoja tu na kwa
jinsi walivyokuwa, walionekana kama mapacha. Wakati mwingine ilikuwa ni
vigumu kwa watu ambao walikuwa hawajawaona kujua mkubwa ni yupi na mdogo
ni yupi.
Siku zilipokaribia za kwenda Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Upendo alijiandaa
barabara kwa ajili ya kuanza masomo ya Chuo. Siku moja kabla ya kuondoka
Mama na Baba yake walimwita na kuzungumza naye mazungumzo ili kumwasa na
kumpa ushauri.
“Upendo tumeishi wote kutoka ukiwa mdogo, hujawahi kuishi mbali nasi kuanzia
masomo ya elimu ya shule ya msingi hadi elimu ya Sekondari. Umesomea
Morogoro, sasa unakwenda Dar es salaam kuanza maisha mapya ya kuishi mbali
na sisi. Ninakuomba ukasome kwa bidii ili ujiandalie maisha yako ya baadaye.”
Mzee Bondi alimaliza kutoa nasaha zake, huku Upendo akisikiliza kwa makini
kabisa.
“Umsikilize baba yako kwa makini kwa sababu dunia ya sasa imeharibika
mwanangu. Magonjwa ni mengi na ukifika huko sio ndio ukasahau
kilichokupeleka. Kumbuka kinachokupeleka ni masomo na sio starehe. Nadhani
umenielewa.” Alisisitiza Mama yake.
“Jamani Mama nitasoma kwa bidii mbona unaongea hivyo.” Upendo alihamaki
“Lazima niongee mwanangu vijana wa sasa mnakutana na mambo mengi na
vishawishi vingi usipokuwa makini utapoteza kabisa mwelekeo na malengo yako.”
Mama upendo aliendelea kutoa nasaha.
“Baba na Mama nimewasikia, kamwe sitoenda kutenda yasiyo sahihi, nitasoma na
nitawafurahisha siku zote wazazi wangu.” Upendo alijibu kwa unyenyekevu.
Baada ya maongezi hayo wote walisimama na kuelekea kulala ili Upendo akaanze
kujiandaa na safari. Upendo aliingia chumbani na kuanza kupanga vitu vyake
akisaidiana na mdogo wake Eliza.
“Ndugu yangu si nilikuwa nimekaa na Mama na Baba sebuleni wananipa wosia
namna ya kuishi huko Chuo.” Alisema Upendo.
3. “Eheh! Ilikuaje? Kwa sababu Mama naye akiamua kuongea ni balaa wamesemaje
hao wazee?” Alidadisi Eliza.
“Mwenzangu, Baba na Mama wameniambia nikienda nisisahau kilichonipeleka
nisiendekeze starehe.” Alisema Upendo.
“Heh! Hao wazee nao inamaana ukakae tu unasoma hata disko usijichanganye?
Aka mwaya sisi bado vijana lazima tujirushe we ngoja mi nimalize Kidato cha Sita
nikienda chuo nitajirusha sana kwani hapa nyumbani hawa wazee wanatubania
sana.” Alizungumza Eliza.
“Usiseme hivyo mdogo wangu mimi naona Baba na Mama wapo sahihi, kwani
nikianza kujiingiza kwenye starehe nitajikuta nafeli mitihani halafu malengo yangu
ya kuwa mwanasheria yasitimie, we mwenzangu unawaza kujirusha tu.” Alijibu
Upendo.
“Kujirusha ni wajibu na kusoma nitasoma tu, haya bwana tufanye haraka tuwahi
kulala hao wazee watakuamsha mapema kesho.” Alimaliza Eliza. Usikose uhondo
zaidi itaendelea katika sura ya 2