1. JOSEPH LILO AFISA MIFUGO -0765096371,0768287853. JORENO VEGETABLE LEATHER TANNINGpg. 1
SURA YA
1. Mbuzi ni baadhi ya wanyama waliko
katika kundi la wanyama wadogo
wanaofugwa nyumbani. Mbuzi anaweza
kufugwa kwa gharama nafuu na kuishi
katika mazingira magumu. Mbuzi
anauwezo wa kuvumilia maradhi na
ukame ukilinganisha na wanyama
wengine.
2. Kwakuwa maumbile ya mbuzi ni
madogo wanaweza kufugwa katika
eneo dogo na wanaweza kuhudumiwa
na familia yenye uwezo wa kufanya kazi
na hivyo kuwaletea kipato katika familia
yao. Mbuzi wanaweza kumpatia mfugaji
mbuzi wengi kwa kipindi kifupi
kwakuwa uzao wao ni wa muda mfupi
ambao hulea mimba kwa kati ya miezi
mitatu hivi
3. Mbuzi hufugwa kwa ajili ya nyama,
ngozi,maziwa,mbolea, kujiongezea
kipato katika familia na mazao mengi
yanayotokana na ufugaji kwa ajili ya
familia na jamii nzima.
4. Mbuzi ni lazima wawekewe utaratibu
mzuri ili wafugwe kwa weledi mkubwa.
kwanza wafugwe kwenye banda zuri au
zizi bora, wachaguliwe kutokana na koo
bora au kutoka katika koo bora
wapatiwe chakula chenye lishe bora na
sahihi inayotegemea mchanganyo mzuri
wa uchanganyaji chakula kutokana na
umri wao na mahitaji ya mwili,
Kuzingatia mbinu za udhibiti wa
magonjwa, kutunza kumbu kumbu na
kuzalisha nyama yenye ubora unaokidhi
viwango kwa walaji.
1.Ni sifa gani zinazomfanya mbuzi afae sana
kufugwa katika maeneo tofauti tofauti?
2.Ni faida zipi ambazo mfugaji anapata akiwa
na shamba la mbuzi ?
3. Kwanini tunafuga mbuzi ?
4. Mahitaji gani mbuzi anapaswa kupatiwa
wakati wa ufugaji ?
SIFA ZA ZIZI BORA LA MBUZI.
5. Kwa kawaida maeneo ya vijijini
kunakuwa na maeneo ya wazi ambapo
mbuzi wanaweza kutengenezewa zizi
kwa ajili ya kuwahifadhi ili wapumzike
kwa ajili ya kesho. Lakini mijini inaweza
kuwa vigumu kuwa na zizi kwakuwa
kuna ufinyo wa maeneo. Kwahiyo
maeneo ya vijijini yanafaa kuwa na
mazizi kwa ajili ya mbuzi.
6. Mbuzi anapaswa kufugwa katika zizi
bora na zizi linapawsa kuwa imara na
linaloweza kumlinda mnyamakutokana
na wadudu na wanyama hatari na
wezi,lijengwe kwenye mwinuko ili maji
yasituamekwa urahisi,ukubwa wa zizi
uzingatie idadi ya mbuzi na mbuzi
watengwe kutokana na umri, zizi
liruhusu usafi kufanyika kwa urahisi
7. Kwa ufugaji wa ndani tu (shadidi)
mahali ambapo mbuzi hufugwa ndani
maisha yake yote na kuletewa chakula
ndani panapaswa kuzingatia banda
bora. Banda linaweza kujengwa kwa
matofali, mabanzi, fito za miti na vifaa
vingine vya ujenzi kutokana na
upatikanaji wa vifaa hivyo. Vifaa hivyo
vinapaswa kuwa imara na vyenye
kudumu na visivyo rahisi kuficha
wadudu au wanyama wakali.vifaa hivyo
viwe rahisi kufanyiwa usafi au
visimjeruhi mtu au mbuzi anapokuwa
ndani ya banda.
5.kwanini kunatofauti kubwa kati ya vijijini na
mijini inapohusu kutengeneza zizi la mbuzi?
6. Taja sifa za zizi bora la mbuzi.
7. Ni ufugaji wa aina gani mbuzi ambapo
mbuzi huletewa chakula ndani tu ?na vifaa
gani vinavyo faa kwa ajili ya ujenzi wa banda
la mbuzi?
SURA YA KWANZA
UFUGAJI WA MBUZI
2. JOSEPH LILO AFISA MIFUGO -0765096371,0768287853. JORENO VEGETABLE LEATHER TANNINGpg. 2
8. Banda bora la mbuzi linapaswa kuwa na
sifa kama hizi; 1.liwe na vyumba tofauti
tofauti kwa ajili ya majike, madume,
watoto, wanaonenepeshwa, wagonjwa
na wazee 2.liwe na sehemu ya kuwekea
chakula,maji na mahali pa kuweka jiwe
la chumvi 3.liwe na sakafu ya kichanja
chenye urefu wa mita 1 kutoka ardhini.
4.liwe katika sehemu isiyotuaimisha
maji kwa urahisi. 5. Liwe mbali kidogo
na makazi au nyumba ya kuishi. 6.
Banda lizingatie mwelekeo wa upepo 7.
Banda lenye mwanga wa kutosha na
nafasi ya kutosha na inayoruhusu usafi
kufanyika.banda linapaswa liwe na
uwezo wa kuwahifadhi kiafya na pia
dhidi ya hewa hatarishi mfano jua kali,
upepo mkali, baridi na mvua kali na
wanyama hatari.
VIFAA VYA KUJENGEA.
9. Kwa ushauri wa kitaalamu banda la
mbuzi linapaswa kutumia vifaa
vinavyopatikana kwa urahisi na karibu
katika maeneo unaoishi. Ukubwa wa
banda unategemea idadi ya mbuzi
wanaofugwa na ukubwa wa umbo la
mbuzi.Watoto 0.3m2
, wasio na mimba
1.5 m2
, wenye mimba 1.9m2
, Dume 2.8
m2
10. Banda la mbuzi linapaswa kuwa na paa
la miti,mbao na kuezekwa kwa
nyasi,makuti,majani ya
migomba,mabati au hata vigae
kutokana na uwezo wa mfugaji. Kuta za
zijengwe kwa
mabanzi,mbao,nguzo,wavu wa waya,
fito na matofali. Kuta ziwe imara
zinazoruhusu hewa na mwanga wa
kutosha.
9.Kutokana na ukubwa na umbile la mnyama
mabanda yanapaswa kuwa na ukubwa gani?
10.Taja vifaa vya kujengea banda bora la
mbuzi.
11. Mlango uwe na ukubwa wa sentimita
60 x 150. Sakafu inaweza kuwa ya zege
au ya kichanja cha fito,miti,mianzi,,
mbao au mabanzi na iweze mkojo na
kinyesi kupita. Chumba cha majike na
watoto kiwe na nafasi ya sentimita 1.25
kati ya papi,fito au mti hadi mti.
Chumba cha mbuzi wakubwa nafasi iwe
sentimita 1.9 kati mbao na mbao.
UCHAGUZI WA MBUZI WA
KUFUGWA.
12. Madhumuni ya kuchagua mbuzi wa
kufugwa ni kuboresha uzalishaji na
kuendeleza kizazi bora kwa sasa na
wakati ujao. Uchaguzi hufanyika kwa
kuangalia umbile, uzalishaji, na kumbu
kumbu za wazazi kama vile umbo
kubwa, ukuaji wa haraka uwezo wa
kutunza watoto na kutoa maziwa.
13. Mbuzi wanaofaa kwa ajili ya nyama ni
boer na chotara wao. Na mbuzi wa asili
kama vile pare white,newala na ujiji.
Mbuzi aina ya malya (blended) wanafaa
kwa ajili ya kuzalisha maziwa na nyama
na wanasifa kama zifutazo; historia ya
kukua,kuzaa ( ikiwezekana pacha) na
uwezo wa kutunza watoto vizuri. Umbo
la mstatili linaloashiria utoaji wa nyama
nyingi na asiwe na ulemavu.
11.Mlango,sakafu na nafasi katika chumba
cha mbuzi kinatakiwa ziwe na sifa?
12.Unatambueje sifa za kuchagua mbuzi bora
13.Mbuzi wanafaa kwa ajili ya matakwa gani
katika jamii ? utachaguaje mbuzi kwa ajili ya
ufugaji ?
3. JOSEPH LILO AFISA MIFUGO -0765096371,0768287853. JORENO VEGETABLE LEATHER TANNINGpg. 3
SIFA ZA ZIADA KWA MBUZI WA MAZIWA
NA DUME
14. Mbuzi anatakiwa kuwa na miguu ya
nyuma iliyo imara na iliyonyooka na
yenye nguvu na nafasi kwa ajili ya
kiwele, ni lazima awe na kiwele kikubwa
na chuchu ndefu zilizokaa vizuri.
15. Dume la mbuzi linatakiwa kuwa na sifa
kama vile miguu iliyonyooka,asiwe na
ulemavu wa aina yeyote, mwenye
uwezo na nguvu ya kupanda, mwenye
kokwa mbili zilizokaa vizuri na
zinazolingana. Dume linapaswa
kuchaguliwa vizuri na kwa umakini wa
hali ya juu kwasababu dume ni nusu ya
kundi.
UTUNZAJI WA VITOTO VYA MBUZI.
16. Utunzaji wa watoto wa mbuzi huanza
mara tu wanapozaliwa. Kitoto
kinapaswa kupatiwa maziwa ya
mwanzo yani ndang’a masaa mawili
tangu kuzaliwa kwa muda wa siku tatu
mfululizo. Kama kinanyweshwa maziwa
kipewe lita 0.7 – 0.9 kwa siku maziwa
haya ni muhimu kwani yana viini lishe
na kinga dhidi ya magonjwa.
17. Iwapo mama hatoi maziwa au amekufa
inashauriwa kutengeneza ndang’a
badala au kama kuna mbuzi mbadala
aliyezaa anaweza kusaidia kunyonyesha
kitoto cha mbuzi. Kitoto cha mbuzi
kinyonyeshwe kwa wiki 12-16 wiki ya
pili baada ya kuzaliwa pamoja na
maziwa kianze kupewa vyakula vingine
kama nyasi laini na chakula cha ziada ili
kusaidia kukua kwa tumbo na kipewe
14,15. Ni sifa zipi za mbuzi wa maziwa na
Dume la mbuzi?
16.Ni mahitaji gani anapaswa kupewa kitoto
cha mbuzi baada tu yakuzaliwa
maji safi wakati wote na vyombo
vinavyotumka kulishia view safi wakati
wote.
18. Kitoto cha mbuzi kikifikisha umri
unaofaa kinapaswa kuachishwa
kunyonya. Umri wa kuachishwa
kunyonya ni miezi mitatu hadi nne
kutokana na hali ya mnyama au
kutegemea afya ya mnyama. Na
mwisho kitoto kipatiwe kinga na tiba ya
magonjwa.
19. Mbuzi huwekewa alama ili atambulike
kwa urahisi na kuwezesha utunzaji wa
kumbu kumbu zake. Shughuli hii
hufanyika kwa mbuzi akiwa na umri wa
siku 3-14. Kuweka alama sikioni kwa
kukata sehemu ndogo ya sikio,kuwapa
majina kwa wale wenye mbuzi
wachache, kumvisha herein ya chuma
au ya pastiki yenye namba kwenye sikio
au kumvalisha mkanda wenye namba
shingoni na kuweka alama ya chapa ya
moto kwenye ngozi ya mnyama hasa
sehemu ambazo hazitaadhiri ubora wa
ngozi.
KUONDOA VISHINA VYA PEMBE NA KUASI.
20. Umri wa kuondoa vishina vya pembe
vya mbuzi ni kati ya siku 3-14.
Visipoondolewa hukua na kusababisha
kuumizana na kuhitaji nafasi kubwa
kwenye banda.Vitoto vya mbuzi
ambavyo havitatumika kwa ajili ya
kuendeleza kizazi vihasiwe kabla ya
kufikia umri wa miezi 3.
17.Eleza jinsi ya kulea kitoto cha mbuzi mpaka
kufikia hatua ya kula majani.
18.Ni muda gani kitoto cha mbuzi kinapaswa
kuachishwa kunyonya?
19.Ili kutambaua utambulisho kwa mnyama
mbuzi anapaswa kuwekwa alama akiwa na
umri gani?
20. Taja Umri wa kutoa vishina vya pembe na
kuasi mbuzi
4. JOSEPH LILO AFISA MIFUGO -0765096371,0768287853. JORENO VEGETABLE LEATHER TANNINGpg. 4
UTUNZAJI WA MBUZI WA MIEZI 4-8 NA UMRI
WA KUPANDISHA
21. Mbuzi wa miezi 4-8 ni wale ambao
wameacha kunyonya mpaka umri wa
kupandishwa kwa mara ya kwanza.
Mbuzi wa umri huu wanauwezo wa kula
aina mbali mbali za malisho kama
nyasi,mikunde,miti malisho na mbaki ya
mazao kutoka shambani. Wakati wa
kiangazi uhitaji wa kupatiwa chakula
cha ziada au kupewa pumba za nafaka
mbali mbali, mashudu ya alizeti,pamba
na dengu,majani ya mikunde
yaliyokaushwa, madini na vitamini.
22. Katika ufugaji huria ni vema kuzingatia
idadi ya mbuzi inayoweza kuchungwa
katika eneo aina na hali ya malisho. Ili
mbuzi aweze kukua na kufikia uzito wa
kuchinjwa mfugaji anapaswa kufuata
kanuni za ufugaji bora kama kumpatia
mbuzi vyakula vya ziada kwa muda
wamiezi 2 mfululizo kiasi cha kilo 0.2 –
0.7 kwa siku kuanzia anapoachishwa
kunyonya, kumpatia dawa za kuzuia
minyoo kila baada ya miezi mitatu na
kutoa kinga za magonjwa mengine,
kuchanja na kuogesha ili kuzuia
magojwa mbali mbali, kukata kwato
mara zinapokuwa ndefu na kuasi
madume yale yasiyotumika kwa
kuzalisha.
23. Mbuzi akitunzwa vizuri anaweza
kupandishwa akiwa na umri wa miezi 8-
12 kwa mbuzi aliyeboreshwa na miezi
18 hadi 24 kwa mbuzi wa asili
kutegemea na afya yake. Hata hivyo
inashauriwa wapandishwe wanapofikia
uzito wa kilo 12 au Zaidi na
wasipandishwe mbuzi wa ukoo mmoja.
21,22. Eleza jinsi ya kumtunza mbuzi mwenye
umri wa miezi 4-8
23.Taja umri wa kupandisha mbuzi
walioborehswa na waasili.
DALILI ZA MBUZI MWENYE JOTO.
24. Mfugaji anashauriwa asipandishe jike
kabla hajafikisha umri wakupandwa wa
miezi 8 – 12 kwa mbuzi walioborehswa
na miezi 18 – 24 kwa mbuzi wa asili
hata kama ataonyesha dalili ya kutaka
kupandwa. Mbuzi aliye kwenye joto
huonyesha dalili zifuatazo; hufuata
dume,huangaika mara kwa mara na
kupiga kelele, hutoa ute mweupe
ukeni,hupanda na kukubali kupandwa
na wengine, hutingisha au kuchezesha
mkia wake, hamu ya kula hupungua,
kukojoa mara kwa mara, uke huvimba
na kuwa na kuwa wekundu isivyo
kawaida na kwa mbuzi anayekamuliwa
hupunguza kiwango cha uzalishaji
maziwa
25. Mbuzi apelekwe kwa dume mara tu
dalili za joto zinapoonekana kwani joto
hudumu kwa wastani wa siku 2 ausaa
48 chunguza tena dalili za joto baada ya
siku 19-21 na kama dalili hazijaonekana
tena kuna uwezekano mkubwa kuwa
mbuzi amepata mimba. Mfugaji apange
msimu mzuri wa mbuzi kuzaa. Msimu
mzuri ni mara baada ya mvua.
UTUNZAJI WA MBUZI MWENYE MIMBA.
26. Kwa kawaida mbuzi hubeba mimba kwa
muda wa miezi 5. Utunzaji wa mbuzi
mwenye mimba ni muhimu kwani ndiyo
chanzo cha kupata vitoto vyene afaya
bora. Mfugaji anashauriwa kufuata
kanuni zifuatazo; mbuzi apatiwe
vyakula vya ziada kilo 0.2 – 0.7 kwa siku
ili kutosheleza mahitaji yake na kitoto
kinachokuwa tumboni. Mbuzi apatiwe
nyasi miti,miti malisho na mikunde
mchanganyiko kilo 1.8 – 2.5 kwa siku.
24,.Taja dalili za mbuzi mwenye joto.
25.Ni muda gani mbuzi jike anapaswa
kupelekwa kwa dume
26.Ni mahitaji gani ambayo mbuzi mwenye
mimba hupatiwa?
DALILI ZA MBUZI ANAYEKARIBIA KUZAA
5. JOSEPH LILO AFISA MIFUGO -0765096371,0768287853. JORENO VEGETABLE LEATHER TANNINGpg. 5
27. Huangaika kwa kulala na kuamka mara
kwa mara, sehemu yanje ya uke wa
mbuzi hulegea, hujitenga na kundi na
hutafuta sehemu kavu na yenye
kivuli,kupiga kelele, hutokwa na ute
mzito ukeni. Mfugaji akiona dalili hizi
anashauriwa asimruhusu mbuzi kwenda
machungaji bali amtenge kwenye
chumba maalumu ampatie maji ya
kutosha na kumuandalia sehemu ya
kuzalia.
UTUNZAJI WA MBUZI ANAYENYONYESHA.
28. Mbuzi anayenyonyesha huitaji chakula
kingi Zaidi ili kukidhi mahitaji ya mwili
na kuzalisha maziwa kwa ajili ya
kitoto/vitoto. Pamoja na nyasi,
mikunde na majani ya miti malisho kilo
1.8 – 2.5 kwa siku ni muhimu apewe
chakula cha nyongeza kilo 0.3 – 0.8 kwa
kila lita ya maziwa inayoongezeka
baada ya lita 2, pia apewe maji safi nay
a kutosha wakati wote
TARATIBU YA KUZINGATIA KATIKA UKAMUAJI
WA MBUZI WA MAZIWA.
29. Kusudi la ufugaji wa mbuzi wa maziwa
ni kupata maziwa mengi, safi na salama
pamoja na mazao yatokanayo na
maziwa. Mambo muhimu ya kuzingatia.
Sehemu ya kukamulia iwe safi na yenye
utulivu,mbuzi awe na afya nzuri,msafi
na kiwele kioshwe kwa maji safi ya
vuguvugu, mkamuaji asibadilishwe
badilishwe awe msafi mwenye kucha
fupi na asiwe na magonjwa ya
kuambukiza,vyombo vya kukamulia
view safi na maziwa ya mwanzo kutoka
kila chuchu yakamuliwe kwenye
chombo maalumu (strip cup) ili
kuchunguza ugonjwa wa kiwele.
27. Ni dalili zipi za mbuzi kukaribia kuzaa ?
28.Unawezaje kumtunza mbuzi
anayenyonyesha?
29. Utazingatia mambo gani katika ukamuaji ?
UTUNZAJI WA DUME LA MBEGU.
30. Dume bora la mbegu ni muhimu
litunzwe ili liwe na uwezo wa kutoa
mbegu bora, kupanda na kuzalisha.
Dume bora huanza kupanda akiwa na
umri kati ya miezi 8- 10 kwa mbuzi
walioborehswa. Katika msimu wa
kupandisha dume moja liruhusiwe
kupanda majike 40 – 50. Aidha
inashauriwa madume wenye umri wa
miezi 8-9 waruhusiwe kupanda majike
ambao ndio mara ya kwanza kupandwa.
Dume anapaswa apatiwe malisho ya
kutosha na vyakula vya ziada kiasi
kisichopungua kilo 0.2 – 0.7 kwa siku na
maji ya kutosha, majani ya miti malisho,
mikunde, na nyasi mchanganyiko na
mabaki ya mazao, kilo 0.45 – 0.9 za
chakula cha ziada cha nyongeza kwa
siku kulingana na uzito wake na wingi
wa majike anayopanda. Wiki 2 kabla na
baada kuanza kupanda.
KUDHIBITI MAGONJWA YA MBUZI
31. Magonjwa husababishwa na vimelea
jamii ya virusi,bacteria, protozoa na
riketsia. Magonjwa mengine
husababishwa na upungufu wa viini
lishe, vitamin na protini
32. Dalili za mbuzi mgonjwa ni pamoja na
manyoya husimama,kuzubaa, kusinzia ,
kukohoa kukosa hamu ya kula na
kunywa maji, kujitenga na kundi,
kuvimba taya la chini, kupumua kwa
shida,kutokwa na machozi , makamasi
na utete mweupe kwenye macho, kuwa
na upele au uvimbe kwenye sehemu ya
mwili, kutupa
mimba,kuharisha,kukohoa na
kuchechemea.
30. Ni namna gani unaweza kutunza dume la
mbegu ?
31.Magonjwa katika mbuzi husababishwa na
vimelea gani?
32. Dalili za mbuzi mgonjwa ni zipi?
33. Mbuzi wachanjwe dhidi ya homa ya
mapafu. Ugonjwa huu ni hatari sana na
6. JOSEPH LILO AFISA MIFUGO -0765096371,0768287853. JORENO VEGETABLE LEATHER TANNINGpg. 6
huenea kwa njia ya hewa na unaweza
kusababisha vifo kati ya asilimia 60 –
100. Kila baada ya miezi 6 mifugo
ipatiwe kinga dhidi ya ugonjwa wa
miguu na midomo na magonjwa
mengine kama vile kimeta, bonde la
ufa, kutupa mimba na cha mbavu (BQ).
Kama kuna wagonjwa walioathirika
watengwe kwenye kundi wasisafirishwe
au kuuzwa.
34. Mbuzi wapatiwe dawaza minyoo. Vitoto
vya mbuzi vipatiwe dawa za minyoo
vinapofikia umri wa mwezi 1. Viendelee
kupatiwa dawa za minyoo kila mwezi
hadi wanapofikia umri wa miezi 5 na
baada ya hapo vipatiwe dawa minyoo
kila baada ya miezi 3 – 4. Zingatia usafi
ili kuwakinga na magonjwa ya kuharisha
na kuharisha damu na magonjwa mbali
mbali.
UTUNZAJI WA KUMBU KUMBU
35. Kuweka kumbu kumbu za mifugo ni
muhimu katika uzalishaji kwa ajili ya
kutambua koo safu, gharama za
utunzaji na faida. Pia humsaidia mfugaji
kufanya uamuzi katika uendelezaji wa
ufugaji wake. Na pia inasaidia
wataalamu wa utafiti kupata takwimu
kwa ajili ya utafiti wao n ahata inaweza
kumsaidia mfugaji kujua historia katika
shamba lake.
33.mbuzi anaweza kupata magonjwa gani?
34.mbuzi anaweza kupewa dawa za minyoo
kwa 35.kwanini kumbu kumbu ni muhimu
katika ufugaji wa mbuzi ?muda gani ?
KUMBU KUMBU MUHIMU ZINAZOTAKIWA
KUTUNZWA.
36. Kumbukumbu za idadi na ukuaji wa
wanyama waliopo,jinsia zao, uzito wa mbuzi
kwa kila mwezi ili kufuatilia ukuaji wake na
tarehe ya kuachishwa kunyonya na na idadi
waliouzwa. wa kuzaliwa.Kumbukumbu za uzazi
zinazoonyesha tarehe ya kuzaliwa, namba yake,
jinsia yake, aina au breed, namba ya dume au
jike na uzito wa kuzaliwa. Kumbu kumbu za
upandishaji zinazoonyesha namba ya mbuzi
anayepandwa, tarehe ya joto nay a kupandwa,
namba ya dume lililotumika kupanda, tarehe ya
joto la pili kama atarudia na tarehe ya kuzaa.
37. Pia kuna kumbu kumbu za chanjo na
matibabu zinazoonyesha namba ya mbuzi,
tarehe ya matibabu, aina ya chanjo au ugonjwa,
dawa iliyotumika, idadi ya waliokufa na
waliopona, kumbukumbu za uzalishaji maziwa
zinazoonyesha namba ya mbuzi, tarehe ya
kuzaa, kiasi cha maziwa kwa siku na kiasi cha
maziwa kwa kipindi chote cha kukamuliwa,
tarehe ya kuacha kukamuliwa na idadi ya siku
alizokamuliwa. Kumbu kumbu za mapato na
matumizi zinazoonyesha mapato na matumizi,
vitu vilivyouzwa au kununuliwa kwa siku, kiasi
cha fedha unachokuwa nacho kila wakati, kiasi
cha fedha unachodai na kudaiwa.
36,37. Ni kumbu kumbu zipi muhimu
zinazohitajiwa katika ufugaji wa mbuzi?